Magari ya Hybrid Kama toyota Aqua

Magari ya Hybrid Kama toyota Aqua

Clack-Sniper

Member
Joined
May 16, 2025
Posts
39
Reaction score
75
Hello wana jamii. Naomba kuuliza kama kuna mwenye uzoefu na uendeshaji wa Toyota AQUA hybrid. Hapa Tanzania experience ikoje?

Je ulaji wa mafuta ni kama wanavyoonyesha kwenye review za mtandaoni 24 - 35 Km/l?

Ufanyaje service je? Mnatumia oil gani. Maana recommended ni SAE 0w20. Ila kwa Hapa Dar ni Brand moja tu ndio ina 0w20. Unatumia oil gani?
 
Hello wana jamii. Naomba kuuliza kama kuna mwenye uzoefu na uendeshaji wa Toyota AQUA hybrid. Hapa Tanzania experience ikoje?

Je ulaji wa mafuta ni kama wanavyoonyesha kwenye review za mtandaoni 24 - 35 Km/l?

Ufanyaje service je? Mnatumia oil gani. Maana recommended ni SAE 0w20. Ila kwa Hapa Dar ni Brand moja tu ndio ina 0w20. Unatumia oil gani?
Ngoja waje tupate kudowea madini
 
Ufanyaje service je? Mnatumia oil gani. Maana recommended ni SAE 0w20. Ila kwa Hapa Dar ni Brand moja tu ndio ina 0w20. Unatumia oil gani?
Service unafanya kama magari mengine tu. Oil uko sawa 0W20 unaweza tumia Liquimolly au Atlantik. Mi natumia Atlantic nishabadirisha mara mbili na inaenda fresh.

Service ya hybrid sio issue ila ukiwa na OBDII unyama na ukawa na App mfano ya Dr. Prius kukiwa na issue unasolve. Kingine kusafisha tu cooling system ya hybrid battery.

Ulaji wa mafuta ni kweli kama ilivokua advertised. Msimu wa joto kama huu kidogo naona matumizi yanaongezeka kufika 22-24 ila msimu mzuri 28km/L hapa mjini bila kutumia nguvu.
 
Hello wana jamii. Naomba kuuliza kama kuna mwenye uzoefu na uendeshaji wa Toyota AQUA hybrid. Hapa Tanzania experience ikoje?

Je ulaji wa mafuta ni kama wanavyoonyesha kwenye review za mtandaoni 24 - 35 Km/l?

Ufanyaje service je? Mnatumia oil gani. Maana recommended ni SAE 0w20. Ila kwa Hapa Dar ni Brand moja tu ndio ina 0w20. Unatumia oil gani?
Kuna kampuni moja kule Kenya unayatumia sana.
Nimeona dashboard ya millage inasoma hadi 300k+ means ni magari mazuri sana.
 
Service unafanya kama magari mengine tu. Oil uko sawa 0W20 unaweza tumia Liquimolly au Atlantik. Mi natumia Atlantic nishabadirisha mara mbili na inaenda fresh.

Service ya hybrid sio issue ila ukiwa na OBDII unyama na ukawa na App mfano ya Dr. Prius kukiwa na issue unasolve. Kingine kusafisha tu cooling system ya hybrid battery.

Ulaji wa mafuta ni kweli kama ilivokua advertised. Msimu wa joto kama huu kidogo naona matumizi yanaongezeka kufika 22-24 ila msimu mzuri 28km/L hapa mjini bila kutumia nguvu.
Shukrani sana kwa mrejesho huu. Angalau napata Moyo maana nilifanya uamuzi wa kununua bila kujua Uhalisia wa Bongo.

Vipi kuhusu ground clearance, Uliinyenyua? Maana naona somehow iko chini
 
Shukrani sana kwa mrejesho huu. Angalau napata Moyo maana nilifanya uamuzi wa kununua bila kujua Uhalisia wa Bongo.

Vipi kuhusu ground clearance, Uliinyenyua? Maana naona somehow iko chini
Angalia unapokaa. Mimi nishazoea gari zinazotambaa siwezi gari za juu.

Badala ya kunyanyua, unaweza badirisha tyre. Ukaongeza profile. Sema itaongeza ulaji wa mafuta kidogo. Stock nyingi 60 unaweza kwenda 65 kama size ni R15 ila kama R14 nenda hadi 70.
 
Angalia unapokaa. Mimi nishazoea gari zinazotambaa siwezi gari za juu.

Badala ya kunyanyua, unaweza badirisha tyre. Ukaongeza profile. Sema itaongeza ulaji wa mafuta kidogo. Stock nyingi 60 unaweza kwenda 65 kama size ni R15 ila kama R14 nenda hadi 70.
Shukrani mkuu. Nimeijaribu naona siyo mbaya sana ila nadhani inbidi niweke tairi kubwa kidogo.

Vipi unaweza jua wapi naweza badili lugha ya redio kwenda Kiingereza. Radio yake ni NSCP-W61 nimeambiwa kuna mahali wanafanya kariakoo ila sijapata mawasiliano yake
 
Shukrani mkuu. Nimeijaribu naona siyo mbaya sana ila nadhani inbidi niweke tairi kubwa kidogo.

Vipi unaweza jua wapi naweza badili lugha ya redio kwenda Kiingereza. Radio yake ni NSCP-W61 nimeambiwa kuna mahali wanafanya kariakoo ila sijapata mawasiliano yake
Radio nyingi za JP hazinadirishiki lugha. Yaani wanaweza tengeneza same radio ila nyingine wakaiuza domestic JP tu. Hiyo inakua na navigation system ya JP tu na lugha yao wakati zile za international unakuta zina lugha nyingi.

Kama yako inabadirishika jaribu hii video YouTube ya sekunde chache tu. Ukiona option ya English haipo basi ujue ni JP tu. Jifunze kuishi nayo na if possible usiweke izo cheap Android za Kariakoo za Laki 2 sijui 3. Acha iyo iyo jifunze kutumia Google Translate jua kuconect simu basi imeisha.


View: https://youtu.be/qyWgur20RJc?si=6wZwa--mJ83lxTNP
 
Radio nyingi za JP hazinadirishiki lugha. Yaani wanaweza tengeneza same radio ila nyingine wakaiuza domestic JP tu. Hiyo inakua na navigation system ya JP tu na lugha yao wakati zile za international unakuta zina lugha nyingi.

Kama yako inabadirishika jaribu hii video YouTube ya sekunde chache tu. Ukiona option ya English haipo basi ujue ni JP tu. Jifunze kuishi nayo na if possible usiweke izo cheap Android za Kariakoo za Laki 2 sijui 3. Acha iyo iyo jifunze kutumia Google Translate jua kuconect simu basi imeisha.


View: https://youtu.be/qyWgur20RJc?si=6wZwa--mJ83lxTNP

Mkuu hivi kwa 12m inawezekana kupata gari aina hyo (hybrid) kutka japan adi kukufikia mkononi?
 
Hello wana jamii. Naomba kuuliza kama kuna mwenye uzoefu na uendeshaji wa Toyota AQUA hybrid. Hapa Tanzania experience ikoje?

Je ulaji wa mafuta ni kama wanavyoonyesha kwenye review za mtandaoni 24 - 35 Km/l?

Ufanyaje service je? Mnatumia oil gani. Maana recommended ni SAE 0w20. Ila kwa Hapa Dar ni Brand moja tu ndio ina 0w20. Unatumia oil gani?
Shida hizo gari kama zinatumia bettri kuendesha injini ,sio za kupelekea fundi jux
 
Radio nyingi za JP hazinadirishiki lugha. Yaani wanaweza tengeneza same radio ila nyingine wakaiuza domestic JP tu. Hiyo inakua na navigation system ya JP tu na lugha yao wakati zile za international unakuta zina lugha nyingi.

Kama yako inabadirishika jaribu hii video YouTube ya sekunde chache tu. Ukiona option ya English haipo basi ujue ni JP tu. Jifunze kuishi nayo na if possible usiweke izo cheap Android za Kariakoo za Laki 2 sijui 3. Acha iyo iyo jifunze kutumia Google Translate jua kuconect simu basi imeisha.


View: https://youtu.be/qyWgur20RJc?si=6wZwa--mJ83lxTNP

Ahaa hii nimeiona redio yake ni tofauti. So nadhani inabidi niishi nayo tu. Siyo mbaya sana
 
Service unafanya kama magari mengine tu. Oil uko sawa 0W20 unaweza tumia Liquimolly au Atlantik. Mi natumia Atlantic nishabadirisha mara mbili na inaenda fresh.

Service ya hybrid sio issue ila ukiwa na OBDII unyama na ukawa na App mfano ya Dr. Prius kukiwa na issue unasolve. Kingine kusafisha tu cooling system ya hybrid battery.

Ulaji wa mafuta ni kweli kama ilivokua advertised. Msimu wa joto kama huu kidogo naona matumizi yanaongezeka kufika 22-24 ila msimu mzuri 28km/L hapa mjini bila kutumia nguvu.
kwa ufupi ukinunua gari hakikisha unaweza troubleshoot vitu vidogo vidogo kabla hujafika kwa fundi.
Au nunua kabisa vifaa vya kufanya matengenezo.
Mafundi wetu badala ya kutengeneza huharibu, sehemu ya kutumia akili wao ni nyundo
 
Mkuu hivi kwa 12m inawezekana kupata gari aina hyo (hybrid) kutka japan adi kukufikia mkononi?
Mkuu. Unaweza lakini naona kama risk. Ila hapo mimi nitaipigia kura Honda Fit Hybrid GP1 (2013 kurudi nyuma). Ngoja tuone:

Nimecheki BF Nimeipata hii (sio cheapest, ila unaweza pata cheaper zaidi yake), hii ni 2011 Honda Fit Hybrid GP1.
IMG_4343.jpeg


Nikajaribu kucheki na TRA kuona gharama za kodi kwa gari iyo iyo nimepata kama Mil 6.8
IMG_4344.jpeg


Ila nimejaribu kuangalia miaka ya nyuma 2010 gari ilo ilo TRA nimepata Mil 6.4 na 2009 gari iyo iyo nimepata Mil 6.2.

Kwahiyo sweet spot hapo ni kutafuta Honda Fit Hybrid GP1 ya mwaka 2009 au 2010 (ambapo utatoa ushuru tuseme Mil 7 maximum) na JP ujitahidi upate nakunegotiate upate kwa Mil 6 kushuka chini, ili jumla ije Mil 13.

Sasa kuhusu Honda Fit Hybrid GP1, hii ni mild hybrid, inamaanisha Engine inafanya kazi muda wote gari likiwa ON ila battery ya hybrid inasaidia kuongeza nguvu ili kupunguza matumizi. Haina fuel consumption nzuri sana ila inatosha. Sometimes kununua mild hybrid naona bora ununue Honda Fit GK isio hybrid. Zinafanana ivyo ivyo na unaweza kupata cheaper ata jumla kwa Mil 12 au less.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom