Magari 1,000 yakwama mpaka wa Tunduma

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
Ikiwa ni siku ya pili tangu serikali ya Zambia kufunga mpaka, shughuli zote za mpakani zimesimama, hali iliyosababisha magari yaliyobeba mizigo kama chakula na mafuta kukwama kuendelea na safari.

Brigedia Jeneral Nicodemas Mwangela, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, jana alifika katika mpaka huo uliopo mji wa Tunduma, wilaya ya Momba, ambapo alijionea bidhaa mbalimbali zikiwa zimekwama kuvuka.

Aliwataka wasafirishaji mizigo hiyo kuwa na subira ambapo alisema kuna mazungumzo yanaendelea, na kwamba huenda mpaka huo ukafunguliwa mapema kufuatia makubaliano ya nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuzuia kufunga mipaka kabisa badala yake bidhaa muhimu kama mafuta na chakula viruhusiwe kuvuka.

Aidha, liwataka wasafilishaji kuondoa hofu kutokana na adhabu ambazo wanaweza kukumbana nazo kufuatia sheria ya kutokaa mpakani bila kuvuka kwa zaidi ya siku saba.

''Tunduma ni salama, Songwe ni salama hakuna haja ya wananchi kuwa na hofu, endeleeni kuchapa kazi,” alisema mkuu wa mkoa.

Juzi, serikali ya Zambia ilianza utekelezaji wa agizo hilo kwa kufunga mageti yote mawili ya kuingilia nchini humu pamoja na maduka, na shughuli zote zinazofanywa kwenye eneo la mpaka, hali iliyoibua vilio kwa wafanyabiashara wa mji wa Tunduma.

Wakizungumza baada ya utekelezaji wa agizo la kufunga mpaka, wafanyabiashara hao walisema kwa sasa wana mazingira magumu ya kumudu maisha yao kwani maisha ya mji wa Tunduma yanategemea sana biashara.

Neema Kalinga, mmoja wa wafanyabiashara waliofungiwa maduka, alisema hawana cha kufanya kwani walishindwa hata kuchukua chochote dukani kufuatia askari wa Zambia kufunga maduka yote majira ya alfajiri, na kwamba hakukutolewa taarifa yoyote kwa ajili ya kujiandaa na hatua hiyo.

Aliongeza serikali ya Zambia ilipaswa kutoa angalau siku moja kwa ajili ya wafanyabiashara kujiandaa kwani wangeweza hata kuhamisha bidhaa zo ili mpaka ukifungwa maisha mengine yaendelee.

George Kyando, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, alisema ulinzi mpakani umeimarishwa vya kutosha, na Watanzania waendelee na shughuli zao kama kawaida.

NIPASHE
 
Hapo boda ya tunduma kuna uhuni unafanyika. Hebu piga hesabu hapo boda ya zambia nakonde saizi wanasema wamewakuta wagonjwa 128 wa corona halafu asilimia kubwa ni watanzania. lakini cha ajabu upande wa pili kwenye boda ya Tanzania hakuna mgonjwa hata mmoja. na wakati huo asimilimia kubwa ya wagonjwa walio wakuta zambia walipita kwenye boda ya tunduma.

Sent from my SM-G975F using Tapatalk
 
Hapo mpakani sio salama means watu zaidi ya 1000 wamekusanyika hapo.

Ni kwanini viongozi wetu wanagoma kushiriki mazungumzo kama wenzetu wa SADC na EAC walivyofanya?
 
Mpaka serikal yenu iwe serious na hili gonjwa ndo mtapata ushirikiano na majirani, mambo hayawezi kwenda kiholela holela kama watanzania mnavyofanya.
 
Hapo boda ya tunduma kuna uhuni unafanyika

hebu piga hesabu hapo boda ya zambia nakonde saizi wanasema wamewakuta wagonjwa 128 wa corona halafu asilimia kubwa ni watanzania. lakini cha ajabu upande wa pili kwenye boda ya Tanzania hakuna mgonjwa hata mmoja. na wakati huo asimilimia kubwa ya wagonjwa walio wakuta zambia walipita kwenye boda ya tunduma.

Sent from my SM-G975F using Tapatalk
Upande wa tanzania wamepima wakakosa wagonjwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka serikal yenu iwe serious na hili gonjwa ndo mtapata ushirikiano na majirani, mambo hayawezi kwenda kiholela holela kama watanzania mnavyofanya.

Mkuu

Kuna mahala umeona serikali haiko serious na huu ugonjwa?

Unataka umakini upi ndiyo ujiridhishe kwamba serikali inachukua hatua stahiki kukabiliana na hii changamoto ya corona?

Kila mtu anapambana na changamoto zake kwa namna yake anayoiona iko sahihi. Tuachie serikali na mamlaka husika zifanye majukumu yake barabara.

Sisi kama wananchi tunalo jukumu la kuendelea kuchukua hatua zinazoelekezwa na mamlaka husika.

Shukrani


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Mimi bado kuna kitu kinanisumbua. Kwani hatua walizochukua Zambia wao haziwaathiri? Nilifikiri wao wangelia zadi yetu, ama?

Sasa ninashangaa Zambia yupo kimya as if haathiriki. Ni sisi ndiyo sasa viongozi wanahangaika kutafuta suluhisho. Ipoje hii?
 
Hapo boda ya tunduma kuna uhuni unafanyika. Hebu piga hesabu hapo boda ya zambia nakonde saizi wanasema wamewakuta wagonjwa 128 wa corona halafu asilimia kubwa ni watanzania. lakini cha ajabu upande wa pili kwenye boda ya Tanzania hakuna mgonjwa hata mmoja. na wakati huo asimilimia kubwa ya wagonjwa walio wakuta zambia walipita kwenye boda ya tunduma.

Sent from my SM-G975F using Tapatalk
Upande wa pili nani kakwambia kuna mtu kapimwa corona?
 
Wewe ngoja matokeo utayaona baada ya wiki 1
Hao hawafikishi mwezi watafungua.
Utakuja kuniambia.
Hivi toka mpaka umefungwa ni upande upi umelalamika? Yaani sisi tunataka kupambana na korona kwa style ambayo na wengine waifatishe hii sio sawa kama ilivyo sisi hatutaki kupangiwa na tusiwapangie wengine,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wazambia jana wametoroka kupitia chobingo kuja kununua bidhaa muhimu huku Tunduma...hali inatisha kwa kweli!
 
Zambia atafungua mpaka mwenyewe tu mji wa Tunduma ni muhimu sana kwa nchi zote 2 bila upendeleo..
 
Back
Top Bottom