sasa wanajamii kama mtu yuko kwenye chama na haruhusiwi kumtuhumu mwenzake ndani ya chama hicho hicho maana yake nini? Kumbe ndo maana mambo yanaharibika tu ndani ya chama kwa kuwa ni kosa kumwambia yule aliyekosea ukweli!!!! Hii ni kanuni au sheria gani katika karne hii tuliyomo jamani?? Hapa kweli panahitaji elimu kulijua hili kuwa ni tatizo ndani ya chama chetu jamani? Kwa nini wakuu mlioko kwenye CC hamlioni hili? Au kwa vile kanuni hizi zinafanikisha ninyi mlioko juu kuwa miungu watu kwenye chama chetu? kwa hali hii chama kikifa tutatafuta mchawi? Wakati sheria na kanuni zetu zinatuloga wenyewe? Jamani fungueni macho muone, mchana kweupe mnajifanya kufunga macho ili msione??? Mungu atawalaani asilani..........