Mafisadi kuhamia CHADEMA?

CHADEMA hawezi kwenda fisadi bana.

Fisadi akitoka CCM anahamia CUF NCCR, TLP au UDP bana kwani umeambiwa CHADEMA ni chama cha mikataba feki.

(CCM) wacha hizo bana fikiri hata kidogo ukipata information bana au unasemaje mkuu.

Hahaha, Jamaa Hii Alipost 2011, Nimeipitia Nkacheka
 
Wajiunge wapi mkuu!! Nape keshaanza kazi huyo au huijui nafasi yake kwenye Chama?
Chadema sio kichaka cha kupokea vilaza wakujivua GAMBA...huku wanakaa wazalendo walio tayari kwa lolote ilimradi waitetee Inji yao hayo ma GAMBA hayana nafasi huku.

naKUKUMBUSHA ULIIPOST MWAKA 2011
 
Huyu Dingi asipokelewe CDM. Tutakuwa tumepoteza dira endapo tutafanya hivyo. Maana isije tunakemea ufisadi kwa kuwa wako ccm na wakiwa cdm ni lulu la hasha tusithubutu kutenda kosa hilo la mapokezi ya EL.

Nani Wa Kumzuia? Nadhan Nyote Mlidhan Ni Uongo Kuwa Mbowe Atapokea Chochote Kuwakaribisha Lowassa And Coy, Sasa Umeona, Ulicoment Hapo Juu Mwaka 2011
 
We mkuu kweli uliaga kwenu!
Post ya 2011?
 
Hii itakuwa kituko cha karne. Ni sawa na Jeshi la Marekani lilipokwenda Iraq kuwatoa Baathists na Saadam Hussein, halafu wakamkamata Saadam na kuamua kumpa nafasi ya ujenerali kwenye jeshi la Marekani huko Iraq. Huo ni wehu.

umeonaee lowasa kupokelewa kimekuwa kituko cha karne maana ulipost hii mwaka 2011
 
Hii Ni Mwaka 2011 Hukujua Kama Mbowe Atapga Ela?

Mbowe anawachezea akili sana wafuasi wa chadema! Haya aliyapanga tangu 2011 alikuwa anangojea muda muafaka ambao wananchi watakuwa wameshika kasi ya kiu ya mabadiliko kiasi kwamba hawasikii la muadhini wala la mnadi swala, wao ni mabadiliko tu, hapo hapo ndio akapiga hela za fisadi na kuanza kumsafisha kwa nguvu zote! Kweli wananchi wanatumika vibaya!
 
CHADEMA ni daladala ya kisiasa.
Aliye na pesa anaikodisha kutekeleza matakwa yake!!
Lowasa kalipa mshikokwa Mbowe na mepewa kugombea kiti cha Urais na hana cheo chochote ndani ya CHADEMA.
Baada ya 25 OCT Lowasa akisha shindwa lazima kutakuwa na ugomvi mkubwa CHADEMA maana hela yake imepotea bure.

Si tumesikia jinsi mabilioni yanavyo kata hewa kuingia akaunti ya Mbowe huko Dubai na Hongkong?
 

Mfano wako au kilinganishi ya Daladala ni nzuri sana mkuu! Na si umesikia Lowassa kasema anarudi kuchunga ng'ombe akishindwa uchaguzi. Hana mpango wa kubaki kujenga chama au kuleta mabadiliko aliyoyahubiri! Ye alitaka urais na Chadema ilikuwa vehicle au platform yake. Kama ilivyotabiriwa 2011!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…