Mafao Ya Wafanyakazi Wa Jumuiya Ya Afrika Mashariki

UniqueTanganyika

New Member
Mar 21, 2008
4
0
Hivi kuna utata gani kuhusu mafao ya wafanyakazi wa iliyokuwa Jumuiya ya Afika Mashariki?Na je,wale wanaoambiwa mafaili yao hayaonekani nini hatima yao?
Hivi kama mtu faili lake halionekani sehemu aliyokuwa anafanyia kazi litaonekana wapi?Nyumbani kwake au kaburini kwake kwa wale waliofariki dunia?
Wafanyakazi wa baadhi ya mashirika yaliyokuwa miongoni mwa mashirika ya Jumuiya hiyo huwajubu waliokuwa wafanyakazi wa jumuiya hiyo au ndugu wa marehemu wa waliokuwa wafanyakazi wa mashirika hayo kuwa mafaili yao hayaonekani.
Mfano mzuri wa mashirika hayo ni TANZANIA PORT AUTHORITY.
Sasa kama mafaili hayaonekani ina maana walengwa ndiyo wamepoteza haki zao?Je,huu ni uzembe wa nani?Je,mamlaka na hazina wameandaa utaratibu gani kwa ajili ya malipo ya watu hawa?Je,kwa mtindo huu watu hawa watalipwa malipo sahihi kweli?

HAZINA KUU MNA TAARIFA YOYOTE KUHUSU MAFAILI YA WAFANYAKAZI WA ILIYOKUWA JUMUIYA AFRIKA YA MASHARIKI AMBAYO HAYAONEKANI?KAMA MNAYO MNAANDAA UTARATIBU GANI?
Mahali pazuri pa kuanzia ni TANZANIA PORT AUTHORITY kwani hawa watu inaelekea ni wazembe kwani hawajui hata kuweka records za wafanyakazi wao.Hawaelewi kuwa records za wafanyakazi ndiyo maisha yao?
Ikibidi watu wa records wote wawajibishwe kwani wamefanya kitengo hicho ndiyo sehemu yao ya kuchuma kwani kila anayeambiwa faili halionekani anaacha pesa ili litafutwe.Pamoja na pesa hizo mafaili yenyewe hayapatikani.

SERIKALI TAFADHALI INGILIENI HILI KWANI FAMILIA ZA WATU ZINASUMBUKA BILA SABABU YOYOTE.
 
Back
Top Bottom