Hili suala nadhani linaleta mjadala wakati ambapo hakuna ulazima wa mjadala huu...ni kweli wamachinga walikuwepo siku zote, lakini ni kweli pia wapo mitaani kinyume na sheria (au by laws) za jiji...utakumbuka kulikuwa na fukuza fukuza ya hapa na pale, lakini wakifukuzwa walikuwa wanarudi kwa kuwa kulikuwa hakuna dhamira ya kweli kwa viongozi wengi wa awamu ya nyuma...Hata bandarini mambo yalikuwa hivyo hivyo, makontena zaidi ya 2000 hayalipiwi ushuru, meli pia hazilipiwi ushuru, na kadhalika...kwa hiyo mambo mengi yalikuwa yamelala...Kwenye awamu iliyopita kulikuwa pia na bomoabomoa lakini utashi wa kisiasa ulikuwa mdogo...mimi binafsi siamini kuwa hiyo hamisha ya wamachinga ni suala kwamba eti kwa kuwa jiji lina madiwani wengi wa vyama vya upinzani...Kumbuka awamu ya JPM ni ya uzinagatiaji wa sheria, na ndiyo maana kuna 'majipu' yanatumbuliwa...cha kusisitiza hapa ni kuwa maeneo yatengwe ili wafanyabiashara ndogo ndogo wapate eneo la kufanya biashara zao...Haiwezekani mji ukawa kila barabara ni soko, no way...pale msimbazi wamachinga wanapanga bidhaa barabarani...nasikia upo wakati teksi dereva alimgonga kwa bahati mbaya muuza bidhaa ndogo ndogo pale msimbazi na akauawa na wamachinga wenye hasira...mtu huwezi kutoka nyumbani kwako na kwenda kutandaza bidhaa barabarani, ukiambiwa uondoke, unadai upewe eneo la kufanya biashara...mambo hayaendi hivyo, lazima kuwe na mipango na taratibu...mimi masuala haya huwa sihusishi na siasa...wawe ni CCM au CHADEMA au CUF au chama chochote sheria lazima zizingagatiwe...
Sidhani kama tunatofautiana ktk hili.
Mimi nimejiuliza tu, kwamba, ilikuwaje hawa watu waanze kupanga biashara ktk maeneo yasiyoruhusiwa kwa shughuli hizo na wakati huohuo mamlaka zinazohusika (serikali) ikiangalia tu hata imefika mahali hawa watu wamejipa uhalali na haki yao ya maeneo hayo?
Jamani serikali ni serikali tu hakuna cha serikali ya wakati ule sijui ilikuwa vile na eti ya sasa iko hivi.
Hapana. Tusiwatafutie excuse ktk hili kwa sababu hakuna nabadiliko yoyote ya sheria. Sheria na taratibu zilizokuwepo wakati ule ndizo hizi ambazo zipo hadi sasa, hazijabadilika!!
Halafu nimesema, pamoja na kwamba makosa yalifanyika kwa pande zote tangu wakati ule kwa maana ya hawa wamachinga kuvamia maeneo yasiyoruhusiwa kufanyia shughuli zao na kwa upande mwingine mamlaka zinazohusika kutozuia kuvunjwa kwa sheria mapema hata sasa tatizo limekuwa kubwa na sugu;
Basi ni kwa nini Baraza la madiwani na Mkurugenzi huyu anayesemwa kuwa ni wa manispaa ya Ilala watofautiane ktk kurekebisha tatizo hili? Hili ndilo tatizo jingine linalotaka kuzalishwa ....... yaani tatizo juu ya tatizo!!
Kwa mwendo huu wa kutunishiana misuli, hawafiki popote na watavurugana tu lazima. Na popote palipo na vurugu, hakuna maendeleo....!!
Narudia tena kusema, kwamba, hawa wote walishakubaliana namna bora ya kutatua tatizo hili, lakini kuna kidudu mtu anataka kuwakoroga kwa sbb anazozijua yeye.
Na bila kupepesa macho, kuna uwezekano mkubwa kidudu mtu huyu akawa si mwingine zaidi ya serikali kuu ya mkoa wa DSM inayoongozwa na CCM kupitia RC Makonda!!
Na kama wataendelea hivi, basi ni wazi watavurugana sana tu to the point ya kusababisha violence hata maumivu kwa baadhi ya watu na kuwachanganya zaidi hao wanaowaongoza - wamachinga!!