Madiwani Ilala wampinga Mkurugenzi juu ya machinga

Madiwani Ilala wampinga Mkurugenzi juu ya machinga

Hawa madiwani nadhani hawatarudi kwenye uchaguzi ujao...watu wengi jijini Dar es Salaam wanataka machinga waache kutandaza bidhaa barabarani, sasa madiwani wanaleta siasa, shauri yao.

Kwani madiwani wamepinga wamachinga kuondolewa? Au wanataka waondolewe kwa utaratibu?
 
Siasa hutawala sana vichwa vya viongozi wetu kuliko utendaji, kila upande hapa unatunisha misuli kwa maslahi ya kichama, machinga ni kero kubwa kwa watumiaji wa barabara iwe waenda kwa miguu au wenye vyombo vya usafiri, nasikitika sana kuona madiwani wanatetea watu wanaovunja sheria hata kama ni wapigakura wao, kumbukeni hata sisi wengine tunaotukanwa au kutolewa maneno ya kuudhi tunapokanyaga mali za machinga walizopanga barabarani kwa bahati mbaya ni wapigakura wenu. Kwa wale wanaojitambua kwa mtu kumtetea mvunja sheria za Nchi kwa masilahi ya kisiasa, anapata mashaka na uwezo wenu ikiwa mtakabidhiwa madaraka makubwa ktk Nchi hii.
 
Hapo umenena na wakuakikisha hizo sheria ndogo zinafuatwa ni madiwani sasa utaratibu umeshawekwa ni nini sasa mkurugenzi anakuja kuingilia?
Hapo umenena na wakuakikisha hizo sheria ndogo zinafuatwa ni madiwani sasa utaratibu umeshawekwa ni nini sasa mkurugenzi anakuja kuingilia?


Ni lazima tusome kazi na wajibu wa madiwani upi na pia kazi na wajibu wa mkurugenzi mtendaji ni upi...haya ndiyo mambo ya kufahamu...tufahamu mkurugenzi mtendaji anateuliwa na nani na anawajibiks kwa nani...tufahamu mkurugenzi mtendaji akikosea anawajibishwa na nani...
 
Kwanza ifahamike hawa jamaa ni hatari walishaua raia mwema just kwa kukanyaga nyanya! Tufike mahali tuseme inatosha tustaarabike sio kuishi kama wakimbizi
 
Ukawa waache siasa
Ili Dar iwe safi inabidi Machinga waondolewe
Mi hilo naungana na ccm
CCM waache kumtumia mkurugenzi kuharibu usimamizi wa manispaa ya Ilala! Waachie madiwani washirikiane na machinga kuona namna nzuri ya kuwahamisha!
 
CCM waache kumtumia mkurugenzi kuharibu usimamizi wa manispaa ya Ilala! Waachie madiwani washirikiane na machinga kuona namna nzuri ya kuwahamisha!
Mkuu kuna sehemu nyingine unaifahamu ya kuwapeleka hao machinga zaidi ya maeneo yaliyoainishwa?
 
Ukawa waache siasa
Ili Dar iwe safi inabidi Machinga waondolewe
Mi hilo naungana na ccm
Mheshimiwa ruhusu akili yako ifanye kazi kidogo, hawajapinga machinga kuondolewa ila walisheweka utaratibu kuwa kabla ya kuwapeleka huko wanakotaka waende ni vizuri waweke miundombinu iliyo sawa. Sasa unapeleka mtu sehemu ambayo haina choo au maji, utakuwa na akili sawa. Hacha kukurupuka mzee mambo mengine kuna haja ya kuyakubali hata kama yametolewa na adui yako.
 
Ukawa waache siasa
Ili Dar iwe safi inabidi Machinga waondolewe
Mi hilo naungana na ccm

Unaungana na CCM? kwani kuondoa wamachinga ni sera ya CCM? wangekuwa na sera hiyo tungefika hapa tulipo?
 
Hata mimi nasubiri kwa hamu nijue kama kweli UKAWA wataweza kuutafuna huu mfupa ambao CCM uliwashinda. Kuwaondoa wamachinga si kazi rahisi kama wanavyofikiri. Hakuna siasa hapo, ni lazima tu kutumia nguvu. Ni kama kujaribu kuwaondoa wapiga debe, hawa watu kama hujatumia nguvu huwezi kupata kitu.
 
Mkuu kuna sehemu nyingine unaifahamu ya kuwapeleka hao machinga zaidi ya maeneo yaliyoainishwa?
Kutaja maeneo siyo hoja, hoja ni utaratibu gani wa kuwaondoa unatumika? Pia ruhusu halmashauri yako ya kichwa ifanye kazi, maana madiwani wanasema hayo siyo maazimio yao ya full council na pia kule anakotaka waende miundombinu haijakamilika! Sasa utapelekaje soko mahali ambako hakuna vyoo? Anataka machinga wafe kwa kipindupindu?
 
Wabadilishe na ile Machinga complex kuwa parking ili jiji lipate mapato.
 
Madiwani wote sio Dar tu acheni siasa barabara zimejengwa kwa ajili ya magari
na pembeni mwa barabara kwa ajili ya waendao kwa miguu biashara zifanyike sokoni na kwenye majumba ya biashara mitaa ya miji sio kutandaza bidhaa barabani.
Hao wamachinga wamekuwepo hata kabla haujazaliwa, sasa leo ndo umewaona kero? Acha kukurupuka, CCM waliwaweka wenyewe sasa ndo imekuwa nongwa wakati wa UKAWA? Acha utaratibu ufuatwe wakati wa kuwatoa kuliko kutumia nguvu
 
Kutaja maeneo siyo hoja, hoja ni utaratibu gani wa kuwaondoa unatumika? Pia ruhusu halmashauri yako ya kichwa ifanye kazi, maana madiwani wanasema hayo siyo maazimio yao ya full council na pia kule anakotaka waende miundombinu haijakamilika! Sasa utapelekaje soko mahali ambako hakuna vyoo? Anataka machinga wafe kwa kipindupindu?
Kwa fununu uzijuazo madiwani walikubaliana nini ktkt maazimio yao
 
Hao wamachinga wamekuwepo hata kabla haujazaliwa, sasa leo ndo umewaona kero? Acha kukurupuka, CCM waliwaweka wenyewe sasa ndo imekuwa nongwa wakati wa UKAWA? Acha utaratibu ufuatwe wakati wa kuwatoa kuliko kutumia nguvu
Nadhani hujui nina umri gani na ni utaratibu gani huo ufuatwe na nijuavyo utaratibu huo utabaki kwenye mafaili na yawezekana wee ni miongoni mwa wanaolalamikia serikali kuhusu uchafu katika miji yetu wakati huohuo ndio mnaacha uchafu huo barabarani na mitaro kuziiba,acheni hizo siasa za kuwatetea eti wapiga kura wangu.
 
Hili suala nadhani linaleta mjadala wakati ambapo hakuna ulazima wa mjadala huu...ni kweli wamachinga walikuwepo siku zote, lakini ni kweli pia wapo mitaani kinyume na sheria (au by laws) za jiji...utakumbuka kulikuwa na fukuza fukuza ya hapa na pale, lakini wakifukuzwa walikuwa wanarudi kwa kuwa kulikuwa hakuna dhamira ya kweli kwa viongozi wengi wa awamu ya nyuma...Hata bandarini mambo yalikuwa hivyo hivyo, makontena zaidi ya 2000 hayalipiwi ushuru, meli pia hazilipiwi ushuru, na kadhalika...kwa hiyo mambo mengi yalikuwa yamelala...Kwenye awamu iliyopita kulikuwa pia na bomoabomoa lakini utashi wa kisiasa ulikuwa mdogo...mimi binafsi siamini kuwa hiyo hamisha ya wamachinga ni suala kwamba eti kwa kuwa jiji lina madiwani wengi wa vyama vya upinzani...Kumbuka awamu ya JPM ni ya uzinagatiaji wa sheria, na ndiyo maana kuna 'majipu' yanatumbuliwa...cha kusisitiza hapa ni kuwa maeneo yatengwe ili wafanyabiashara ndogo ndogo wapate eneo la kufanya biashara zao...Haiwezekani mji ukawa kila barabara ni soko, no way...pale msimbazi wamachinga wanapanga bidhaa barabarani...nasikia upo wakati teksi dereva alimgonga kwa bahati mbaya muuza bidhaa ndogo ndogo pale msimbazi na akauawa na wamachinga wenye hasira...mtu huwezi kutoka nyumbani kwako na kwenda kutandaza bidhaa barabarani, ukiambiwa uondoke, unadai upewe eneo la kufanya biashara...mambo hayaendi hivyo, lazima kuwe na mipango na taratibu...mimi masuala haya huwa sihusishi na siasa...wawe ni CCM au CHADEMA au CUF au chama chochote sheria lazima zizingagatiwe...

Sidhani kama tunatofautiana ktk hili.

Mimi nimejiuliza tu, kwamba, ilikuwaje hawa watu waanze kupanga biashara ktk maeneo yasiyoruhusiwa kwa shughuli hizo na wakati huohuo mamlaka zinazohusika (serikali) ikiangalia tu hata imefika mahali hawa watu wamejipa uhalali na haki yao ya maeneo hayo?

Jamani serikali ni serikali tu hakuna cha serikali ya wakati ule sijui ilikuwa vile na eti ya sasa iko hivi.

Hapana. Tusiwatafutie excuse ktk hili kwa sababu hakuna nabadiliko yoyote ya sheria. Sheria na taratibu zilizokuwepo wakati ule ndizo hizi ambazo zipo hadi sasa, hazijabadilika!!

Halafu nimesema, pamoja na kwamba makosa yalifanyika kwa pande zote tangu wakati ule kwa maana ya hawa wamachinga kuvamia maeneo yasiyoruhusiwa kufanyia shughuli zao na kwa upande mwingine mamlaka zinazohusika kutozuia kuvunjwa kwa sheria mapema hata sasa tatizo limekuwa kubwa na sugu;

Basi ni kwa nini Baraza la madiwani na Mkurugenzi huyu anayesemwa kuwa ni wa manispaa ya Ilala watofautiane ktk kurekebisha tatizo hili? Hili ndilo tatizo jingine linalotaka kuzalishwa ....... yaani tatizo juu ya tatizo!!

Kwa mwendo huu wa kutunishiana misuli, hawafiki popote na watavurugana tu lazima. Na popote palipo na vurugu, hakuna maendeleo....!!

Narudia tena kusema, kwamba, hawa wote walishakubaliana namna bora ya kutatua tatizo hili, lakini kuna kidudu mtu anataka kuwakoroga kwa sbb anazozijua yeye.

Na bila kupepesa macho, kuna uwezekano mkubwa kidudu mtu huyu akawa si mwingine zaidi ya serikali kuu ya mkoa wa DSM inayoongozwa na CCM kupitia RC Makonda!!

Na kama wataendelea hivi, basi ni wazi watavurugana sana tu to the point ya kusababisha violence hata maumivu kwa baadhi ya watu na kuwachanganya zaidi hao wanaowaongoza - wamachinga!!
 
Hao madiwani

Hao madiwani wamewahi kupita Kariakoo na hasa mtaa wa Msimbazi wakaona hadha?
Wamepita zaidi ya hamsini iliyopita mpaka sasa bado wanapita.
Tangia utawala wa ccm Dar mpaka utawala Chadema Dar machinga walikuwepo mitaani .
Ccm haijawahi kuwatoa sasa kihelehele cha nini?
Baada ya kupigwa chini Dar mnajifanya mnalipenda jiji?
Haiwasaidii kitu nyie magamba na hamtakaa mshike hili jiji tena kwa tabia yenu hiyo.
 
Wamepita zaidi ya hamsini iliyopita mpaka sasa bado wanapita.
Tangia utawala wa ccm Dar mpaka utawala Chadema Dar machinga walikuwepo mitaani .
Ccm haijawahi kuwatoa sasa kihelehele cha nini?
Baada ya kupigwa chini Dar mnajifanya mnalipenda jiji?
Haiwasaidii kitu nyie magamba na hamtakaa mshike hili jiji tena kwa tabia yenu hiyo.
Sawa, lakini tuangalie hali halisi ili tuboreshe jiji na kuimarisha afya za wakazi wa Jiji.
 
Back
Top Bottom