Madiwani Ilala wampinga Mkurugenzi juu ya machinga

Madiwani Ilala wampinga Mkurugenzi juu ya machinga

Ndio maana UKAWA wameshinda NA kuonhoza jiji kwa kuwa Serikali soku zote imejuwa hautendi haki kwa Machinga. Ni vema taratibu na ushikishwaji ufanyike ili ufunbuzi was pamoja na kudumu was suala hiki ufanyike.
Hizi operesheni zinaendeshwa kinyanyasaji mno.
 
Hawa madiwani nadhani hawatarudi kwenye uchaguzi ujao...watu wengi jijini Dar es Salaam wanataka machinga waache kutandaza bidhaa barabarani, sasa madiwani wanaleta siasa, shauri yao.

Hivi hawa wamachinga wameanza kufanyia shughuli zao ktk maeneo hayo mara baada ya uchaguzi mwaka jana?

Je, si kwamba walikuwepo miaka na miaka wakifanya shughuli zao ktk maeneo hayo tangu manispaa hizo zikiongozwa na CCM?

Hao CCM walichukua hatua gani kuwaandalia maeneo maalumu kama ambavyo sasa inafanyika chini ya usimamizi wa uongozi mpya wa manispaa hizi?

Sidhani kama ishu hapa ni Mkurugenzi au Mayor/baraza la madiwani. Mimi kwa mtazamo wangu hawana haja yoyote ya kutofautiana rather waandae timeframe ya kutekeleza hilo.

Lazima tukubaliane kuwa hawa ni binadamu walikuwa wanafanya shughuli zao halali ambazo pengine mpaka serikali ilikuwa inakusanya kodi zake kutoka kwao.

Sema tu kuwa walikuwa wanafanyia shughuli zao ktk maeneo yasiyo rasmi kwa shughuli. Na hii ndiyo inazaa swali la kwanini mamlaka zinazohusika zilishindwa kuzuia uvamizi huo mapema hata watu hao kujiona kuwa hiyo ni haki yao?

Baraza la madiwani nadhani limeona hili na kimsingi linakubaliana na maamuzi ya mkurugenzi. Wanatofautiana ktk namna ya kulitekeleza tu. Mkurugenzi hayuko sahihi ktk hili.

Mm ninahisi hili ni shinikizo la kisiasa toka kwa waliomteua, kwamba apindue maamuzi halali ya baraza la madiwani!!
 
Hivi hawa wamachinga wameanza kufanyia shughuli zao ktk maeneo hayo mara baada ya uchaguzi mwaka jana?

Je, si kwamba walikuwepo miaka na miaka wakifanya shughuli zao ktk maeneo hayo tangu manispaa hizo zikiongozwa na CCM?

Hao CCM walichukua hatua gani kuwaandalia maeneo maalumu kama ambavyo sasa inafanyika chini ya usimamizi wa uongozi mpya wa manispaa hizi?

Sidhani kama ishu hapa ni Mkurugenzi au Mayor/baraza la madiwani. Mimi kwa mtazamo wangu hawana haja yoyote ya kutofautiana rather waandae timeframe ya kutekeleza hilo.

Lazima tukubaliane kuwa hawa ni binadamu walikuwa wanafanya shughuli zao halali ambazo pengine mpaka serikali ilikuwa inakusanya kodi zake kutoka kwao.

Sema tu kuwa walikuwa wanafanyia shughuli zao ktk maeneo yasiyo rasmi kwa shughuli. Na hii ndiyo inazaa swali la kwanini mamlaka zinazohusika zilishindwa kuzuia uvamizi huo mapema hata watu hao kujiona kuwa hiyo ni haki yao?

Baraza la madiwani nadhani limeona hili na kimsingi linakubaliana na maamuzi ya mkurugenzi. Wanatofautiana ktk namna ya kulitekeleza tu. Mkurugenzi hayuko sahihi ktk hili.

Mm ninahisi hili ni shinikizo la kisiasa toka kwa waliomteua, kwamba apindue maamuzi halali ya baraza la madiwani!!

Hili suala nadhani linaleta mjadala wakati ambapo hakuna ulazima wa mjadala huu...ni kweli wamachinga walikuwepo siku zote, lakini ni kweli pia wapo mitaani kinyume na sheria (au by laws) za jiji...utakumbuka kulikuwa na fukuza fukuza ya hapa na pale, lakini wakifukuzwa walikuwa wanarudi kwa kuwa kulikuwa hakuna dhamira ya kweli kwa viongozi wengi wa awamu ya nyuma...Hata bandarini mambo yalikuwa hivyo hivyo, makontena zaidi ya 2000 hayalipiwi ushuru, meli pia hazilipiwi ushuru, na kadhalika...kwa hiyo mambo mengi yalikuwa yamelala...Kwenye awamu iliyopita kulikuwa pia na bomoabomoa lakini utashi wa kisiasa ulikuwa mdogo...mimi binafsi siamini kuwa hiyo hamisha ya wamachinga ni suala kwamba eti kwa kuwa jiji lina madiwani wengi wa vyama vya upinzani...Kumbuka awamu ya JPM ni ya uzinagatiaji wa sheria, na ndiyo maana kuna 'majipu' yanatumbuliwa...cha kusisitiza hapa ni kuwa maeneo yatengwe ili wafanyabiashara ndogo ndogo wapate eneo la kufanya biashara zao...Haiwezekani mji ukawa kila barabara ni soko, no way...pale msimbazi wamachinga wanapanga bidhaa barabarani...nasikia upo wakati teksi dereva alimgonga kwa bahati mbaya muuza bidhaa ndogo ndogo pale msimbazi na akauawa na wamachinga wenye hasira...mtu huwezi kutoka nyumbani kwako na kwenda kutandaza bidhaa barabarani, ukiambiwa uondoke, unadai upewe eneo la kufanya biashara...mambo hayaendi hivyo, lazima kuwe na mipango na taratibu...mimi masuala haya huwa sihusishi na siasa...wawe ni CCM au CHADEMA au CUF au chama chochote sheria lazima zizingagatiwe...
 
Waondolewe kwani jiji limekuwa kama gulio kero kila kona! Sasa hawa wafanyabiashara wa "efd"watafanyaje biashara kama wamachinga wameziba kila kona na hawalipi kodi?? Tuwe wakweli tuache siasa! Mkurugenzi wengi tuko nyuma yako! Simamia sheria kariakoo ni kero sana kwa sasa
 
Ukawa waache siasa
Ili Dar iwe safi inabidi Machinga waondolewe
Mi hilo naungana na ccm
Nimesoma kwa makini madiwani na Meya wako sahihi. Huwezi mpeleka mfanyabiashara mahali mpaka pawe conducive kufanya biashara. Kumbuka kama unavyokwenda ofisini Posta au Mlimani City ili upate mshahara, basi nao hapo ndipo ofisi yao ilipo.

So wawatengezee mahali pazuri kisha wawape deadline. Watakaokaidi wafikishwe mbele ya mahakama, nukta! Hayo mambo ya Ukawa na porojo zingine za kisiasa peleka huko. Acha serikali zifanye kazi kwa weledi.
 
Katika hili Mkurugenzi kakurupuka inapaswa yaandaliwe mzingira mazuri kule watakapohamia kwanza Ukawa wapo sahihi, ifanyike kama hile ya ubungo to mawasiliano
 
Waondolewe kwani jiji limekuwa kama gulio kero kila kona! Sasa hawa wafanyabiashara wa "efd"watafanyaje biashara kama wamachinga wameziba kila kona na hawalipi kodi?? Tuwe wakweli tuache siasa! Mkurugenzi wengi tuko nyuma yako! Simamia sheria kariakoo ni kero sana kwa sasa
Mkuu Hili tatizo lisingekuwepo kama wakuu wa jiji wasingehozi vizimba Machinga Complex
 
Na hizo barabara nizawananchi
Barabara ni za wananchi kwa ajili ya kupita na sio biashara, utalia chakula chooni kisa ni chako....badilika na anza kufikiri kama mtu anayejielewa la sivyo hii nchi itaenda mbele na wengi wenu mtabaki nyuma!
 
Huku kutetea upuuzi kwa sababu za kisiasa kutaisha lini? wanachojali hapa ni kuonekana wanatetea raia kumbe wasijue maisha bora ni pamoja na kuishi kwa mpangilio, au labda tumekuwa watu wa ovyo kiasi kwamba ishu za usafi, kufuata utaratibu na mpangilio wa maeneo sio muhimu tena kwetu.....sikutegemea kama kuna watu wangepinga busara kama hizi, ama kweli nchi isipoendelea si kwa bahati mbaya, ni wazi nchi hii ujinga umekithiri!!
 
NI LAZIMA TUFIKE MAHALI TUKUBALIANE NA UKWELI, HAWA WAMACHINGA NI JIPU LILILOLELEWA KWA MUDA MREFU SANA TOKA MH KITWANA KONDO AKIWA MAYOR WA JIJI, HAIINGII AKILINI JIJI KAMA LA DAR ESALAAM LINAKUWA DAMPO, SIO KTK WALA VITONGOJI VYAKE, HAO WA FANYA BIASHARA NDOGO NDOGO NI SHEEDER, TUNALIPA KODI TRA, TUNAPANGIWA BIASHARA HADI MLANGONI !!!! WAMEPEWA MAENEO YA BIASHARA HAWATAKI, NI KWELI KABISA HAKUNA ALIYEPEWA MTAJI NA SERIKALI AFANYE BIAS HARP AJABU WANADAI MAENEO YA KUFANYIA BIASHARA!!! UNA MTAJI TAFUTA PANGO PANGA FANYA BIASHARA, LEO WATU WANAIBUKA KUTETEA UOVU, HAO MADIWANI WA UKAWA WANA KAZI MOJA TU KUTEKELEZA WALIYOAHIDI IKIWEPO USAFI WA JIJI HAKUNA MJADALA, WAFANYE HIMA, WENZAO WA KINONDONI WALILIONA HILO WAKAANZA MAPEMA. HAKUNA MAENDELEO YANAYOPATIKANA KWA KUVUNJA SHERIA, WAKAE CHINI NA WAMACHINGA WAWACHANGISHE NA HALMASHAURI ICHANGIE WANUNUE MAENEO WANAYOONA NI RAFIKI KWA SHUGHULI ZAO NA SI MAENEO HATARISHI KM ROAD RESERVE. LA SIO WAONDOKE KAMA WALOVYOKUJA.
 
Hili suala nadhani linaleta mjadala wakati ambapo hakuna ulazima wa mjadala huu...ni kweli wamachinga walikuwepo siku zote, lakini ni kweli pia wapo mitaani kinyume na sheria (au by laws) za jiji...utakumbuka kulikuwa na fukuza fukuza ya hapa na pale, lakini wakifukuzwa walikuwa wanarudi kwa kuwa kulikuwa hakuna dhamira ya kweli kwa viongozi wengi wa awamu ya nyuma...Hata bandarini mambo yalikuwa hivyo hivyo, makontena zaidi ya 2000 hayalipiwi ushuru, meli pia hazilipiwi ushuru, na kadhalika...kwa hiyo mambo mengi yalikuwa yamelala...Kwenye awamu iliyopita kulikuwa pia na bomoabomoa lakini utashi wa kisiasa ulikuwa mdogo...mimi binafsi siamini kuwa hiyo hamisha ya wamachinga ni suala kwamba eti kwa kuwa jiji lina madiwani wengi wa vyama vya upinzani...Kumbuka awamu ya JPM ni ya uzinagatiaji wa sheria, na ndiyo maana kuna 'majipu' yanatumbuliwa...cha kusisitiza hapa ni kuwa maeneo yatengwe ili wafanyabiashara ndogo ndogo wapate eneo la kufanya biashara zao...Haiwezekani mji ukawa kila barabara ni soko, no way...pale msimbazi wamachinga wanapanga bidhaa barabarani...nasikia upo wakati teksi dereva alimgonga kwa bahati mbaya muuza bidhaa ndogo ndogo pale msimbazi na akauawa na wamachinga wenye hasira...mtu huwezi kutoka nyumbani kwako na kwenda kutandaza bidhaa barabarani, ukiambiwa uondoke, unadai upewe eneo la kufanya biashara...mambo hayaendi hivyo, lazima kuwe na mipango na taratibu...mimi masuala haya huwa sihusishi na siasa...wawe ni CCM au CHADEMA au CUF au chama chochote sheria lazima zizingagatiwe...
Hapo umenena na wakuakikisha hizo sheria ndogo zinafuatwa ni madiwani sasa utaratibu umeshawekwa ni nini sasa mkurugenzi anakuja kuingilia?
 
Back
Top Bottom