Shonza wakati unafukuzwa Chadema ulituhumiwa na kundi lako akiwemo Chagulani kuwa ninyi ndio wasaliti wa Chadema. Chagulani anajulikana kwa michezo yake michafu na Meya feki wa CCM anayejiita Chadema - Matata. Shonza mnafahamika mlivyoingizwa kwenye chama chetu (CCM ) mkaanza kutumika kuchafua Chadema mpaka sisi CCM tukachukiwa na wananchi, nyie na Mwigulu na Nape kila pahala eti na kwenye UVCCM kaanzishwa ka cheo ili Mwampamba ateuliwe, ujue tuliokuwa CCM tangu siku nyingi hatupendi unatujengea mazingira ya kuchukiwa kwa sababu ya post zako zisizo na adabu kila siku, unajihusisha na mambo binafsi ya watu hata kama sio ya kisiasa. Gazeti unalolitaja tunajua jinsi mnavyolitumia, vijipesa vyenu, mliandika sana mambo ya Ludo, mkaandika sana hadi kusingizia Mama wa Zitto katekwa na vijana wa Chadema, kesi iliripotiwa buguruni mkaandika na kubadili maelezo kila baada ya siku tatu, hadi leo hiyo kesi mmekaa kimya, hatuisikii, unahangaisha watu na kusababisha CCM ichukiwe. Chadema walikushindwa huku nako kuvumilia kwetu kunakaribia mwisho. Uwe na aibu mtoto, unatumika sana.