Madaktari KCMC wemeuwasha upya

Madaktari KCMC wemeuwasha upya

phina

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2011
Posts
414
Reaction score
126
Madaktari leo asubuhi wameukoleza moto kweli kweli!madaktari waliokwenye mafunzo ya vitendo (interns) wanazunguka tu wodini leo na madaktari wakazi(residents) wamekusanyika jengo la chuo cha kcmc wakiomba kupewa madarasa ya kusomea. Hii inatokana na vitisho walivyopewa na mkurugenzi wa hospitali kwamba hawaruhusiwi kugoma kwa sababu wao ni wanafunzi!
Madai yao ni kwamab 'sisi ni wanafunzi wa chuo hivyo hatuendi hospitali kutibu!tupewe madarasa tusome!'
Aluta continua
 
jana,mkurugenzi aliwaitia mapolisi madaktari walio katika mafunzo ya vitendo-waliokuwa katika 'vikao' vyao!
Huu si muda wa vitisho jamani-ni muda wa majadiliano!mnalazimisha punda kwenda mtoni hamwezi kumlazimisha kunywa maji!
 
KCMC walikuwa wanajivunia residents..tuone ujanaja wao sasa!
 
kitendo cha rais kubariki posho za wabunge ndio kimewatia zaidi hasira wafanyakazi wote wa sekta ya serikalini
 
Tanzania kuna shida nyingi sana,watu hawajali wengine wenye shida,kila mtu anajiangalia mwenyewe tu
 
Japo kulikua na mgomo lakini kcmc walikua wanafanya kazi kiaina sasa wamewatishia wameharibu kila kitu
 
Huuu mwaka umeanza vibaya kwa watawala wetu, wanasahau kuwa nyakati za vitisho ulishakwisha na sasa ni wakati mwingine watu wanajua na kutambua haki zao.

Watawala wakubali mazungumzo waache ubabe usio na maana wala faida kwa raia maskini na wasio na hatia hata kidogo wanaolipa kodi nyingi na kbwa kuliko wafanyabiashara wakubwa katika nchii hiii
 
Residents,kazeni buti wasiwatishe hao hawana lolote,huyo mkurugenzi anaona yeye ndo mtumishi bora na hajali maslahi ya wengine,aingie mwenyewe WODINI atibu wagonjwa.
Msitishike hata kidogo,sisi tunawaunga mkono,hadi kieleweke.
 
Rais hajasaini.

Hizo ni propaganda tu, Wabunge wanakula posho mpya toka kikao kilichopita.

Je, kama Raisi hajasaini hizo posho zinatoka katika mfuko wa Spika Makinda. Kwani yeye mwenyewe amekili Bungeni kuwa "toka kikao kilichopita wanapokea posho mpya"

Je, nani ni mkweli kati ya IKULU (Mtoa taarifa) na MBUNGE (Anayepokea bahasha)?????????

Lile ni changa la macho toka Ikulu kutufanya watoto kwani hatuendi kuchungulia maakaunti yao yanavyonona kipindi hiki.

Lakini ukweli ni kutoka kwa Spika ambaye ni kiongozi wa Wabunge amethibitisha hili jana.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Madaktari leo asubuhi wameukoleza moto kweli kweli!madaktari waliokwenye mafunzo ya vitendo (interns) wanazunguka tu wodini leo na madaktari wakazi(residents) wamekusanyika jengo la chuo cha kcmc wakiomba kupewa madarasa ya kusomea. Hii inatokana na vitisho walivyopewa na mkurugenzi wa hospitali kwamba hawaruhusiwi kugoma kwa sababu wao ni wanafunzi!
Madai yao ni kwamab 'sisi ni wanafunzi wa chuo hivyo hatuendi hospitali kutibu!tupewe madarasa tusome!'
Aluta continua

Jamani sasa hali imekua mbaya ndugu zetu wanazidi kupoteza maisha hosptali kwa ajili ya serikali.wanasema hawana uwezo huku nyuma wanajiongeza posho wao.kwakuzingatia madai ya madoctor umuhmu wake kwao pamoja na sie wananch kushindwa kutimizwa na serikali.mm naona ikohaja ya kutowaachia madoctor wenyewe inabidi nasie tutoke barabarani kwa maandamano kuunga mkono wapewe haki yao ya msingi.nasie tuwekewe mazingira mazuri ya afya.pamoja na kuokoa ndugu zetu ambao mpaka sasa wanateseka hosptal ikiwa nipamoja nakupoteza maisha kwakukosa huduma.naomba kuwakilisha.
 
na wanfunzi walio wodini (MD3,4 and 5) wako mbioni kuungana nao!hata vidondwa havitaoshwa i say!na damu ya kufanyiwa vipimp haitachukukiwa!
Maskini watanzania..
 
Back
Top Bottom