cartura
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,026
- 788
Kama concussion huenda kweli alianguka mna kugonga kichwa chake au alipigwa na chupa ya pombe kichwani kama wanavyodai!
ngoma bado mbichi hii....; mpaka hapo binti hajachomoka bado
Kama concussion huenda kweli alianguka mna kugonga kichwa chake au alipigwa na chupa ya pombe kichwani kama wanavyodai!
ina maana hujaelewa ubongo ulitikisikate mkuu? Hapo ndipo huyu Dogo anatakiwa kueleza zaidi ilikuwaje kampigiza au kajipigiza mpaka ubongo utikisike.
Kama sio Lulu basi kuna mwingine mwenye kesi ya kujibu. Concussion haitokei bila kugongwa ama kujigonga. Ila ile story ya Kanumba alilegea akaanguka inaweza kumtoa (after walau 3 years). Akitoka huko atakuwa mkubwa, anaweza kugombea ubunge wa vijana ccm
Kama sio Lulu basi kuna mwingine mwenye kesi ya kujibu. Concussion haitokei bila kugongwa ama kujigonga. Ila ile story ya Kanumba alilegea akaanguka inaweza kumtoa (after walau 3 years). Akitoka huko atakuwa mkubwa, anaweza kugombea ubunge wa vijana ccm
Kwa kifupi kabisa kama yaliyoripotiwa yote ni kweli basi Huyu mdogo wake Kanumba anapaswa kubeba lawama nzito na ninashauri baada ya mazishi ya leo huyu mdogo wake Marehemu Kanumba akamatwe na kuhojiwa kwa uzembe wa kutaka kuficha skendo la ufuska kati ya Lulu na Kanumba, hakuna Mtanzania mwenye utaratibu wa kuita daktari nyumbani panapotokea ugonjwa wa dharura.So kama haki itatendeka Lulu atakuwa huru ahame nchi..bt yule mdogo wa SK,mzito mzito flan hata mdomo yan kalegealegea,hakuwa seriouz tangu bro aanguke et ad doc wake aje!je kama asingepokea cmu?kwan alishndwa kupiga kelele majiran waje,au hata fasta fasta wangemuwahisha hosptal ya karibu af ndo ampgie doc wake,kwamba tupo sehem flan coz kwa nlivoelewa hiyo brain concussion angeweza kuomba hata maji,bt walilichukulia tatizo ki-star zaidi! Af pili kutokana na causes za tatizo,lazima kuna reason behind the scene! It is very confussing lakini! May his soul Rest in peace!
MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.
Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.
Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion, alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.
Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.
Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.
Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.
Dalili zinazoonyeshwa na madakatari hawa kutokana na autopsy zinaonyesha kuwa Kanumba alikuwa na kitu kinachoitwa "epidural hematoma." Kutokana na kuanguka kwa kawaida tu na kujigonga kwenye ukuta au sakafu, tatizo hili lisingejitokeza mara moja mpaka baada ya muda mrefu kidogo. Ndiyo maana wapigana ngumi na wacheza futiboli ya kimarekani hupata head trauma sana lakini dalili zake zinakuja kujitokeza miaka mingi baada ya wao kustaafu. Watu wote walioripotiwa kufa kutokana na tatizo hili kwa kuanguka, hasa kwenye michezo ya kwenye barafu, huwa wamaunguka kutoka kima cha juu kidogo, na huanza kupata kizunguzungu na mwishoni kufa baada ya muda mrefu kidogo kati ya nusu saa (severe impacts) hadi hata siku nzima tangu wapate hiyo impact ya kichwa. Ili tatizo hili likue ghafla na kusababisha kifo, inabidi impact ya kichwa iwe ni kubwa sana kwa ama kuanguka kutoka kwenye ngazi, accident ya gari lilikuwa katika mwendo wa kasi, au kupigwa kwa nguvu sana na kitu kigumu kama rungu.
Kwa hiyo kuna mambo mawili ya kuangalia:
(a) Je kulikuwa na silaha yoyote kama vile rungu au nondo iliyopatikana chumbani kwa Kanumba ambayo ilitumiwa na Lulu kumpigia Kanumba kichwani? Kama ipo, finger prints zinaweza kusaidia kuonyesha ni mtu gani aliyetumia silaha hiyo, unless kama crime scene imekwisha kuwa contaminated.
(b) Je Kanumba aliwahi kupata trauma ya kichwa ama mchana huo au jana yake halafu trauma hiyo ikaja kutoneshwa na impact nyingine wakati tayari ubongo ulishaanza kuvimba?.
Vile vile kutokana na ukweli huo wa tatizo linaloweza kuwa limemuua Kanumba, inaonyesha pia kulikuwa na uzembe uliofanyika katika kujaribu kuokoa maisha yake. Muda mwingi sana ulipotea kabla hajafikishwa hosptilai na kupata huduma; alikufa kabla hajapata huduma yoyote. Iwapo angewahishwa emergency room na kufanyia CT scan ya kichwa, ni dhahiri kuwa madakatri wangeliona tatizo hilo kabla halijwa fatal na hivyo wangemfungua kichwa chake kuruhusu uvimbe uishe kwanza kusudia ubongo usiharibike kabla ya kukifunika tena.
labda niulize,SO lulu is innocent mpaka apo
Labda kweli alianguka kwa bahati mbaya au alijigonga sehemu, Lulu nae apewe sehemu ya kujieleza, asionewe bure mtoto wa watu. Kama Lulu ni kicheche kwa nini marehemu alitembea nae..
Apewe nafasi ya kutueleza yaliyojiri siku hiyo.