Madai ya Wenyeviti wa CCM Vs Kubenea

Anyway, inaonekana hiyo njia ya kuelekea mahakamani ni ndefu sana kiasi kwamba wanashindwa kufika haraka!!!!
 
HABARI za kuaminika zilizochapishwa katika magazeti mbalimbali nchini hivi leo zinasema kwamba Viongozi wanne wa chama cha Mapinduzi wanamshtaki Bw. Said Kubenea, Mhariri wa gazetil lililosimamishwa na serikali ya Chama hicho kwa madai ya uchochezi ambayo hayakupitia polisi wala mahakamani shilingi Bilioni 4.

Questioning the News inauliza hivi Kubenea mwenyewe ana thamani ya milioni 10.

Na, je, viongozi wote wa mikoa wa CCM wakiwekwa pamoja wana thamani ya bilioni 4 unless, of cource, EPAnization imepenyeza mpaka ngazi hizo za chini?

Sintoshangaa, kama viongozi hawa wote wako upande mmoja wa itikadi au imani......
 
HABARI za kuaminika zilizochapishwa katika magazeti mbalimbali nchini hivi leo zinasema kwamba Viongozi wanne wa chama cha Mapinduzi wanamshtaki Bw. Said Kubenea, Mhariri wa gazetil lililosimamishwa na serikali ya Chama hicho kwa madai ya uchochezi ambayo hayakupitia polisi wala mahakamani shilingi Bilioni 4.

Questioning the News inauliza hivi Kubenea mwenyewe ana thamani ya milioni 10.

Na, je, viongozi wote wa mikoa wa CCM wakiwekwa pamoja wana thamani ya bilioni 4 unless, of cource, EPAnization imepenyeza mpaka ngazi hizo za chini?

Sintoshangaa, kama viongozi hawa wote wako upande mmoja wa itikadi au imani......


Mi nadhani hiyo ni vyema ili Kubenea akifika huko amwage yote hadharani na ushahidi kedekede. Patakuwa ptamu hapo.
 
WENYEVITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa mikoa minane ya Tanzania Bara, wametoa siku saba kwa Kampuni ya Hali Halisi Publishers kuwalipa sh bilioni nne na kuwaomba msamaha katika vyombo mbalimbali vya habari, vinginevyo watakwenda mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Wakili wa wenyeviti hao kutoka katika Kampuni ya Amicus, Abduel Kitururu, alisema fidia hiyo inatokana na kuchafuliwa majina kwa wenyeviti hao.

Alisema gazeti ya Mwanahalisi toleo namba 118 lililotoka Oktoba 8, lilikuwa na kichwa cha habari: ‘Njama za kumng'oa Kikwete zafichuka,' liliwataja wateja wao (wenyeviti wanane) kuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifanya njama hizo.

Alisema jana wametoa ‘demand notice' kwa Kampuni ya Hali Halisi Publishers kutaka kulipwa fedha hizo katika kipindi cha siku saba pamoja na kuombwa msamaha kwa kuchafuliwa majina ya wateja wao.

Alisema kila mwenyekiti aliyechafuliwa jina lake atapaswa alipwe sh milioni 500 kama fidia.

"Leo tumewapelekea demand notice watu wa Mwanahalisi tukitaka wateja wetu walipwe sh bilioni nne na kuombwa msamaha ndani ya siku saba na kama hawatalipwa tutakwenda mahakamani," alisema Kitururu.

Alisema wamezingatia mambo manne katika kutaka fidia hiyo, mosi ni ukubwa wa kashfa, nafasi za waliochafuliwa katika chama na jamii, mazingira yote ya kesi na mzunguko wa kashfa yenyewe, ambapo gazeti hilo hufika mbali zaidi.

Alisema lengo lao si kupimana ubavu na Mwanahalisi, bali wanapenda kuona haki inatendekea kwa kila upande, na kama hawatafikia makubaliano ndani ya siku hizo, basi mahakama ndiyo itakuwa sehemu ya mwisho.

Awali akizungumza kwa niaba ya wenyeviti wenzake, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam John Guninita alisema wameiteua Kampuni ya Amicus Attorneys kusimamia suala hilo.

Alisema hivi sasa wameamua kulipeleka suala hilo kisheria zaidi kuliko kisiasa, hivyo kuanzia sasa hawatakuwa wasemaji kuhusu ufunguaji wa kesi na mwenendo wake.

Wenyeviti hao ni John Guninita (Dar es Salaam), Clement Mabina (Mwanza) Khamis Mgeja (Shinyanga), Deo Sanga (Iringa), Onesmo Nangole (Arusha), Hypolitus Matete (Rukwa), Nawab Mulla (Mbeya) na William Kusila (Dodoma).

Uamuzi huo wa wenyeviti wa mikoa minane ya CCM umekuja takriban wiki tatu baada ya Serikali kulifungia gazeti la Mwanahalisi kwa kile kilichodaiwa kuandika habari za uchochezi mara kwa mara.

Tanzania Daima
 
Guninita ana nini cha kusema zaidi ya njaa tu,si alienda upinzani akaambiwa kijana utakufa njaa rudi ccm akarudi mbio,kwahiyo amerudi na wasio na aibu wakampa uenyekiti wakamuona wa maana wakaacha wanaccm halisi sio vinyonga kama yeye sasa ameamua kuwadanganya wenyeviti wa mikoani watake pesa nao wameingia mkenge,ila tunashukuru kujua thamani zao kumbe ni ndogo hivyo yaani mtu mzima kama Guninita ambae hata chama chake na wanaccm dar wamemuamini binadamu ambae thamani yake inapimwa kwa pesa,tukitaka kumvunjia heshima tunaandaa milioni 500 tu,tuambie na thamani ya wanao ili tujue familia yenu mna thamani gani kwa jumla.
 
kazi ipo mwaka huu wa shetani, wanaenda leo mahakamani au wataenda (waiting forever)
 
Kwa hiyo wenyeviti wanane wana thamani ya bil 4? Hivi tuna vigezo vya kukadiria thamani ya mtu katika masuala ya kulipana fidia nchini? hawa wamejuaje kuwa thamani yao ni hiyo?
Pia, wanachotaka ni kuombwa radhi ya fedha?
 
HABARI za kuaminika zilizochapishwa katika magazeti mbalimbali nchini hivi leo zinasema kwamba Viongozi wanne wa chama cha Mapinduzi wanamshtaki Bw. Said Kubenea, Mhariri wa gazetil lililosimamishwa na serikali ya Chama hicho kwa madai ya uchochezi ambayo hayakupitia polisi wala mahakamani shilingi Bilioni 4.

Questioning the News inauliza hivi Kubenea mwenyewe ana thamani ya milioni 10.

Na, je, viongozi wote wa mikoa wa CCM wakiwekwa pamoja wana thamani ya bilioni 4 unless, of cource, EPAnization imepenyeza mpaka ngazi hizo za chini?

Sintoshangaa, kama viongozi hawa wote wako upande mmoja wa itikadi au imani......

U need to be questioned ur self Sharif- ni CCM inayoshitaki au hao viongozi binafsi. Be specific.
 
Uwiiiii jamani!
Yani hawa wenyeviti wote wanane kuchafuliwa kote wanakodai wanadai Tsh. 500 Millioni kila moja. Yani Gunitita na Uzee wote kumbe hata Nape amekuzidi thamani, tena si Nape hata Wajumbe wa nyumba kumi sijawaiona wanathaminishwa kwa makaratasi (PESA).

Kwa kweli CCM imekishwa jamani tuipumzishe.
Kama ndiyo hivyo basi naomba anayejua thamani ya Makamba, Lowassa, Rostam, Kikwete anipe. Nataka niwalipue wakimbilie mahakamani then niwalipe makaratasi.

Gunitita yani hata mtoto wa miaka miwili amekuzidi thamani!
 
Hapo patamu.
Najua hizo bilioni 4 halipwi mtu,wala msamaha hauombwi katika hadhara yeyote. Hivyo nasubiri hawa ngumbalu wa marumbano wadhanio kila kitu ni pesa waende Mahakamani tupate pa kusemea.
Fupa hili liliwashinda mafisadi wote 11 sijui hawa wanajivunia nini, ni hivyo visenti vyao vya utajiri wa ujangiri wa meno ya tembo na faru na kupora abiria kwa mtutu wa bunduki???
 
Unajua hawa jamaa wa CCM hawana nauli za kwenda huko Mahakamani na labda wanachangiana nauli kwanza
 
Badala yake watajikuta wao wanamlipa Kubenea pesa hizo hizo.
Kubenea ni mwandishi machachali, mjanja na si kama wakina Guninita wanavyomtegemea.
Yeye ni mwangalifu sana anapoandika hoja zake.
Kama nasema uongo wakaulize kule Habari corparation ya enzi za ulimwengu wanajua hili.
Waliwahi kumtuhumu kwamba ameandika habari za uongo kuhusu mwenyekiti mmoja wa sisiemu mkoa mmoja wa kanda ya ziwa, simply tu kwa sababu huyo mwenyekiti alizikana habari hizo kwenye gazeti.
Baada ya kumdhalilisha alilishitaki gazeti la Rai na akaishia kulipwa mamilioni ya pesa maana alidhihirisha kuwa habari ile ilikuwa ni ya kweli.
Be carefull nyie wenye vigoda vya sisiemu. Msije jikuta mko kule kule kwa kumtajirisha zaidi. Msidhani mtapona kirahisi.
 
Wenyeviti wanane wa CCM wa mikoa , wamefungua kesi Mahakama Kuu dhidi ya gazeti la MwanaHalisi, wakitaka walipwe bilioni 4, kwa madai ya kukashfiwa na gazeti hilo. Katika hati ya mashitaka, wenyeviti hao wanataka kila mmoja alipwe Sh milioni 500, kutokana na gazeti hilo kuripoti kuwa makada hao wa CCM, wanashiriki kwenye njama za kutaka kumng’oa madarakani Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu ujao wa 2010.

Wenyeviti hao ni Deo Sanga (Iringa), Clement Mabina (Mwanza), Khamisi Mgeja (Shinyanga), John Guninita (Dar es Salaam), Nawab Mullah (Mbeya), Onesmo Ngole (Arusha), William Kusila (Dodoma) na Hypolitus Matete (Rukwa). Wenyeviti hao wanailalamikia kampuni inayochapisha gazeti la MwanaHalisi, Mhariri wa gazeti hilo, Kiwanda cha Pritech na Kiwanda cha Standard, ambavyo vinachapisha gazeti hilo pamoja na Saed Kubenea, ambaye ni mwandishi wa habari hiyo.


Duh hii kali Kubenea ana vijisenti vya kutosha kuwalipa waheshimiwa sanaaa !.

Gazeti linalolalamikiwa na wenyeviti hao ni lililotoka Oktoba 8, mwaka huu, likiwa na habari kuwa ‘Njama za kumng’oa Kikwete zafichuka’, huku habari hiyo ikiambatana na picha ya Rais Kikwete, mwanawe Ridhiwan na Rostam Aziz.

Wanadai katika kesi hiyo, kuwa mwandishi akifahamu nafasi walizo nazo walalamikaji katika jamii, aliamua kwa makusudi kuchapisha habari hiyo, wanayodai ya uongo, ambayo imewaondolea uaminifu wao kwa kiongozi wao wa chama, Rais Kikwete.

Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye anayeongoza vikao vya Kamati Kuu, Halmashauri Kuu ya Taifa na Mkutano Mkuu wa Taifa, ambao walalamikaji ni watajwa wa baadhi ya vikao hivyo. Wamenukuu aya iliyosema ‘kundi la watuhumiwa wa ufisadi limejipanga kumng’oa Rais Jakaya Kikwete ili asigombee urais mwaka 2010’, ikimaanisha kuwapo kwa njama chafu za kuwarubuni baadhi ya watu, wasipitishe jina la Kikwete kugombea nafasi hiyo.

Kwenye hati yao, pia wamenukuu aya iliyosema ‘katika CCM taarifa zinasema kundi lililopanga kugombea urais mwaka 2010, limekuwa linapigania kuwapo watu wake katika nafsi za juu za uongozi katika Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati Kuu.’

Wanadai kuwa habari hiyo, ilienda mbali zaidi na kuwaingiza wenyeviti hao wanane, kuwa wako katika mpango huo mchafu, kuhakikisha Rais Kikwete hachaguliwi na chama chake, kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao. Kwenye hati hiyo, walalamikaji wanaonyesha aya inayomtaja Guninita, akitajwa kwamba mjenga mkakati, akitumiwa na baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi, wenye ushawishi mkubwa ndani ya CCM.

Wameonyesha pia namna gazeti hilo, lilivyotaja sehemu za Mwanza, Dodoma, Arusha na Dar es Salaam, kuwa tayari baadhi ya mikutano ya mikakati imeanza. Walalamikaji wanachambua kashfa katika habari hiyo, kuwa ni kichwa cha habari, kilichosomeka njama kumng’oa Kikwete zafichuka na wao kuhusishwa kwenye mpango huo na kumtaja Guninita, kama kiongozi wa mkakati huo.

Pia, wanadai kuwa wamekashfiwa, kwa kuelezwa kuwa ni miongoni mwa kundi la mafisadi, wenye njama hizo, wakati ikitambulika kuwa fisadi ni mtu mwovu, ambaye anaishi kwa ulaghai wa rushwa na mfujaji wa mali ya umma.

Kutokana na mazingira hayo, wenyeviti hao wanaiomba mahakama, itamke kuwa habari hiyo iliwachafua mbele ya jamii wenyeviti hao wa CCM, imwamuru mhariri wa gazeti hilo, awaombe radhi, awalipe fidia waliyoainisha pamoja na riba pia ilipwe kuanzia kesi hiyo ilipofunguliwa; na gazeti hilo liwalipe gharama za mahakama. Gazeti hilo limefungiwa na serikali, baada ya kuchapisha habari hiyo, kwa madai kuwa ilikuwa ya uchochezi, yenye nia ya kumkosanisha Rais Kikwete na mtoto wake Ridhiwan.
 
Wenyeviti wanane wa CCM wa mikoa , wamefungua kesi Mahakama Kuu dhidi ya gazeti la MwanaHalisi, wakitaka walipwe bilioni 4, kwa madai ya kukashfiwa na gazeti hilo. Katika hati ya mashitaka, wenyeviti hao wanataka kila mmoja alipwe Sh milioni 500, kutokana na gazeti hilo kuripoti kuwa makada hao wa CCM, wanashiriki kwenye njama za kutaka kumng’oa madarakani Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu ujao wa 2010.

Wenyeviti hao ni Deo Sanga (Iringa), Clement Mabina (Mwanza), Khamisi Mgeja (Shinyanga), John Guninita (Dar es Salaam), Nawab Mullah (Mbeya), Onesmo Ngole (Arusha), William Kusila (Dodoma) na Hypolitus Matete (Rukwa). Wenyeviti hao wanailalamikia kampuni inayochapisha gazeti la MwanaHalisi, Mhariri wa gazeti hilo, Kiwanda cha Pritech na Kiwanda cha Standard, ambavyo vinachapisha gazeti hilo pamoja na Saed Kubenea, ambaye ni mwandishi wa habari hiyo.


Duh hii kali Kubenea ana vijisenti vya kutosha kuwalipa waheshimiwa sanaaa !.

Gazeti linalolalamikiwa na wenyeviti hao ni lililotoka Oktoba 8, mwaka huu, likiwa na habari kuwa ‘Njama za kumng’oa Kikwete zafichuka’, huku habari hiyo ikiambatana na picha ya Rais Kikwete, mwanawe Ridhiwan na Rostam Aziz.

Wanadai katika kesi hiyo, kuwa mwandishi akifahamu nafasi walizo nazo walalamikaji katika jamii, aliamua kwa makusudi kuchapisha habari hiyo, wanayodai ya uongo, ambayo imewaondolea uaminifu wao kwa kiongozi wao wa chama, Rais Kikwete.

Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye anayeongoza vikao vya Kamati Kuu, Halmashauri Kuu ya Taifa na Mkutano Mkuu wa Taifa, ambao walalamikaji ni watajwa wa baadhi ya vikao hivyo. Wamenukuu aya iliyosema ‘kundi la watuhumiwa wa ufisadi limejipanga kumng’oa Rais Jakaya Kikwete ili asigombee urais mwaka 2010’, ikimaanisha kuwapo kwa njama chafu za kuwarubuni baadhi ya watu, wasipitishe jina la Kikwete kugombea nafasi hiyo.

Kwenye hati yao, pia wamenukuu aya iliyosema ‘katika CCM taarifa zinasema kundi lililopanga kugombea urais mwaka 2010, limekuwa linapigania kuwapo watu wake katika nafsi za juu za uongozi katika Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati Kuu.’

Wanadai kuwa habari hiyo, ilienda mbali zaidi na kuwaingiza wenyeviti hao wanane, kuwa wako katika mpango huo mchafu, kuhakikisha Rais Kikwete hachaguliwi na chama chake, kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao. Kwenye hati hiyo, walalamikaji wanaonyesha aya inayomtaja Guninita, akitajwa kwamba mjenga mkakati, akitumiwa na baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi, wenye ushawishi mkubwa ndani ya CCM.

Wameonyesha pia namna gazeti hilo, lilivyotaja sehemu za Mwanza, Dodoma, Arusha na Dar es Salaam, kuwa tayari baadhi ya mikutano ya mikakati imeanza. Walalamikaji wanachambua kashfa katika habari hiyo, kuwa ni kichwa cha habari, kilichosomeka njama kumng’oa Kikwete zafichuka na wao kuhusishwa kwenye mpango huo na kumtaja Guninita, kama kiongozi wa mkakati huo.

Pia, wanadai kuwa wamekashfiwa, kwa kuelezwa kuwa ni miongoni mwa kundi la mafisadi, wenye njama hizo, wakati ikitambulika kuwa fisadi ni mtu mwovu, ambaye anaishi kwa ulaghai wa rushwa na mfujaji wa mali ya umma.

Kutokana na mazingira hayo, wenyeviti hao wanaiomba mahakama, itamke kuwa habari hiyo iliwachafua mbele ya jamii wenyeviti hao wa CCM, imwamuru mhariri wa gazeti hilo, awaombe radhi, awalipe fidia waliyoainisha pamoja na riba pia ilipwe kuanzia kesi hiyo ilipofunguliwa; na gazeti hilo liwalipe gharama za mahakama. Gazeti hilo limefungiwa na serikali, baada ya kuchapisha habari hiyo, kwa madai kuwa ilikuwa ya uchochezi, yenye nia ya kumkosanisha Rais Kikwete na mtoto wake Ridhiwan.

Shauri yao wamejiingiza kwenye shida bure. Maana ninavyomjua Kubenea na ujanja wake katika mashauri kama haya. Watamlipa wao hizo pesa. Hii si kesi yake ya kwanza katika masuala ya uandishi. Nakumbuka alishawahi kupata nyingine miaka ya nyuma.
 
Guninita na hao wenyeviti wenzie wote ni wachumia tumboni na ndio maana kundi la Lowassa[ Masha, Adam Malima, Peter Serukamba etc] not to mention Rostam wakawaidentify kuwa wao ni rahisi kuweza kuwatumia kufanikisha mpango wao. Sio siri kuwa walikwishapewa pesa nyingi kama kianzio na waliahidiwa fedha zaidi!! Sasa kwa vile MwanaHalisi limewaumbua ni lazima wajitetee kuwa wao wako pamoja na Jakaya.Sio siri tena kuwa wapambe wa Lowassa : Masha Malima na Serukamba wamekuwa wakisema hadharani kuwa wao watahakikisha kuwa Jakaya is a one term Rais na kosa lake ni kumtosa GOD FATHER wao Lowassa baada ya kufichuliwa ufisadi wake. Guninita na genge lake kama kweli watakwenda mahakamani wawe tayari kufedheheshwa kwani Kubenea ana ushahidi wa kujitosheleza.
 
Back
Top Bottom