Makaimati
JF-Expert Member
- Apr 4, 2011
- 462
- 87
Sun, 24 Apr 2011
Salma Said
WAKATI vikosi vya majeshi ya Ulinzi na usalama yakiendelea na mazoezi ya gwaride katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar kwaajili ya maadhimisho ya sherehe za kutimiza miaka 47 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Wazanzibari 15 wanaojulikana kama G15 wamejitokeza na kuhoji uhalali wa muungano huo kwakuwa hauna mkataba.
G15 ni kati ya vikundi mbalimbali vinavyojitokeza kuhoji uhalali wa muungano huku vingine vikishia kuishitaki serikali mahakamani.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar jana, Makamu mwenyekiti wa G 15 Rashid Yusuf Mshenga amesema kuwa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar hauna uhalali kwa kuwa Zanzibar hawakupewa mkataba.
"Muungano huu ni ‘verbal' tu, ni wa kuchanganya mchanga tu wan chi mbili, lakini ukiuliza Mkataba wa muungano haupo. Tunataka muuungano huu upitiwe upya" alisema Mshenga.
Alisema kuwa upande wa Tanzania bara walipata mkataba wa Muungano uliokuwa umesainiwa, lakini upande wa Zanzibar mkataba huo haukupatikana hali inayotia shaka katika muungano, "Wenzetu bara, Spika wa kwanza Adam Sapi Mkwawa na Pius Msekwa walibaki na nakala ya Mkataba, lakini Zanzibar hakukuwa na Barza la Mapinduzi lililokaa kujadili muungano. Hata Mzee Aboud Jumbe alipoingia madarakani alikiri kuwa hakukuwa na mkataba" alisema Mshenga.
Alisema kuwa harakati za kundi hilo zilianza tangu mwaka 2005 kwa kuishitaki Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili ionyeshe mkataba wa muungano na ndipo Mwanasheria mkuu wa SMZ alipokiri kuwa hana mkataba huo.
Alisema kuwa hata mwanasheria mkuu wa Zanzibar wa kwanza Dourado amethibitisha kuwa hakupewa makataba wa Muungano wala Katibu mkuu wa kwanza Baraza la Mapinduzi naye hakuhusishwa kwenye mkataba huo wa muungano, hali inayoonyesha kuwa Muungano huo haukuwa na uhalali.
Alisema kuwa baada ya kuthibitisha kuwa hakuna mkataba ndipo walipoandika barua Ofisi za Umoja wa Mataifa.
"Tuliandika barua Umoja wa Mataifa Aprili 2010, lakini kwakuwa hawakutujibu, tumewaandikia nyingine kuwakumbusha. UN wanapaswa kusimama kama waamuzi katika suala hili" alisema. Alisema kuwa mara Umoja wa Mataifa watakapowajibu, watafungulia kesi SMZ ili kutaka muungano ujadiliwe upya.
Mbali na Umoja wa Mataifa, Machenga alisema kuwa nakala ya barua hiyo pia ameipeleka katika balozi za nchi za Marekani, Uingereza, Urusi, Ufaransa, Ujerumani na Umoja wa Nchi huru za Afrika.
Machenga alishangazwa na Serikali ya Muungano na SMZ kuweka kamati ya kushughulikia kero za Muungano wakati hata Mkataba wa muungano haupo akisema kuwa hiyo ndiyo kero ya kwanza.
"Kamati ya kushughulikia kero za muungano inaundwa na makada wa CCM, kama Waziri mkuu na viongozi wa SMZ, wote hawawezi kuhoji mambo muhimu".
Machenga alishauri kuwa ili kupata uhalali wa Muungano, Serikali ya Muungano na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar waunde timu za kuujadili muungano kasha iitishwe kura ya maoni ili wananchi waamue muungano wanaoutaka.
Kuhusu uhalali wa kikundi hicho alichosema kuwa kinawawakilisha Wazanzibari wote, Machenga alisema kuwa wanaamini kuwa Wazanzibari wengi wanawaunga mkono kwakuwa hukumu ya kesi iliyothibitisha kutokuwepo kwa mkataba wa muungano imeungwa mkono na Wanzibari wengi.
Hata hivyo alisema kuwa hawatawahamasiaha Wazanzibari kwa maandamano kupinga muungano akisema kuwa hilo ni suala la kisheria hivyo wataendelea kufuata sheria tu.
Naye Sheikh Farid Hadi Ahmed aliyechana nakala ya muswada wa marejeo ya Katiba katika kongamano la kuujadili hivi karibuni, alisema kuwa hadi sasa hakuna muungano, ni maigizo tu.
Akizungumza nyumbani kwake Darajani mjini Zanzibar, Sheikh Ahmed alishauri kuwepo na kura ya maoni ili kutafuta uhalali wa muungano.
"Muungano umeshakufa, tangu walipokufa Karume na Mwalimu Nyerere, hakuna tena muungano. Cha kufanya sasa ipigwe kura ya maoni ili tuone kama wananchi wanautaka muungano"
Alisema kuwa muungano uliopo sasa haukuwa na uhalali kwakuwa wananchi hawakushirikishwa,
"Karume na Nyerere walikuja na kuwekea saini bila hata kuwashirikisha wananchi.hakuna aliyeweza kuhoji wakati ule kwakuw ailikuwa ni ubabe tu" alisema.
Aliufananisha muungano huo na muungano wan chi za Ulaya akisema kuwa Muungano unatakiwa uvutie siyo ulazimishwe,
"Kitu chochote kizuri kinavutia watu kuja. Angalia Jumuiya ya Ulaya, nchi nyingi zinaomba uanachama, lakini huu muungano wetu wa kulazimisha. Kama kweli kulikuwa na umuhimu wa kuungana, mbona tusiungane na Uganda na Kenya? Kwanini Zanzibar tu? alihoji Sheikh Ahmed
Salma Said
WAKATI vikosi vya majeshi ya Ulinzi na usalama yakiendelea na mazoezi ya gwaride katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar kwaajili ya maadhimisho ya sherehe za kutimiza miaka 47 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Wazanzibari 15 wanaojulikana kama G15 wamejitokeza na kuhoji uhalali wa muungano huo kwakuwa hauna mkataba.
G15 ni kati ya vikundi mbalimbali vinavyojitokeza kuhoji uhalali wa muungano huku vingine vikishia kuishitaki serikali mahakamani.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar jana, Makamu mwenyekiti wa G 15 Rashid Yusuf Mshenga amesema kuwa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar hauna uhalali kwa kuwa Zanzibar hawakupewa mkataba.
"Muungano huu ni ‘verbal' tu, ni wa kuchanganya mchanga tu wan chi mbili, lakini ukiuliza Mkataba wa muungano haupo. Tunataka muuungano huu upitiwe upya" alisema Mshenga.
Alisema kuwa upande wa Tanzania bara walipata mkataba wa Muungano uliokuwa umesainiwa, lakini upande wa Zanzibar mkataba huo haukupatikana hali inayotia shaka katika muungano, "Wenzetu bara, Spika wa kwanza Adam Sapi Mkwawa na Pius Msekwa walibaki na nakala ya Mkataba, lakini Zanzibar hakukuwa na Barza la Mapinduzi lililokaa kujadili muungano. Hata Mzee Aboud Jumbe alipoingia madarakani alikiri kuwa hakukuwa na mkataba" alisema Mshenga.
Alisema kuwa harakati za kundi hilo zilianza tangu mwaka 2005 kwa kuishitaki Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili ionyeshe mkataba wa muungano na ndipo Mwanasheria mkuu wa SMZ alipokiri kuwa hana mkataba huo.
Alisema kuwa hata mwanasheria mkuu wa Zanzibar wa kwanza Dourado amethibitisha kuwa hakupewa makataba wa Muungano wala Katibu mkuu wa kwanza Baraza la Mapinduzi naye hakuhusishwa kwenye mkataba huo wa muungano, hali inayoonyesha kuwa Muungano huo haukuwa na uhalali.
Alisema kuwa baada ya kuthibitisha kuwa hakuna mkataba ndipo walipoandika barua Ofisi za Umoja wa Mataifa.
"Tuliandika barua Umoja wa Mataifa Aprili 2010, lakini kwakuwa hawakutujibu, tumewaandikia nyingine kuwakumbusha. UN wanapaswa kusimama kama waamuzi katika suala hili" alisema. Alisema kuwa mara Umoja wa Mataifa watakapowajibu, watafungulia kesi SMZ ili kutaka muungano ujadiliwe upya.
Mbali na Umoja wa Mataifa, Machenga alisema kuwa nakala ya barua hiyo pia ameipeleka katika balozi za nchi za Marekani, Uingereza, Urusi, Ufaransa, Ujerumani na Umoja wa Nchi huru za Afrika.
Machenga alishangazwa na Serikali ya Muungano na SMZ kuweka kamati ya kushughulikia kero za Muungano wakati hata Mkataba wa muungano haupo akisema kuwa hiyo ndiyo kero ya kwanza.
"Kamati ya kushughulikia kero za muungano inaundwa na makada wa CCM, kama Waziri mkuu na viongozi wa SMZ, wote hawawezi kuhoji mambo muhimu".
Machenga alishauri kuwa ili kupata uhalali wa Muungano, Serikali ya Muungano na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar waunde timu za kuujadili muungano kasha iitishwe kura ya maoni ili wananchi waamue muungano wanaoutaka.
Kuhusu uhalali wa kikundi hicho alichosema kuwa kinawawakilisha Wazanzibari wote, Machenga alisema kuwa wanaamini kuwa Wazanzibari wengi wanawaunga mkono kwakuwa hukumu ya kesi iliyothibitisha kutokuwepo kwa mkataba wa muungano imeungwa mkono na Wanzibari wengi.
Hata hivyo alisema kuwa hawatawahamasiaha Wazanzibari kwa maandamano kupinga muungano akisema kuwa hilo ni suala la kisheria hivyo wataendelea kufuata sheria tu.
Naye Sheikh Farid Hadi Ahmed aliyechana nakala ya muswada wa marejeo ya Katiba katika kongamano la kuujadili hivi karibuni, alisema kuwa hadi sasa hakuna muungano, ni maigizo tu.
Akizungumza nyumbani kwake Darajani mjini Zanzibar, Sheikh Ahmed alishauri kuwepo na kura ya maoni ili kutafuta uhalali wa muungano.
"Muungano umeshakufa, tangu walipokufa Karume na Mwalimu Nyerere, hakuna tena muungano. Cha kufanya sasa ipigwe kura ya maoni ili tuone kama wananchi wanautaka muungano"
Alisema kuwa muungano uliopo sasa haukuwa na uhalali kwakuwa wananchi hawakushirikishwa,
"Karume na Nyerere walikuja na kuwekea saini bila hata kuwashirikisha wananchi.hakuna aliyeweza kuhoji wakati ule kwakuw ailikuwa ni ubabe tu" alisema.
Aliufananisha muungano huo na muungano wan chi za Ulaya akisema kuwa Muungano unatakiwa uvutie siyo ulazimishwe,
"Kitu chochote kizuri kinavutia watu kuja. Angalia Jumuiya ya Ulaya, nchi nyingi zinaomba uanachama, lakini huu muungano wetu wa kulazimisha. Kama kweli kulikuwa na umuhimu wa kuungana, mbona tusiungane na Uganda na Kenya? Kwanini Zanzibar tu? alihoji Sheikh Ahmed