Madai ya CCJ ya kipuuzi - Msekwa

Madai ya CCJ ya kipuuzi - Msekwa

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
305
Pasco na MMKJ nafurahi kuona mnavyojitahidi kuwafanya watu waone Ccj ni mkombozi, ni kama vile namona Pasco alivyokaa akisubiria hilo tamko. Jamani tumeona na kusikia matamko mangapi we need physical action now na si blaa blaa, leo Ccj wakimaliza tamko lao kesho Tendwa anatoa tamko lake keshokutwa Ccj watakuja na tamko kali maradufu baadaye Tendwa atawapuuza na sinema itakuwa imefika tamati. Mwisho Ccj kwa kujitetea watasema mnaona wasingenishika shati ningemgaragaza, ngumi za utotoni hizo.
Kama nilivyobashiri kuwa CCM na Tendwa watakuja na majibu ya kupuuza madai ya Ccj ndivyo inavyotokea sasa bado tutasikia mengi toka kwa Tendwa,

SIKU moja baada ya Chama Cha Jamii (CCJ) kutoa shutuma kali za kuhujumiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kisipate usajili wa kudumu, madai hayo yamepuuzwa na uongozi wa juu wa chama tawala.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara na Spika wa zamani, Pius Msekwa, aliwataka Watanzania kupuuza madai hayo aliyoyaita ya kizushi.

“Ndiyo binti yangu, kwani wewe unayaamini hayo?” Msekwa alimuuliza mwandishi wa habari hizi aliyeomba kupata kauli ya CCM kuhusu madai ya kufanya hujuma pamoja na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ili kukinyima usajili wa kudumu CCJ.

Hakuishia hapo Msekwa aliendelea kusema, “Jawabu lako ni kupuuzia maneno usiyoyaamini… usiyape uzito maneno ya kipuuzi na kizushi ambayo hata wewe huyaamini, eee basi tuishie hapo endelea kuyapuuzia,” alisema Msekwa.

Katika madai yake, CCJ ilinukuu kauli mbalimbali za kejeli, zenye kuonyesha kuwa ni ndoto kwa chama hicho kipya kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao zilizotolewa na viongozi wa chama tawala na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kwa nyakati tofauti.
 
Kama nilivyobashiri kuwa CCM na Tendwa watakuja na majibu ya kupuuza madai ya Ccj ndivyo inavyotokea sasa bado tutasikia mengi toka kwa Tendwa,

SIKU moja baada ya Chama Cha Jamii (CCJ) kutoa shutuma kali za kuhujumiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kisipate usajili wa kudumu, madai hayo yamepuuzwa na uongozi wa juu wa chama tawala.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara na Spika wa zamani, Pius Msekwa, aliwataka Watanzania kupuuza madai hayo aliyoyaita ya kizushi.

“Ndiyo binti yangu, kwani wewe unayaamini hayo?” Msekwa alimuuliza mwandishi wa habari hizi aliyeomba kupata kauli ya CCM kuhusu madai ya kufanya hujuma pamoja na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ili kukinyima usajili wa kudumu CCJ.

Hakuishia hapo Msekwa aliendelea kusema, “Jawabu lako ni kupuuzia maneno usiyoyaamini… usiyape uzito maneno ya kipuuzi na kizushi ambayo hata wewe huyaamini, eee basi tuishie hapo endelea kuyapuuzia,” alisema Msekwa.

Katika madai yake, CCJ ilinukuu kauli mbalimbali za kejeli, zenye kuonyesha kuwa ni ndoto kwa chama hicho kipya kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao zilizotolewa na viongozi wa chama tawala na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kwa nyakati tofauti.

Huyu mzee anazeeka vibaya! Walichofanya CCJ ni kunukuu aliyoyasema huko nyuma. Kwa nini anataka Watanzania wayapuuzie aliyoyasema mwenyewe?
 
Sisi wenye akili tuna jua yeye Msekwa ndiye mpuuzi na anafaa kupuuzwa!
 
Tutakutana huko mzee!

Na wewe unakwenda kwenye hichi chama kipya nini?

Bado ni siri mkubwa ila utaona vipeperushi! Jamaa yetu ana ID kibao siku hizi....nimemshtukia font zake!
 
Nadhani mwandishi hakumbana vizuri kwa maswali huyo Msekwa. Ina maana anakanusha kauli za viongozi wa Chama Cha Majambazi (CCM) ambazo CCJ wameziweka vizuri sana kuonyesha kuwa wanahujumiwa? Halafu huyu Msekwa naye siku hizi akili zake zinakuwa kama za Makamba tu. Ni pumba tupu.
 
Msekwa kafilisika kisiasa, namshauri apunzike siasa asije adhilika maana sasa anaongea tumba tupu.CCJ oyeeeeeeeeeeeee
 
Kama nilivyobashiri kuwa CCM na Tendwa watakuja na majibu ya kupuuza madai ya Ccj ndivyo inavyotokea sasa bado tutasikia mengi toka kwa Tendwa,

SIKU moja baada ya Chama Cha Jamii (CCJ) kutoa shutuma kali za kuhujumiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kisipate usajili wa kudumu, madai hayo yamepuuzwa na uongozi wa juu wa chama tawala.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara na Spika wa zamani, Pius Msekwa, aliwataka Watanzania kupuuza madai hayo aliyoyaita ya kizushi.

"Ndiyo binti yangu, kwani wewe unayaamini hayo?" Msekwa alimuuliza mwandishi wa habari hizi aliyeomba kupata kauli ya CCM kuhusu madai ya kufanya hujuma pamoja na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ili kukinyima usajili wa kudumu CCJ.

Hakuishia hapo Msekwa aliendelea kusema, "Jawabu lako ni kupuuzia maneno usiyoyaamini… usiyape uzito maneno ya kipuuzi na kizushi ambayo hata wewe huyaamini, eee basi tuishie hapo endelea kuyapuuzia," alisema Msekwa.

Katika madai yake, CCJ ilinukuu kauli mbalimbali za kejeli, zenye kuonyesha kuwa ni ndoto kwa chama hicho kipya kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao zilizotolewa na viongozi wa chama tawala na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kwa nyakati tofauti.

Kwa mtizamo wangu, kwa mtu mwingine yeyote anayejua siasa ila siyo mwanasiasa, angeweza kudhani kuwa CCM imennuliwa na CCJ ili kuipigia debe kwa wananchi. Pengine labda mimi huwa nafikiria kinyume tofauti na binadamu wenzangu. Mikwala kwa CCJ ni debe moja kali sana kwa CCJ, kwa mtu aliye makini na siasa za hapa!
 
Tatizo sijasoma Msekwa anasema upuuzi wenyewe ni upi? Kwa sababbu ni rahisi sana kumuita mtu mpuuzi kuliko kuonesha upuuzi wenyewe. Kwamba viongozi wa CCM hawajatoa kauli za kuonekana kujua kile msajili wa vyama vya siasa atafanya dhidi ya CCJ tena kwa uhakika mkubwa na kuwatisha wale wote wanaotaka kujiunga nacho? Kwamba CCM kupitia Marmo - Mbunge na kada wa CCM wamekula njama kukinyima CCJ usajili wa kudumu?
 
Mlinitaka aseme 'ndiyo tumekula njama'-are you serious? Karibu kwenye siasa za upinzani MM mtayakuta mengi. Hapo bado hamjashinda uchaguzi lakini mkurugenzi wa uchaguzi anamtangaza ambaye hakushinda, na akishatamka yeye ndiyo imetoka hiyo, welcome to TZ politics!!
 
Mlinitaka aseme 'ndiyo tumekula njama'-are you serious? Karibu kwenye siasa za upinzani MM mtayakuta mengi. Hapo bado hamjashinda uchaguzi lakini mkurugenzi wa uchaguzi anamtangaza ambaye hakushinda, na akishatamka yeye ndiyo imetoka hiyo, welcome to TZ politics!!

very true.. kuna gharama na ni lazima ilipwe.
 
.. ccj ni wapuuzi tu, watajiandaaje kushiriki uchaguzi wakati hawana chama?.... haya ndiyo ya kuchemsha maji ya ugali kisha unaanza safari ya kwenda kusaga unga! ...sasa akikuta mashine imeishiwa dizeli anasema mwenye mashine anamkosesha ugali wakati maji tayari yameishacheka, .. hawa ccj wataimba sana mwaka huu kila kukicha wanakuja na visingizio kibao, wamemuingiza mjini mpendazote na sasa kaamua kufa nao, heri mrema angalau enzi zake aliambulia kugombea na urais akajiandikia kahistoria... haahah...... watanzania bwana ... upuuzi mtupu
 
Back
Top Bottom