Madagascar wavumbua mafuta.

Tiger

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2007
Posts
1,747
Reaction score
387
Nimesikia asubuhi leo kupitia BBC kuwa kisiwa kikubwa cha madagascar kimevumbua hifadhi kubwa ya mafuta aridhini.
Mwenye taarifa zaidi anaweza-share nasi.
 
lkn kwanini bei yake haishuki? au ndiyo kusema
wazalishaji wameamua kujipatia faida ya kufa mtu
 
Mkuu naona pwani ya Africa Mashariki itakuwa kama mashariki ya KATI.
 
Dah!Lakini Rais wao yule disco joker anayetawala kimabavu anawaangusha sana aisee!Sasa hivi kwa Africa Madagascar nafikiri ipo kwenye bottom 10 ya nchi masikini. Kila la heri jirani zetu!
 
Tanzania tukipata kiongozi mzuri anayeangalia maslahi ya taifa kwanza kabla ya maslahi ya familia yake, ni dhahiri kuwa raslimali zetu zitaturusha mbali sana kama taifa. Wakati wa Nyerere sera ilikuwa ni kutoruhusu raslimali zetu zichukuliwe na wageni kwa matumanini ya kusubiri hadi watanzania wafikie uwezo wa kuzitumia. Wakati wa Mkapa, mambo yakabadilika ikawa ni kuuza raslimali hovyo hovyo kwa maslahi ya viongozi; leo hii imekuwa ni ada kuwa wanasiasa wetu pamoja na familia zao wamechukulia kuwa raslimali zetu ni trufu yao kupatia mlungula wa kununua vitu vikubwa lakini vyenye thamani ndogo sana kulingana na raslimali hizo. Unaposikia mawaziri wanapewa mlungula kununua apartments za dola laki saba kwa kutoa vibali vyenye mabilioni ya dola basi ujue uongozi huo una matatizo; hali imekuwa vivyo hivyo kwa familia ya mkuu wa nchi!
 
Tanzania tukipata kiongozi mzuri anayeangalia maslahi ya taifa kwanza kabla ya maslahi ya familia yake, ni dhahiri kuwa raslimali zetu zitaturusha mbali sana kama taifa. Wakati wa Nyerere sera ilikuwa ni kutoruhusu raslimali zetu zichukuliwe na wageni kwa matumanini ya kusubiri hadi watanzania wafikie uwezo wa kuzitumia. Wakati wa Mkapa, mambo yakabadilika ikawa ni kuuza raslimali hovyo hovyo kwa maslahi ya viongozi; leo hii imekuwa ni ada kuwa wanasiasa wetu pamoja na familia zao wamechukulia kuwa raslimali zetu ni trufu yao kupatia mlungula wa kununua vitu vikubwa lakini vyenye thamani ndogo sana kulingana na raslimali hizo. Unaposikia mawaziri wanapewa mlungula kununua apartments za dola laki saba kwa kutoa vibali vyenye mabilioni ya dola basi ujue uongozi huo una matatizo; hali imekuwa vivyo hivyo kwa familia ya mkuu wa nchi!
 
Ile AFRICOM haikuanzishwa kwa bahati mbaya.

link US building a 'constellation' of drone bases - Threat Matrix

Thanks 4the info mkuu, having said that, the last but two paragraph caught my eye, take a look:


Mkuu ma-YANKEE wana mbinu nyingi za kutaka ku-contain mataifa yenye mali nyingi za asilia specifically OIL, walisha smell a rat katika kanda ya pwani ya Africa Mashariki - hapa watajifanya kufukuzana na Al-Qaeda kumbe malengo yao ya kweli ni tofauta kabisa, sasa hivi wako obsessed na vitu viwili: MAFUTA na Kujaribu kuidhibiti CHINA isijitanue Barani Africa na Latin America. Kinacho nishangaza, asubuhi hii nili-tune kwenye channel ya CBS nikasikia wanasema come 2020 America itakuwa inaongoza Duniani katika nishati ya mafuta i.e Taifa lao lina mafuta mengi kuliko URUSI!! sasa kama ndio hivyo kwa nini wanaendelea kununua na kuhodhi mafuta mengi kutoka dunia za tatu?

Kitu kingine ni kuhusu tekinolojia ya kutumia DRONES, mkuu unajuwa tutarudi katika enzi za mashindano ya kuhunda silaha - kumbuka nuclear arm RACE, MATAIFA makubwa na madogo waliona salama yao itatokana na ku-posses a NUCLEAR BOMBS however crude; matokeo yake kila Taifa linagwaya kuwa la kwanza kutumia silaha hizo kwa mahasimu wake save Hiroshima na Nagasaki.

Nionavyo mimi DRONES zitafuatana mkondo huo huo wa silaha za NUCLEAR, kila Taifa litataka liwe na squadron upon squadron za DRONES na actually mashindano ya kuhunda DRONES yamikwisha anza, DRONES ni rahisi kuzihunda kuliko mabomu ya Nuclear - juzi juzi IRAN ilitumia wapiganaji wa Hezibbola huko Lebanon kurusha DRONES kwenye hanga la Israel, Waisreal walishtukia inakaribia Nuclear Complex yao ya DIMONA katika jangwa la Negev - mambo haya ni hatari sana.
 
Nimesikia asubuhi leo kupitia BBC kuwa kisiwa kikubwa cha madagascar kimevumbua hifadhi kubwa ya mafuta aridhini.
Mwenye taarifa zaidi anaweza-share nasi.

Mkuu ni kugundua siyo kuvumbua. Kuvumbua= to invent ni endapo kitu hakikuwepo aslan, kama kuvumbua gari.
Ama kugundua= to discover ni endapo kitu kilikuwepo lakini hakikujulikana kuwa kipo, aidha kwa kukosa nyenzo na maarifa, au kwa kutofikiwa na binadamu. Kugundua Ziwa Victoria.
Halafu unamaaanisha nini kusema 'hifadhi ya mafuta'? Jaribu kuandika Kiswahili rahisi cha kawaida na usitie madoido hayo ndiyo yanapelekea kwenye makosa ya sarufi, isimu au mawako.
 

Kiswahili kigumu mkuu.
Asante kwa elimu.
 

Mkuu kama sikosei ni Gesi Marekani anahifadhi ya Gesi ya Cubic mita trilion 28 wkati Urusi ni cubic mita 30 trilion. Ila USA itaipiku Urusi na kuwa namba moja katika Kuuza Gesi Duniani na Urusi itakuwa ya Pili. Kuhusu Silaha za Nyukilia hapo Bado inabakia mataifa Makubwa kama Urusi na Marekani na China, India, Pakstan na baadhi ya Nchi za Ulaya,

Kwa sasa Ushindani mkubwa wa Silaha ni Kati ya USA na URUSI na kama Ukiangalia triend ya Biashara ya Siraha Duniani USA ndo kiongozi ikifuatiwa na Urusi, then China na kwa haya mataifa makubwa kupigana ni Ngumu sana make kuingia vitani yenyewe kwa yenyewe ni kama kuwa Mwisho wa Dunia, Tutabakia kuona vita kati ya mataifa makubwa na na madogo, Ila makubwa kwa makubwa haiwezekani
 

link http://www.africom.mil/fetchBinary.asp?pdfID=20120302120151

link 2. Bad News for Africa: 3,000 More U.S. Soldiers are on the Way | Black Agenda Report
 

Mkuu Nonda thanks a lot 4 the info especially link No.2, yaani hiyo ina confirm hidden Agenda zao nilizo taja hapo juu - wanachota akili waswahili ili waendeleze unyonyaji wao, akili zao zote ziko kwenye MAFUTA na kuafanya Wafrica wapigane prox war on their behalf!

Alafu wasivyo kuwa na aibu wanakwenda mbali zaidi kutaka kuchagulia Nchi za Kiafrica marafiki - Bahati mbaya viongozi wa Africa sijuhi huwa awaelewi mbinu chafu za Taifa hili au ni kutaka kutafuta kukubalika au ukosefu wa ku-analyse mambo kwa kina? hata huwa sielewi mimi!!! Taifa linalo eleza dunia kwamba halina marafiki/enemies wa kudumu!!! Taifa kigeu geu kama hilo, viongozi wa ki-Africa wanawezaje kulichukulia SERIOUSLY??

Wenzetu Kenya wamekwisha vunja shackle za kuwa tegemezi la Mataifa ya Magharibi, wako beneti na WACHINA na Wakenya walivyo makini wamekwisha wapa Wachina mipango yao ya maendeleo katika nyanja za miundo mbinu,tekinolojia na viwanda - muda si mrefu Wakenya watakuwa wana paa kimaendeleo wakishirikiana na Wachina, sisi Watanzania tunashindwa ku-grab opportunity kama hiyo na actually Wachina wanatoa mpaka mikopo ya muda mrefu yenye riba nafuu kwa ajili ya maendeleo - baadhi ya Watanzania (Viongozi) wasio wahadirifu hawataki kuchangamkia chances kama hizo adimu kwa kuwa wanajua fika kwamba Wachina hawatoi RUSWA - wale wapi POLISI!! Attitude za namna hiyo ndio zimechangia katika kudumaza ufufuaji wa viwanda vyetu vya kuongeza ajila kwa vijana, tumboni street ndio imekalia DRIVE'S SEAT ya maendeleo ya TAIFA letu - mambo ya kusema sijuhi wanakemea ruswa/ufisadi ni kihini macho tu, Mh Mlema alikuwa anatumia mbinu zipi ku-contain zahama hizi ya RUSHWA iliyo kithili - kwa nini asipewe wizara ya mambo ya ndani akanusuru TAIFA letu.

Back to the point nataka kumalizia kwa kusema kwamba Watanzania tujaribu ku-emulate ndugu zetu wa Kenya na sisi tuwe karibu na Wachina ambao wanatoa misaada na mikopo nafuu kwa ajili ya maendeleo, tukiganganiza kukumbatia nchi za magharibi unnecessarily Wakenya watatuacha kwenye MATAA, oh yes tutaishia kuambulia mosquito nets na vidonge vya ARV kutoka nchi za magharibi!!! Tuwe wakweli nchi za magharibi azina nia thabiti ya kuendeleza nchi za ki-Africa, ni Viongozi wachache walio kuwa na ujasiri wa kuwambia ukweli wanyonyaji hawa, viongozi kama: The late Lumumba, late Kwame Nkruma, Nassar, late Kambarage, Mzee Mandela, Askofu TUTU bila kumsahau Robert Mugabe.
 
Nimesikia asubuhi leo kupitia BBC kuwa kisiwa kikubwa cha madagascar kimevumbua hifadhi kubwa ya mafuta aridhini.
Mwenye taarifa zaidi anaweza-share nasi.
Bila shaka ulitaka kumaanisha kuwa "wamegundua" lakini si "Kuvumbua" Tunaposema kuvumbua tunamaanisha ni aina fulani mpya ya kitu. Mafuta yaliyo"vumbuliwa" Madagascar ni aina ileile ya mafuta yaliyopo kote huko wanakochimba mafuta. Kama yangekuwa ni mafuta ambayo components zake ni tofauti na haya tunayoyafaha basi kweli wangekuwa wamevumbua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…