Mada: Kwanini tumefika hapa?

Daudi1

JF-Expert Member
Dec 14, 2013
8,761
8,640
Umofia kwenu!!!!!1

Kwanza kabisa niwatakie heri ya mwaka mpya 2022, ni muda mrefu kidogo nimekuwa ndugu mtazamaji lakini kwa leo naomba nilete hili kwenu.

Kwanza kabisa ijulikane taasisi ya mahusiano na ndoa ndio taasisi mama katika kuishape jamii, kumbuka taasisi hii ndiyo inayozalisha familia na familia ndio msingi wa maendeleo katika jamii yoyote, kupitia hii familia tunapata watu mashuhuri,viongozi wa dini,wanasiasa mashuhuri nk.

Lakini upepo unavyoenda hii taasisi imekubwa na dhoruba kuu, kutokana na changamoto zimewafanya vijana wengi wa kike na wa kiume kukata tamaa juu ya ndoa,ni kawaida tu kusikia "mimi nitafuta wa kuzaa naye tu basi, sitaki kuoa au kuoelewa kama mambo yenyewe ndio haya" Sasa kwanini tumefika hapa???....

1. Mahusiano yamegeuzwa ni sehemu ya ujasiliamali
Vijana wengi wa sasa wamegeuza mapenzi ni fursa ya kutoka, sio tena platform ya kuweza kutengeneza familia bora, vijana wakiume nao siku hizi wanatafuta mwanamke anayejiweza ukiwasikiliza wanasema maisha ni kusaidiana, hiyo kauli imewafanya wengi kupenda kitonga, mabinti nao ni hivyo hivyo unaweza kumpenda binti na kutimiza jukumu lako lakini ukaitwa danga na akawa na mahusiano na mtu mwingine kwa kigezo et huyu ndiye wa moyo, kama huyo ni wa moyo kwanini msiweke juhudi ya kutafuta vya mwili pamoja??

2. Mmong'onyoko wa maadili
Maadili yamepungua kabisa miaka ya nyuma mwanaume kutembea na mke wa mtu, suala lilikuwa halikubaliki yaani iweje utembee na mwanamke ambaye mwenzio amemgharamia na kujiwekea usingizi wake ndani wewe ukammendee ili hali wapo wanawake wengi wanahitaji kuhifadhiwa?? siku hizi imekuwa sifa na nyie ni mashahidi humu halafu inaanza kuonekana ni fahari kwa kijana kutembea na mke wa mtu, inaonekana ni ushujaa huku mwenye mke akionekana hajui mambo maarufu kama "kupeleka moto" Sasa kijana ambaye anatembea na mke wa mtu unafikiri ataoa?... hofu na mashaka ya kutafuniwa itamtafuna

3. Kuwa na Matarajio Makubwa
Vijana wengi wanapoingia kwenye mahusiano au ndoa huwa wanakuwa na matarajio makubwa kutoka kwa wenzi wao hii hutokana na ubinafsi, ule umimi, huyu hanifanyii hivi, mbona hafanyi hivi kama fulani, mwisho wa siku humpelekea mtu kutodumu katika mahusiano aliyoyaanzisha ama ndoa husika, inatakiwa ukumbuke wote ni binadamu na hakuna anayeweza kumtimizia mwenzake mahitaji yake kwa 100% hivyo tuwe wenye kutosheka na kuridhika.

4. Harakati za Haki sawa
Hiki ni kirusi kinachotafuna mahusiano na ndoa za wengine, dada yangu nikukumbushe tu kwenye suala la mahusiano hakuna kitu kinaitwa haki sawa, kwenye mahusiano mwanaume ni kiongozi na ili mahusiano yako yadumu lazima uzingatie hili "Akamwambia mwanamke, hakika nitakuzidishia uchungu, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo naye atakutawala" (mwanzo 3:15) . utii ndio kitu pekee na cha msingi sana wanawake wa kizazi hiki wamekosa, wanafikiri utii ni manyanyaso, ni ukatili na ndivyo linavyoweka kwa sura hiyo kitu ambacho si kweli.

5. Wanaume kutotaka kuwajibika katika mahusiano
Mahusiano ni zaidi ya tendo la ndoa ambalo wengi ndio hufikri ni mapenzi hayo, na ndio maana utaona wengi wakilalamika oooh mara ananinyima, oooh mara hafanyi sawa sawa, mahusiano ni zaidi ya hilo tendo hapa tukumbushane, baadhi ya wanaume wanasema kuoa mwanamke mwenye mtoto ni risk, ni kweli lakini huyo mtoto mwanamke anamtoa wapi?? usikute mwanaume umezalisha huko halafu unatembea kifua mbele kwamba sioi mwanamke mwenye mtoto, huyo uliyempa mtoto amuoe nani?? hao watoto/mtoto anatengenezewa sai8kolojia ya namna gani? muda mwingine akina dada mnasababisha hili mkihadaika kwamba pengine nikibeba mimba atanioaa, au anakuambia nizalie mtoto sitashindwa kumlea wakati unaona kabisa wewe mwenyewe mahitaji yako hupati sawa sawa, mwisho wa siku tunatengeneza watoto ambao hawana upendo wa kweli, watoto wanakuwa hawajali wala kuheshima

Tusipoliangalia hilop tukalichukulia kawaida basi tunatengeneza kizazi cha ajabu sana hapo baadaye, tutakao kuja kulaumiwa ni sisi, sasa hivi hali sio nzuri huwezi ukapita nyumba mbili tatu ukakosa binti aliyezalia nyumbani, itafika kipindi kumpata mwanamke ambaye hajazaa kabla ya ndoa itakuwa kama kusaka bikira, na litakuwa jambo la kufurahiwa sana kuliko kukutwa na bikra.

Samahani kwakuwachosha kwa thread ndefu najua mnapenda fupi fupi, mniwe radhi kwakweli, na hayo ni kulingana na mtazamo wangu na hali ya mazingira yaliyopo kwa sasa.
KARIBUNI KWA MJADALA​
 
yote haya
FB_IMG_16443502069653764.jpg
utandwazi
 
Binafsi naweza kusema

Mpango wa shetani ndio chanzo cha haya yote na hii kutokana na watu wengi hawajui nguvu ambayo ipo ndani ya familia. Hii inawafanya watu kutochukulia uzito swala hili

Kwakuwa baba ndio msingi wa familia shetani anatumia nguvu kubwa sana kuondoa neno ubaba ndani ya familia ili kusiwepo msingi. Kuna takwimu zinasema asilimia 90 ya watu waliopo jela kwa kesi za ubakaji na wizi ni kutokana na wao kutokuwa na baba

Nafikiri jamii na wakina baba wasisahau kuwa wao ndio chanzo kikubwa cha mabadiliko. Imewabidi kumtumainia Mungu ili wawe msingi imara wenye kutengeneza nyumba (familia) imara
 
Binafsi naweza kusema

Mpango wa shetani ndio chanzo cha haya yote na hii kutokana na watu wengi hawajui nguvu ambayo ipo ndani ya familia. Hii inawafanya watu kutochukulia uzito swala hili

Kwakuwa baba ndio msingi wa familia shetani anatumia nguvu kubwa sana kuondoa neno ubaba ndani ya familia ili kusiwepo msingi. Kuna takwimu zinasema asilimia 90 ya watu waliopo jela kwa kesi za ubakaji na wizi ni kutokana na wao kutokuwa na baba

Nafikiri jamii na wakina baba wasisahau kuwa wao ndio chanzo kikubwa cha mabadiliko. Imewabidi kumtumainia Mungu ili wawe msingi imara wenye kutengeneza nyumba (familia) imara
Ngoja nimtag mwnyw Iblis Bin Shetan aje akuparue vizur
 
Binafsi naweza kusema

Mpango wa shetani ndio chanzo cha haya yote na hii kutokana na watu wengi hawajui nguvu ambayo ipo ndani ya familia. Hii inawafanya watu kutochukulia uzito swala hili

Kwakuwa baba ndio msingi wa familia shetani anatumia nguvu kubwa sana kuondoa neno ubaba ndani ya familia ili kusiwepo msingi. Kuna takwimu zinasema asilimia 90 ya watu waliopo jela kwa kesi za ubakaji na wizi ni kutokana na wao kutokuwa na baba

Nafikiri jamii na wakina baba wasisahau kuwa wao ndio chanzo kikubwa cha mabadiliko. Imewabidi kumtumainia Mungu ili wawe msingi imara wenye kutengeneza nyumba (familia) imara
Ni sahihi kabisa kuna juhudi kubwa zinafanyika kumshusha mwanaume na kumuweka mwanamke kwenye nafasi ya mwanaume, na ndio maana utaona na wao wanasema mwanume siku hizi anaolewa kwasababu wana uwezo wa pesa, na wao et wakihitaji mwanaume muda wote wanampata kwa sababu pesa wanayo, ni suala la mwanaume kusimama kwenye nafasi bila kuyumba hiyo itasaidia kurudisha hali kuwa sawa
 
Uzi mzur sana,
Nmeusoma point to point, una hoja za msingi Sana.

Sema
Sasa wee kwa mtizamo wako unashaur Nini kifanyike.

Kisha na sisi ndio tufate Sasa
1. Wanaume kuwajibika katika mahusiano, kumbuka anayeanzisha mahusiano ni mwanaume, na mahusiano yana gharama,(muda,fedha, kujitoa) lazima mwanaume asimame, sifa ya mwanaume kamili ni kumfanya mwanamke ajione salama mwanaume akishindwa hapo tatizo linaanzia hapo

2. Wanawake wakubali kuwa hakuna usawa kwenye mahusiano wakitaka kutengeneza familia nzuri waliogundua hili ndoa/mahusiano yao yako imara licha ya kuwepo kwa changamoto mbali mbali

3. Kupunguza matarajio unapokuwa na mwanamke/mwanaume mahali pengine mwanamke anakuwa na mpenzi basi atamfanya mpenzi wake ndio mzazi wake, mara ada, kodi, sijui ada ya mtoto ambaye amezaa na mwingine, lakini pia tutambue hakuna binadamu aliyekamilika kila mmoja anamadhaifu tukiweza hapa usalama utakuwepo.
"Usiwe na haki kupita kiasi; wala usijiongezee hekima mno; kwani kujiangamiza mwenyewe?(Mhubiri 7:16)

" Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali akikutukana. Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unjua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana wengine" (Mhubiri 7:21-22)
 
Maumbile ya wanadamu, wajibu na majukumu yao yametanabaishwa wazi na Mungu muumba......

Kama ambavyo ili uwe salama kwenye chombo cha moto unapaswa kufuata maelekezo ku toka kwa mtengenezaji.....na ilivyo kupitia dini Mungu ametoa maelekezo ya namna ya kuishi kwenye ulimwengu ili viumbe wake wabaki salama......

Ukitazama kwa umakini utagundua kuwa wanadamu wametoka nje ya mikono ya muumba wanaenenda kulingana na utashi wa matamanio yao......

Mwanadamu hawezi kubakia salama kwa kutimiza kila hitaji la nafsi Bali kwa kutumia ufahamu na muongozo wa muumba......

Turudi kwa muumba........
 
Maumbile ya wanadamu, wajibu na majukumu yao yametanabaishwa wazi na Mungu muumba......

Kama ambavyo ili uwe salama kwenye chombo cha moto unapaswa kufuata maelekezo ku toka kwa mtengenezaji.....na ilivyo kupitia dini Mungu ametoa maelekezo ya namna ya kuishi kwenye ulimwengu ili viumbe wake wabaki salama......

Ukitazama kwa umakini utagundua kuwa wanadamu wametoka nje ya mikono ya muumba wanaenenda kulingana na utashi wa matamanio yao......

Mwanadamu hawezi kubakia salama kwa kutimiza kila hitaji la nafsi Bali kwa kutumia ufahamu na muongozo wa muumba......

Turudi kwa muumba........
Ubarikiwe sana,# turudi kwa Muumba#
 
Maumbile ya wanadamu, wajibu na majukumu yao yametanabaishwa wazi na Mungu muumba......

Kama ambavyo ili uwe salama kwenye chombo cha moto unapaswa kufuata maelekezo ku toka kwa mtengenezaji.....na ilivyo kupitia dini Mungu ametoa maelekezo ya namna ya kuishi kwenye ulimwengu ili viumbe wake wabaki salama......

Ukitazama kwa umakini utagundua kuwa wanadamu wametoka nje ya mikono ya muumba wanaenenda kulingana na utashi wa matamanio yao......

Mwanadamu hawezi kubakia salama kwa kutimiza kila hitaji la nafsi Bali kwa kutumia ufahamu na muongozo wa muumba......

Turudi kwa muumba........
Sahii kabisa,
namimi Ngoja nitafte Cha kuchangia afu narudi
 
Ngoja nimtag mwnyw Iblis Bin Shetan aje akuparue vizur
Hapa shetani anahusikaje lakini yaan mtu unaenda kufanya maovu kutumia akili yako unamsingizia shetani unaenda kuchepuka kwa tamaa ya kuendekeza akili yako then unasema shetani unauwa watu kwa ukatili unamsingzia shetani.

Kwa mantiki hii shetani ana ushawishi mkubwa nguvu kushinda jambo lolote iwe mungu sijui yesu sijui muhammad wote hawana ushawishi maana asilimia 90 ya wanadamu wanadhambi kasoro mimi peke yangu sina dhambi
 
MAHUSIANO yanazidi kuwa magumu zama hizi yaani kila mmoja anawaza kufaidika na mwenzako.. awe na pesa au mali kwao au awe na kazi nzuri daah ntasubiri mda mrefu sana
Na ndio maana mahusiano yanaonekana hayana maana, huko tunakoelea mauaji yatakuwa mengi zaidi kupitia mahusiano kama hatutaka kurudi kwenye msingi
 
Hapa shetani anahusikaje lakini yaan mtu unaenda kufanya maovu kutumia akili yako unamsingizia shetani unaenda kuchepuka kwa tamaa ya kuendekeza akili yako then unasema shetani unauwa watu kwa ukatili unamsingzia shetani
Kwa mantiki hii shetani ana ushawishi mkubwa nguvu kushinda jambo lolote iwe mungu sijui yesu sijui muhammad wote hawana ushawishi maana asilimia 90 ya wanadamu wanadhambi kasoro mimi peke yangu sina dhambi
Shetani ndiye mvurugaji wa kila jema linalotengenezwa, kwa habari ya ndoa mahusiano amevuruga saizi watu hata haoni umuhimu wa ndoa tena, saizi hata wanawake wanaweza kuridhishana wenyewe kwa wenyewe bila kuhitaji mwanaume tofauti na mpango wa Mungu, wanaume nao wanatamani kuolewa wenzao tofauti na mpango wa Mungu, lile kusudi la Mungu la kuzaliana nakuongezeka litatimiaje???
 
Sijasoma thread yote ila nafikiri chanzo kikubwa na mategemeo na matarajio ya wanaoingia ndoani, watu wanasahahu kwamba wanaooa na kuolewa nao si malaika kwenye mahusiano unaweza mfahamu mtu kwa asilimia chache sana ukiingia ndani ndipo unapoona rangi halisi ya mwenza wako ndipo watu wanaposhindwa kuchukuliana na ndoa kuvunjika.

Na ambao hawajaingia ndoani wakiangalia ndoa zilizokufa kwasababu izo, wanapata hofu na kusema bora nizae nisiolewe.
Waswahili ua wanasema kama zingine zimewashindwa haina maana na yako pia itashindwa.

Sidhani kama nmechangia sawa sawa na mada inavosema.
 
Sijasoma thread yote ila nafikiri chanzo kikubwa na mategemeo na matarajio ya wanaoingia ndoani, watu wanasahahu kwamba wanaooa na kuolewa nao si malaika kwenye mahusiano unaweza mfahamu mtu kwa asilimia chache sana ukiingia ndani ndipo unapoona rangi halisi ya mwenza wako ndipo watu wanaposhindwa kuchukuliana na ndoa kuvunjika.

Na ambao hawajaingia ndoani wakiangalia ndoa zilizokufa kwasababu izo, wanapata hofu na kusema bora nizae nisiolewe.
Waswahili ua wanasema kama zingine zimewashindwa haina maana na yako pia itashindwa.

Sidhani kama nmechangia sawa sawa na mada inavosema.
Sahihi kabisa, na hayo matarajio makubwa yanasababishwa na ubinafsi, kila mtu anaingia katika ndoa akitamani ya kwake yaende, kuna wengine huwa wanagombana kisa kutoa jina la mtoto anapozaliwa yaani kila mmoja anatamani yeye ndio atoe jina kwa mtoto na ugomvi unakuwa mkubwa hatari
 
Hapa shetani anahusikaje lakini yaan mtu unaenda kufanya maovu kutumia akili yako unamsingizia shetani unaenda kuchepuka kwa tamaa ya kuendekeza akili yako then unasema shetani unauwa watu kwa ukatili unamsingzia shetani.

Kwa mantiki hii shetani ana ushawishi mkubwa nguvu kushinda jambo lolote iwe mungu sijui yesu sijui muhammad wote hawana ushawishi maana asilimia 90 ya wanadamu wanadhambi kasoro mimi peke yangu sina dhambi
 
Hapa shetani anahusikaje lakini yaan mtu unaenda kufanya maovu kutumia akili yako unamsingizia shetani unaenda kuchepuka kwa tamaa ya kuendekeza akili yako then unasema shetani unauwa watu kwa ukatili unamsingzia shetani.

Kwa mantiki hii shetani ana ushawishi mkubwa nguvu kushinda jambo lolote iwe mungu sijui yesu sijui muhammad wote hawana ushawishi maana asilimia 90 ya wanadamu wanadhambi kasoro mimi peke yangu sina dhambi
Fact
 
Utandawazi, + Unyumbulifu wa maadili +

Ndio mchawi mkuu, Utandawazi umekuja Africa wakati Ambao Jamii zetu zikiwa bado hazijajiandaa vyema kifikira dhidi ya mapokeo ya utawazi huo na kujua jinsi ya kuendana nao , Matokeo yake vijana wa sasa tumejikuta tuna fuata kila Aina ya mapokeo toka ktika Mataifa yenye nguvu ya ushawishi Basi kujali zuri ama baya , pasipo kutazama Nguvu zetu za kisaikojia Kama zinaweza kuhandle pressure ya Yale tunayo yaiga ,

Leo hii mahala tulipofika ktika vijana 10 ni vijana wawili tu ndio utakuta hawana picha za ngono za wapenzi wao ktika device zao ,

Dunia imefika pabaya Sana,
 
Back
Top Bottom