Machungu ya kukosa ajira

Machungu ya kukosa ajira

2018

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2018
Posts
547
Reaction score
795
Aisee wewe acha kabisa, sikia tuu story kwa watu ila omba yasikukute au uwe ushapita kwenye kipindi kama hiki, ni ngumu sana kukubaliana na hii hali ya kukosa ajira hasa ukikumbuka miaka mingi uliyoipoteza kuipata elimu, 1+7+4+2+3/4/5 years in school halafu unafika mtaa unakutana na stori za kujiajiri halafu ukicheki huna hata mia ya mtaji.

Wengi watabeza na kukejeli lakini kwa wanaopitia hali hii wanaelewa uchungu na mateso yaliyomo hasa kifikra na kihisia, it's very hard to live it.

Namuomba Mungu akatufanyie wepesi vijana wenzangu wote tunaopitia hali hii na ikafike mwisho kabla mwaka huu haujaisha either tuwe tumepata ajira au mitaji kwa ajili ya biashara au kilimo au ishu yoyote.

Zaidi ya yote usiombe uwe ulijifunza na kubet ukiwa chuo au ukiwa mtaani, hio ndio balaa zaidi, unaweza ukasema hii buku em ngoja niikuze walau nipate elfu tano, Bayern Munich anapigwa wakati kila game alikua anashinda.

Oyaa sio poa wazee, sema fresh nothing is permanent.
 
Noma sana nimeuza sana matunda Kinondoni studio nikaja kuuza ma apple Mbagala Rangi tatu pamoja na ubuyu nikajaribu kuchukua vitu kutoka Zanzibar naleta DSM sio poa unakimbiwa na mchuchu pamoja na washikaji wanakudharau ila alhmdulilah sasa hivi kila mwisho wa mwezi unaona sms ndugu mteja umepokea kiasi cha kitoka kwenye namba hyo ni jambo la kushukuru kwa kweli.
 
Aiseeee wewe acha kabisa, sikia tuu story kwa watu ila omba yasikukute au uwe ushapita kwenye kipindi kama hiki,...
Man U unampa ashinde mara paaap anachakazwa na Brentford

Unamuona Underdog akicheza na Liverpool unampa Liverpool mara paaap Man U anashinda Liverpool anachakazwa vibaya

Hapo ndipo ile kauli ya maisha popote inakuingia akilini
 
Mimi najisemeaga miongoni mwa vitu ambavyo omba Mungu usivipitie basi ni kukosa ajira. Tena hasa pale linapogeuka kuwa tatizo sugu kwa upande wako, yaani unakaa mtaani miaka 3,4,5+ huelewi.

Halafu kumbuka umri haukusubiri unakuta wenzio wanaotea magepu vitengo vizito vizito, wanaoa/kuolewa, wanafanya maisha mengine wewe bado umestuck palepale, nyumbani unaanza kudharaulika unaonekana hamna kitu.

Hizo stress zake aiseee hakuna rangi utaacha ona. Mbona utaona duniani sio mahala salama pa kuishi!
 
Sio poa man. Nakumbuka nilipigaga mishe moja siku ikatokea ajali ya nusura kudondekewa na ukuta nilihisi ndio mwisho wa maisha nikaapa sintorudi tena kufanya ile kazi lakini kesho yake asubuhi nikicheki dharau za mtaani nikaona haiwezekani nikarudi kupiga mzigo kama kawa..
 
Mi najisemeaga miongoni mwa vitu ambavyo omba Mungu usivipitie basi ni kukosa ajira. Tena hasa pale linapogeuka kuwa tatizo sugu kwa upande wako, yani unakaa mtaani miaka 3,4,5+ huelewi. Halafu kumbuka umri haukusubiri unakuta wenzio wanaotea magepu vitengo vizito vizito, wanaoa/kuolewa, wanafanya maisha mengine we bado umestuck palepale, nyumbani unaanza kudharaulika unaonekana hamna kitu. Hizo stress zake aiseee hakuna rangi utaacha ona. Mbona utaona duniani sio mahala salama pa kuishi!
Nimepitia hayo
 
Kuna siku nilibamizwa na njaa mpaka nikaanza kucheka bila kujua nacheka nini.

Nikiwa kitaa nilipita sehemu ya chakula nikamuona mtu amechukua chakula kidogo nikaanza kumtukana kimoyomoyo si angechukua chakula kingi halafu anipunguzie abakishe ale hicho kidogo anachotaka.
 
Hiyo siku nimetoka kupiga zege hatujalipwa siku hiyo. Narudi geto sijui nakula nini hapo nimechoka kinyama. Nampigia simu bi mkubwa saa nne usiku hiyo anicheki hata hela ya kula.

Kama balaa vile katuma wakala kakosea namba. Mpaka wakala apige simu makao makuu wairudishe ilifika saa tano holaa. Dah nikaumiza kichwa ikabidi nimcheki mdada mmoja niliyekua nimezoeana nae muuza duka. Muda huo saa tano alishafunga mda,ila nikaenda kumgongea kubahatisha kama ataamka.

Kwa bahati nzuri aliamka nikamuelezea shida yangu. Akanipa unga wa ngano, sukari na majani. Nikarudi geto nikakanda unga nipike chapati na chai ninywe nilale. Asee sitasahau nilipika chapati ngumu ukikunja inavunjika .

Sikujali nilikunywa na chai nikalala na ule uchovu wa zege usingizi ulikua mtam sana. Sitasahau hiyo siku mpaka nilipiga selfie nikiwa nakula hizo chapati nimehifadhi nitakuja waonyesha watoto wangu.
 
Back
Top Bottom