Machungu ya kukosa ajira

Machungu ya kukosa ajira

Aisee wewe acha kabisa, sikia tuu story kwa watu ila omba yasikukute au uwe ushapita kwenye kipindi kama hiki, ni ngumu sana kukubaliana na hii hali ya kukosa ajira hasa ukikumbuka miaka mingi uliyoipoteza kuipata elimu, 1+7+4+2+3/4/5 years in school halafu unafika mtaa unakutana na stori za kujiajiri halafu ukicheki huna hata mia ya mtaji.

Wengi watabeza na kukejeli lakini kwa wanaopitia hali hii wanaelewa uchungu na mateso yaliyomo hasa kifikra na kihisia, it's very hard to live it.

Namuomba Mungu akatufanyie wepesi vijana wenzangu wote tunaopitia hali hii na ikafike mwisho kabla mwaka huu haujaisha either tuwe tumepata ajira au mitaji kwa ajili ya biashara au kilimo au ishu yoyote.

Zaidi ya yote usiombe uwe ulijifunza na kubet ukiwa chuo au ukiwa mtaani, hio ndio balaa zaidi, unaweza ukasema hii buku em ngoja niikuze walau nipate elfu tano, Bayern Munich anapigwa wakati kila game alikua anashinda.

Oyaa sio poa wazee, sema fresh nothing is permanent.
Ushuhuda ilipita mwezi mmoja na kidogo baada ya kunuwia katika uzi huu nikapata ajira private sector ambapo nilifanya kwa muda wa miezi sita tuu kisha nikapata ajira ya kudumu serikalini,namshukuru Mwenyezi Mungu,Muumba wa mbingu na nchi Kwa kunisaidia, pia vijana wenzangu napenda kuwatia moyo kwamba msikate tamaa,Mungu yupo na anajibu maombi
 
1.Nilikuwa sijui kuwa mtu anaweza kula sukari kwa kuilamba hadi asubuhi, hadi siku nilipojikuta kitu pekee kilichopo geto ni sukari tuu. Hakuna gesi wala majani, hiyo ni saa tano usiku.
2.Nilikuwa sijui kama jagi la umeme linawezakupikia wali na mtu ukala fresh tuu. Nina mchele tuu ndani, sina gesi, sina vocha, sina hata mia mbovu mfukoni.
3.Nilikuwa sijui kama mtu yeyote anawezakuwa fundi. Nilijikuta nimekuwa fundi mzuri tuu baada ya kukaa mtaani miaka 7 baada ya kuhitimu chuo.

Hapo nilikuwa nimeshahudhuria saili kadhaa DUCE na baadae zikahamishiwa Dodoma nikawa naona matangazo ya kazi tuu lakini siombi kwasababu hata nikiitwa usahili dodoma sina nauli.

Mwanamke niliyezaa nae mtoto wa kwanza akanikimbia na mtoto ila nikapata wa kunifaa na mwenye maono, tukajichanga tukakodi fremu baada ya mama mmoja kutuamini na kutuachia vitendea kazi vya grocery na jiko kufuatia kuhamia dodoma kumfuata mumewe kikazi. Hapo vinywaji kreti mbili mchanganyo. Nikitoka kwenye ufundi nawashawishi wenzangu tunakuja kujipooza kwenye grocery yangu. Akiwa mjamzito akanisihi niende dodoma kwenye kazi niliyoitwa usahili ila nikakataa sina pesa na kichwa kilishasahau yote ya chuoni hivyo nikupoteza tuu pesa maana sitoboi. Miaka saba mtaani siyo mchezo. Alipokea pesa wenyewe wanaita ya mchezo, akanikabidhi niende tuu maana tulioitwa usahili ni wachache hivyo kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata au kuingia database. Nikaenda dom kwa gari za IT za usiku asubuhi nikapiga pepa na kujishikiza kwa dogo UDOM hostel kusikilizia matokeo kesho yake ya kwenda usahili wa vitendo, nikaitwa na nikafanya na kurudi Dar kuendelea na mishe za saidia fundi na wakati mwingine fundi na kila aina ya kibarua ninachopata. Miezi mitatu baadae nikiwa nasafisha kiwanja cha mtu kwa kufyeka napigiwa simu ya "hongera, nimeona jina lako walioitwa kazini".
Kwasasa namshukuru Mungu kwa yote kwani kupitia mshahara niliweza kuboresha biashara, kuitanua na kufungua ofisi ya pili kubwa zaidi na kuwaajiri vijana wenzangu wasio na ajira nao wapambanie kombe na mama watoto kazi yake ni kwenda kukagua na kukusanya maokoto.
Msikate tamaa vijana wenzangu, ipo siku milango itafunguka. Pia omba Mungu umpate mwenza wakukustahimili wakati huu wa dhiki kwani huyo ndie atakayekupa moyo na nguvu ya kuvuka hiki kipindi
 
1.Nilikuwa sijui kuwa mtu anaweza kula sukari kwa kuilamba hadi asubuhi, hadi siku nilipojikuta kitu pekee kilichopo geto ni sukari tuu. Hakuna gesi wala majani, hiyo ni saa tano usiku.
2.Nilikuwa sijui kama jagi la umeme linawezakupikia wali na mtu ukala fresh tuu. Nina mchele tuu ndani, sina gesi, sina vocha, sina hata mia mbovu mfukoni.
3.Nilikuwa sijui kama mtu yeyote anawezakuwa fundi. Nilijikuta nimekuwa fundi mzuri tuu wa baada ya kukaa mtaani miaka 7 baada ya kuhitimu chuo.

Hapo nilikuwa nimeshahudhuria saili kadhaa DUCE na baadae zikahamishiwa Dodoma nikawa naona matangazo ya kazi tuu lakini siombi kwasababu hata nikiitwa usahili dodoma sina nauli.

Mwanamke niliyezaa nae mtoto wa kwanza akanikimbia na mtoto. Nikapata wa kutanana na mimi ila mwenye maono, tukajichanga tukakodi fremu baada ya mama mmoja kutuamini na kutuachia vitendea kazi vya grocery na jiko kufuatia kuhamia dodoma kumfuata mumewe kikazi. Hapo vinywaji kreti mbili mchanganyo. Nikitoka kwenye ufundi nawashawishi wenzangu tunakuja kujipooza kwenye grocery yangu. Akiwa mjamzito akanisihi niende dodoma kwenye kazi niliyoitwa usahili ila nikakataa sina pesa na kichwa kilishasahau yote ya chuoni hivyo nikupoteza tuu pesa maana sitoboi. Miaka saba mtaani siyo mchezo. Alipokea pesa wenyewe wanaita ya mchezo, akanikabidhi niende tuu maana tulioitwa usahili ni wachache hivyo kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata au kuingia database. Nikaenda dom kwa gari za IT za usiku asubuhi nikapiga pepa na kujishikiza kwa dogo UDOM hostel kusikilizia matokeo kesho yake ya kwenda usahili wa vitendo, nikaitwa na nikafanya na kurudi Dar kuendelea na mishe za saidia fundi na wakati mwingine fundi. Miezi mitatu baadae nikiwa nasafisha kiwanja cha mtu kwa kufyeka napigiwa simu ya "hongera, nimeona jina lako walioitwa kazini".
Kwasasa namshukuru Mungu kwa yote kwani kupitia mshahara niliweza kuboresha biashara, kuitanua na kufungua ofisi ya pili kubwa zaidi na kuwaachia vijana wapambanie kombe na mama watoto kazi yake ni kwenda kukagua na kukusanya maokoto.
Msikate tamaa vijana wenzangu, ipo siku milango itafunguka. Pia omba Mungu umpate mwenza wakukustahimili wakati huu wa dhiki kwani huyo ndie atakayekupa moyo na nguvu ya kuvuka hiki kipindi
Mtunze sana huyo mwanamke, ana maono
 
1.Nilikuwa sijui kuwa mtu anaweza kula sukari kwa kuilamba hadi asubuhi, hadi siku nilipojikuta kitu pekee kilichopo geto ni sukari tuu. Hakuna gesi wala majani, hiyo ni saa tano usiku.
2.Nilikuwa sijui kama jagi la umeme linawezakupikia wali na mtu ukala fresh tuu. Nina mchele tuu ndani, sina gesi, sina vocha, sina hata mia mbovu mfukoni.
3.Nilikuwa sijui kama mtu yeyote anawezakuwa fundi. Nilijikuta nimekuwa fundi mzuri tuu wa baada ya kukaa mtaani miaka 7 baada ya kuhitimu chuo.

Hapo nilikuwa nimeshahudhuria saili kadhaa DUCE na baadae zikahamishiwa Dodoma nikawa naona matangazo ya kazi tuu lakini siombi kwasababu hata nikiitwa usahili dodoma sina nauli.

Mwanamke niliyezaa nae mtoto wa kwanza akanikimbia na mtoto. Nikapata wa kutanana na mimi ila mwenye maono, tukajichanga tukakodi fremu baada ya mama mmoja kutuamini na kutuachia vitendea kazi vya grocery na jiko kufuatia kuhamia dodoma kumfuata mumewe kikazi. Hapo vinywaji kreti mbili mchanganyo. Nikitoka kwenye ufundi nawashawishi wenzangu tunakuja kujipooza kwenye grocery yangu. Akiwa mjamzito akanisihi niende dodoma kwenye kazi niliyoitwa usahili ila nikakataa sina pesa na kichwa kilishasahau yote ya chuoni hivyo nikupoteza tuu pesa maana sitoboi. Miaka saba mtaani siyo mchezo. Alipokea pesa wenyewe wanaita ya mchezo, akanikabidhi niende tuu maana tulioitwa usahili ni wachache hivyo kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata au kuingia database. Nikaenda dom kwa gari za IT za usiku asubuhi nikapiga pepa na kujishikiza kwa dogo UDOM hostel kusikilizia matokeo kesho yake ya kwenda usahili wa vitendo, nikaitwa na nikafanya na kurudi Dar kuendelea na mishe za saidia fundi na wakati mwingine fundi. Miezi mitatu baadae nikiwa nasafisha kiwanja cha mtu kwa kufyeka napigiwa simu ya "hongera, nimeona jina lako walioitwa kazini".
Kwasasa namshukuru Mungu kwa yote kwani kupitia mshahara niliweza kuboresha biashara, kuitanua na kufungua ofisi ya pili kubwa zaidi na kuwaachia vijana wapambanie kombe na mama watoto kazi yake ni kwenda kukagua na kukusanya maokoto.
Msikate tamaa vijana wenzangu, ipo siku milango itafunguka. Pia omba Mungu umpate mwenza wakukustahimili wakati huu wa dhiki kwani huyo ndie atakayekupa moyo na nguvu ya kuvuka hiki kipindi
Hongera mkuu
 
1.Nilikuwa sijui kuwa mtu anaweza kula sukari kwa kuilamba hadi asubuhi, hadi siku nilipojikuta kitu pekee kilichopo geto ni sukari tuu. Hakuna gesi wala majani, hiyo ni saa tano usiku.
2.Nilikuwa sijui kama jagi la umeme linawezakupikia wali na mtu ukala fresh tuu. Nina mchele tuu ndani, sina gesi, sina vocha, sina hata mia mbovu mfukoni.
3.Nilikuwa sijui kama mtu yeyote anawezakuwa fundi. Nilijikuta nimekuwa fundi mzuri tuu baada ya kukaa mtaani miaka 7 baada ya kuhitimu chuo.

Hapo nilikuwa nimeshahudhuria saili kadhaa DUCE na baadae zikahamishiwa Dodoma nikawa naona matangazo ya kazi tuu lakini siombi kwasababu hata nikiitwa usahili dodoma sina nauli.

Mwanamke niliyezaa nae mtoto wa kwanza akanikimbia na mtoto ila nikapata wa kunifaa na mwenye maono, tukajichanga tukakodi fremu baada ya mama mmoja kutuamini na kutuachia vitendea kazi vya grocery na jiko kufuatia kuhamia dodoma kumfuata mumewe kikazi. Hapo vinywaji kreti mbili mchanganyo. Nikitoka kwenye ufundi nawashawishi wenzangu tunakuja kujipooza kwenye grocery yangu. Akiwa mjamzito akanisihi niende dodoma kwenye kazi niliyoitwa usahili ila nikakataa sina pesa na kichwa kilishasahau yote ya chuoni hivyo nikupoteza tuu pesa maana sitoboi. Miaka saba mtaani siyo mchezo. Alipokea pesa wenyewe wanaita ya mchezo, akanikabidhi niende tuu maana tulioitwa usahili ni wachache hivyo kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata au kuingia database. Nikaenda dom kwa gari za IT za usiku asubuhi nikapiga pepa na kujishikiza kwa dogo UDOM hostel kusikilizia matokeo kesho yake ya kwenda usahili wa vitendo, nikaitwa na nikafanya na kurudi Dar kuendelea na mishe za saidia fundi na wakati mwingine fundi na kila aina ya kibarua ninachopata. Miezi mitatu baadae nikiwa nasafisha kiwanja cha mtu kwa kufyeka napigiwa simu ya "hongera, nimeona jina lako walioitwa kazini".
Kwasasa namshukuru Mungu kwa yote kwani kupitia mshahara niliweza kuboresha biashara, kuitanua na kufungua ofisi ya pili kubwa zaidi na kuwaajiri vijana wenzangu wasio na ajira nao wapambanie kombe na mama watoto kazi yake ni kwenda kukagua na kukusanya maokoto.
Msikate tamaa vijana wenzangu, ipo siku milango itafunguka. Pia omba Mungu umpate mwenza wakukustahimili wakati huu wa dhiki kwani huyo ndie atakayekupa moyo na nguvu ya kuvuka hiki kipindi
Ulisoma course gani maana course nayo inachangia upate kazi
 
1.Nilikuwa sijui kuwa mtu anaweza kula sukari kwa kuilamba hadi asubuhi, hadi siku nilipojikuta kitu pekee kilichopo geto ni sukari tuu. Hakuna gesi wala majani, hiyo ni saa tano usiku.
2.Nilikuwa sijui kama jagi la umeme linawezakupikia wali na mtu ukala fresh tuu. Nina mchele tuu ndani, sina gesi, sina vocha, sina hata mia mbovu mfukoni.
3.Nilikuwa sijui kama mtu yeyote anawezakuwa fundi. Nilijikuta nimekuwa fundi mzuri tuu baada ya kukaa mtaani miaka 7 baada ya kuhitimu chuo.

Hapo nilikuwa nimeshahudhuria saili kadhaa DUCE na baadae zikahamishiwa Dodoma nikawa naona matangazo ya kazi tuu lakini siombi kwasababu hata nikiitwa usahili dodoma sina nauli.

Mwanamke niliyezaa nae mtoto wa kwanza akanikimbia na mtoto ila nikapata wa kunifaa na mwenye maono, tukajichanga tukakodi fremu baada ya mama mmoja kutuamini na kutuachia vitendea kazi vya grocery na jiko kufuatia kuhamia dodoma kumfuata mumewe kikazi. Hapo vinywaji kreti mbili mchanganyo. Nikitoka kwenye ufundi nawashawishi wenzangu tunakuja kujipooza kwenye grocery yangu. Akiwa mjamzito akanisihi niende dodoma kwenye kazi niliyoitwa usahili ila nikakataa sina pesa na kichwa kilishasahau yote ya chuoni hivyo nikupoteza tuu pesa maana sitoboi. Miaka saba mtaani siyo mchezo. Alipokea pesa wenyewe wanaita ya mchezo, akanikabidhi niende tuu maana tulioitwa usahili ni wachache hivyo kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata au kuingia database. Nikaenda dom kwa gari za IT za usiku asubuhi nikapiga pepa na kujishikiza kwa dogo UDOM hostel kusikilizia matokeo kesho yake ya kwenda usahili wa vitendo, nikaitwa na nikafanya na kurudi Dar kuendelea na mishe za saidia fundi na wakati mwingine fundi na kila aina ya kibarua ninachopata. Miezi mitatu baadae nikiwa nasafisha kiwanja cha mtu kwa kufyeka napigiwa simu ya "hongera, nimeona jina lako walioitwa kazini".
Kwasasa namshukuru Mungu kwa yote kwani kupitia mshahara niliweza kuboresha biashara, kuitanua na kufungua ofisi ya pili kubwa zaidi na kuwaajiri vijana wenzangu wasio na ajira nao wapambanie kombe na mama watoto kazi yake ni kwenda kukagua na kukusanya maokoto.
Msikate tamaa vijana wenzangu, ipo siku milango itafunguka. Pia omba Mungu umpate mwenza wakukustahimili wakati huu wa dhiki kwani huyo ndie atakayekupa moyo na nguvu ya kuvuka hiki kipindi
Huu uzi utakuwa reference nzuri kwa jobless wote kutokata tamaa.
Hizi nyuzi zipo kama mbili hivi zinazoelezea msoto wetu kipindi tuko jobless.
 
Aisee wewe acha kabisa, sikia tuu story kwa watu ila omba yasikukute au uwe ushapita kwenye kipindi kama hiki, ni ngumu sana kukubaliana na hii hali ya kukosa ajira hasa ukikumbuka miaka mingi uliyoipoteza kuipata elimu, 1+7+4+2+3/4/5 years in school halafu unafika mtaa unakutana na stori za kujiajiri halafu ukicheki huna hata mia ya mtaji.

Wengi watabeza na kukejeli lakini kwa wanaopitia hali hii wanaelewa uchungu na mateso yaliyomo hasa kifikra na kihisia, it's very hard to live it.

Namuomba Mungu akatufanyie wepesi vijana wenzangu wote tunaopitia hali hii na ikafike mwisho kabla mwaka huu haujaisha either tuwe tumepata ajira au mitaji kwa ajili ya biashara au kilimo au ishu yoyote.

Zaidi ya yote usiombe uwe ulijifunza na kubet ukiwa chuo au ukiwa mtaani, hio ndio balaa zaidi, unaweza ukasema hii buku em ngoja niikuze walau nipate elfu tano, Bayern Munich anapigwa wakati kila game alikua anashinda.

Oyaa sio poa wazee, sema fresh nothing is permanent.
Mm naona wanaofuzu na kukaa mtaani wangekua vielelezo machuoni kuhusu kujiajiri ili watu wasisome wakidhani mbeleni Kuna ajira
 
Kuna ile tabia unajikuta unalala tu ghetto kama una smart na bando unaingia mtandaoni njaa ikikushika haswa unapika msosi hauna ratiba maalum unakula Unarudi mtandaoni baadae unalala unashtuka mwendo ni uleule hadi siku inaisha unalala


Ukichoka kukaa ndani unaenda kuzurura kutembea hovyo tu mtaani una muelekeo usio usioujua ili mradi tu uone njia ya kutokea utapita sehemu malaya wanajiuza hata kama huna pesa ili mradi uwaangalie tu roho isuhuzike

Kila demu kwako ni mkali na unataman kutongoza tongoza hovyo

Unakua na bajeti hatari elfu 1000 unaweza itumia siku mbili vocha tu ndio zinakuharibia hela

Yaani ukiwa jobless lazima phase hizi upite

Sema nini mwanangu utatoboa na utarudi kwenye hii komenti kuniambia mark my words
Mzee naona kama umenizungumzia mimi... yaaan umetembea mle mle... daaah ujobless uskie tu... ni kisanga sana🥲🥲
 
Ushuhuda ilipita mwezi mmoja na kidogo baada ya kunuwia katika uzi huu nikapata ajira private sector ambapo nilifanya kwa muda wa miezi sita tuu kisha nikapata ajira ya kudumu serikalini,namshukuru Mwenyezi Mungu,Muumba wa mbingu na nchi Kwa kunisaidia, pia vijana wenzangu napenda kuwatia moyo kwamba msikate tamaa,Mungu yupo na anajibu maombi
Nikucheki PM
 
Pole sana. Vijana tunapitia nyakati tofauti katika maisha ili kutujenga kuna kipindi unachapika hatari huna mbele wala nyuma.
Tusikate tamaa ipo siku itafika.
Halafu siku unapata mchongo utasahau shida zote yani unakua mpyaaaaaa.......
 
Back
Top Bottom