Machafuko na wakimbizi vyaongezeka ndani ya Israel. Wananchi wasema hawaelewi elewi

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,186
10,922
Mamia ya raia wa Israel wameendelea kuandamana karibu na makazi ya raisi wa nchi hiyo wakitaka vitu viwili.Kwanza ndugu zao waliotekwa warudishwe na Benjamin Netanyahu aondoke madarakani kwa kuitumbukiza nchi hiyo kwenye machafuko.

Hayo yakitokea kumekuwa na ukimbizi mkubwa wa ndani ya nchi ambapo wakazi wote wanaokaa mipakani ama wameondoka kuelekea katikati ya nchi au wamepata amri ya kuhama kwa hofu ya kutokea mapigano karibu na makazi yao.Hali hiyo imeonekana kuwaathiri zaidi wakazi wa kaskazini ambako mapigano kati ya Israel na kundi la Hizbolah ymekuwa yakiongezeka muda baada ya muda.

Umoja wa wenye mahoteli wanalalamika kupelekewa wateja wasiowatka waliojaza hoteli zoo.

 
Wayahudi wana maguvu meeengi ya kijeshi lakini Wayahudi wa leo wamekuwa mdebwedo, siyo kama wale akina Moshe Dayan
(1) Ni waoga mno, wanapenda kitonga , Marekani anawadekeza mno
(2) Ni taifa lililochanganyikiwa, Mazionists wanapigia upatu ushoga ndani ya ardhi takatifu
(3) Hawana amani kabisa mioyoni, ila wana kiburi ajabu. Superiority complex yao ni ya kutisha

Wakati mwingine Marekani inaona bora iendelee kuwasaidia kijeshi tu maana ikiwaacha wenyewe kama wenyeywe wakizidiwa hawachelewi kutandika nchi nyingine nuclear.
 
Sisi tuliojaaliwa kuwa angalao na kaamani kidogo (japo tumboni kweupe njaa zinauma) tujifunze na tuelewe namna vita ilivyo mbaya.

Just imagine hao jamaa na sifa zote wanazopewa kuhusu uwezo wa kivita intelligence support kutoka mataifa makubwa etc lakini wanaweweseka kiasi hiki hivi mimi na wewe tutakimbilia wapi?hapo Kenya?kuna njaa wenyewe hawaelewi hapo Uganda Mu7 haelewi Rwanda ndiyo kabisaa hatutoshi tutaenda wapi?kuna umuhimu kwa imani zetu kuendelea kuomba kwa ajili ya amani.
 
Back
Top Bottom