Mabibi na mabwana Afya wako wapi? Wateja na wahudumu wengi wa sehemu za kula hawajui kunawa mikono kwa usahihi kabla ya kula

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,260
Nimeshuhudia sehemu nyingi za kuuza vyakula au vinywaji wakiwa hawazingatii kabisa kanuni za usafi, na sio kwa sababu wanafanya makusudi bali kwa sababu ya uelewa mdogo.

Haya ndiyo niliyoshudia kwenye migahwa, mama ntilie na Bar

1. Wakati wa kunawa mikono kabla ya kula usitegemee upewe sabuni ya kunawa ila ukimaliza kula sabuni ya kunawa itatafutwa popote ilipo na kama haipo itaenda kununuliwa ukiisubiria! Hali hii inaonyesha wahudumu na wateja wengi hawajui kinyume chake ndio sahihi na kwamba ukinawa bila sabuni hujanawa umejipaka maji tu kwenye uchafu wa mikono.

2. Nimeshuhudia wahudumu wakitumia majagi au mabakuli wanayonawishia wateja baada ya maji kuisha kuchotea maji mengine ambayo wanawanawishia wateja wengine.Nimeshuhudia pia ndoo inayotumika kukingia maji ya kunawia ikichotea maji yanayotumika kunawia mikono tena.

3. Nimeshuhudia maji waliyonawai wateja yakitumika kuoshea vitambaa vya kufuta meza za wateja kuwekea chakula.

Haya ni mambo yanayofanyika na wateja na wahudumu mara nyingi sio kwa sababu maji ni machache au hakuna sabuni bali kwa sababu ya ujinga wa kutofahamu nini umuhimu na jinsi ya kunawa mikono kwa usahihi kabla ya kula na mazingira ya ujumla ya usafi wa chakula.
 
Wizara ya afya endeleeni kutoa elimu kuhusu namna bora ya kunawa mikono. Nina imani hata katika takwimu zenu kipindi cha kurona idadi ya wagonjwa wa kuumwa matumbo na kuharisha walipungua kwa kiwango kikubwa hospitali zote.
 
Tuwapime kwanza pombe

 
Halafu kuna hili jingine la kufunika chakula na mifuko ya plastic ili chakula kisipoe imeenea sana kwa mama ntilie walio wengi ....hawajui hio njia waitumiayo inaweza kuwa mojawapo ya kisababishi cha kansa.
 
1. Jagi lenye maji ya kunawishia kukalishwa ndani ya besen lenye maji machafu aliyonawa mteja.
2. Wateja Kunawa yale maji machafu ya kwenye ndoo ya kukingia maji tiririka.
3. Wahudum kushika mabaki ya chakul hasa mifupa ya Samaki na nyama kwa mikono
4. Kuchangany vyombo na taka zenye mafuta, taka ngum nk
 
Hii nchi ya ajabu sana yani miaka zaidi ya 60 ya uhuru kuna mijitu haijui kuzingatia afya zao.
 
Jagi linakalishwa ndani ya beseni la maji machafu na linatumbukizwa kwenye ndoo kuchotea maji, uchafu sana.
1. Jagi lenye maji ya kunawishia kukalishwa ndani ya besen lenye maji machafu aliyonawa mteja.
2. Wateja Kunawa yale maji machafu ya kwenye ndoo ya kukingia maji tiririka.
3. Wahudum kushika mabaki ya chakul hasa mifupa ya Samaki na nyama kwa mikono
4. Kuchangany vyombo na taka zenye mafuta, taka ngum nk
 
Nimewakuta wazungu Arusha hawajaoga siku nane wakitokea milimani, nywele vumbi, masharubu ndio duh makamasi yaliyokauka unayaona, ilivyonekana walikuwa na njaa sana kwani baada ya kufika kwa mama ntilie waliosha mikono na maji tuu na moja kwa moja kwenye msosi, walikuwa kinyaa kuwaangalia kabla, na kinyaa wakati wanakula. Hatari sana.
Uhamiaji wawe wanawaambia kuwa kuingia Tanzania lazima waoge, wasafishe masharubu yao pia.
 
Usafi wa vyakula mitaani bongo ni changamoto sana
 
Back
Top Bottom