Elections 2010 Mabere Marando kuibukia CHADEMA?

Marando ni Usalama wa Taifa na CCM na aliapa, never happen on earth akakiuka kiapo chake.
 
Hivi ninyi mnaomhukumu Marando kama vile ni mkimbizi-mvurugaji, mnajua keshafanya mangapi ya kimkakati yaliyonufaisha Chadema hata kabla ya kuja hadharani kutangaza kuhamia? Nijuavyo mie, kama uanachama sio kadi basi Marando ni Chadema toka kitambo kidogo.
Hakuna anayemuhukumu ila historia ya aliyoyatenda huko nyuma ndio inayomuhukumu
 
Kuna mashushu wengi tu wamekuwa mstari wa mbele kupigania mageuzi. To mention a few ni kuwa James Mapalala ni ofisa usalama wa Taifa aliyekuwa mstari wa mbele kupigania "mageuzi", Harold Jaffu ofisa usalama wa taifa mzuri tu aliyefanya kazi nzuri sana ya kuhakikisha TLP haipati nguvu hata kidogo, mabere marando amefanya azi nzuri sana ya kuhakikisha NCCR Mageuzi inakuwa kopo tu. Huwa Mabere hashindwi assignments zake, TISS wanajua kuwa yeye ni mtu smart na capable. He will deliver the goods and CHADEMA will go to their knees sooner than later.
Serikali iliposema inaruhusu vyama vingi vya siasa, ilifanya hivyo ili kuwaridhisha donors lakini ukweli ni kuwa haitaki na wala haikutaka. Mpaka leo watu wa usalama wa Taifa wanaambiwa kabisa kuwa mama ni CCM (sio Tanzania) so at any cost CCM itaendelea kulindwa na kuhakikisha inapata ushindi. Mnaosema kuwa mapandikizi ya CCM sasa hawako active TISS mnaota ndoto za mchana, just ask George Liundi atawaeleza. So if you think Marando is harmless you are dreaming, just wait and see.

Ndugu yangu, unafikri wakitaka kuvuruga wataanzia wapi kama sio huko kwenye miundo mbinu? Watapika majungu tu ili muweze kuvurugana while themselves (TISS - eg Mrema na Marando) wanajua nini wanachotaka ku achieve! Sasa ninyi mtabaki kusema...Ohh Tatizo la kimiundo mbinu, oh mara mrema alitaka kuhodhi madaraka NCCR, no .... that was a well planned deal.
 
Thx zangu nying kwa, Mwanakijiji, Meg3, Kichuguu na wengine wengi ambao mmejaribu kumwelezea maranda kwa undani.

1. Najua wengi wetu hapa tz tunadhani tumejawa na woga wa kupita kiasi, hatapale anapotokea mtu muhimu kutaka kutoa mchango wake ktk jamii anaonekana ni adui. tumezama kwenye propaganda za sisim hadi tunashindwa kuruhusu mifumo yetu ya kufikiri ifanye kazi zake vizuri.

2. tumekuwa watu wa ajabu sana kwa woga, na pale panapotajwa neno TIS. Hao Usalama ni mimi,wewe, mkeo, dadako, mamako,mwanao, babako na ndugu,jamaa na marafiki. wapo na wataendelea kuwepo na nina uhakika wapo wanao sapoti hata vyama vya upinzani. hata hapa jamii wamejazana tele.

3. Marando ni mwana mageuzi, na kama mnakumbuka kunawakati wanachama wa jamiiforums waliletewa za kuleta na polisi na kukamatwa na katika kumbukumbu zangu marando alikuwa kati ya watu waliyokuwa wanafatilia hiyo issue. mbona hatukumkataa kuwa yeye ni usalama atazidi kuihatarisha jamiiforums?

4. Mageuzi yetu yanahitaji ujasiri na wa hali ya juu, tusimwogope mtu, tujaribu kuangalia mchango wake wenye tija kwenye upinzani. marando namjua vizuri sana tena sana. kama kaamua kwenda chadema basi chademu imtumie kwa manufaa zaidi.

5. Rorya chadema wakijipanga vizuri zaidi watalichukua jimbo kiulaini sana, maana sisiem hamnakitu, Sarungi kajichokea sana tu, LameckAiro Eti naye anagombea ubunge!!!!!!.

Kumbukeni kuwa Rorya ni kati ya majimbo ya awali kabisa kuwa na vyama vya upinzani. na hatakipindi cha operation sangara Chadema walipata wanachama wengi rorya na hasa maeneo ya Nyambori anakotoka Marando.
Naamini kabisa CHADEMA wana utaratibu unaoeleweke. Marando kila la kheri huko Chadema!!!!
 
Marando kisha sema yeye ni mwanachama wa kawaida na hataki cheo hapo CHADEMA. Anasema yeye atabaki kuwa wakili wa kujitegemeana covert works nyingine teh teh teh!
 
Acheni utani jamani Mabere siyo ajenti wa TISS na wala hajawahi kuwa ajenti wa TISS.. kama makumi ya watu ambao wamekuwa wakijipitisha kuwa ni maajenti wa TISS.. ni wale wanaoitwa huku "starving artists"
Ni vigumu sana kukuamini wewe MMKJ kwani hata wewe upo against CHADEMA. Kule kuna thread ya kuhusu muasisi wa CCJ kujiunga TLP, so hatujui wewe utakuwa uko upande upi baada ya ile project kufa (maybe upo sambamba na Mabere). Kwa hiyo kwa sasa wale wote wanaotiliwa mashaka na CHADEMA waache waendelee kuwa under surveillance hadi baada ya uchaguzi.
 
Kwani mna uhakika gani kwamba hata Dr Slaa sio TISS? Waseminari wengi walioshindwa upadre walichukuliwa huko. La kujiuliza hapa ni kwamba Marando atakuwa "asset" au "liability" kwa CHADEMA?
 
Mageuzi hayaji kwa kuletewa mezani kwenye sahani, historia inatufundisha kuwa mageuzi yoyote ya kweli yanakuja kwa misuko suko yenye mchanganyiko wa ushindi, kushindwa, kujifunza na kuvumilia.

Leo hapa tunaviangalia NCCR, TLP, UDP n.k kama somo la kwa nini upinzani una hali mbaya Tanzania, kabla ya 1992 na bila juhudi za kina Mabere Marando tusingekuwa na NCCR wala chama cha kukiongolea. Sasa unapotaka kutushawishi tuachane na sababu za kisayansi na badala yake tukubali kuwa vyama vya upinzani vinakufa kwa sababu vimejaa Wapelelezi wa usalama wa Taifa bila ushahidi wowote ni kuturudisha nyuma.

Wanabodi wameweka hapa structural problems zilizojionyesha NCCR (kuwepo Mrema juu kuliko chama), sasa iwapo unaona hata CCM, Chadema etc na wao wana hizo structural issues; tuwekee hapa nina uhakika wanabodi watachangia kufanunua kwa nini NCCR imeumia lakini CCM bado inazidi kuwa imara.

Hivi bwana au sijui bibi Phares unazungumza maneno kimantiki au kinadharia? Nadhani wengine wetu mkiwa huko nje ya nchi mnazungumzo maswala ya mapinduzi pasina kuangalia nini kinaendelea Tanzania. Kuna mamluki wanatumwa na CCM kwenda upinzani kuhakikisha kuwa upinzani unakuwa dhaifu. Hivyo basi kuifanya CCM iendelee kutawala milele. Ndio maana mwenyekiti wa tume ya uchaguzi aliyepita aliwahi kusema siku moja kuwa kuna wanaccm ndani ya vyama vya upinzani. Sasa jiulize wewe kwanini Marando ameenda Chadema? Unapata majibu mengi mojawapo Dr Slaa anakubali na wengi wana CCM, Wanaupinzani na sie tusio na chama chochote kwamba ni mtu makini. Hilo ni tishio kwa Kikwete kwani akifanya masikhara atashindwa mwaka huu. Sasa sijui nia ya marando but dalili zinaonyesha kama alikuwa kweli ana mapenzi na mabadiliko angelihamia Chadema tangu mwaka jana. Kwanini amekaa muda mrefu mpaka leo karibuni? Na sio tu kuwa waoga bali ni kuwa makini kwani atakapoingia akajua siri zenu unadhani Chadema watashinda? Unafikiri CCM wajinga wawache mshinde kwa ubua? Mifano iko mengi tu mfano wazo la ujenzi wa chuo kikuu dodoma lilikuwa la chadema, CCM wamelibebaje kama sio kustuliwa na watu kuhusu nini Chadema wanataka kufanya.

Au nyie mnaosupport Marando mnataka akienda Chadema awavuruge vuruge ili turudi hapa JF kulalalama kuwa tunaonewa na nini kumbe mnafurahia utawala uliopo madarakani??? Mie niliwahi kusema mwanzoni watanzania lazima tuwe wanamapinduzi wa kweli. na sio mamluki wa chama tawala tukiwa hivyo mafisadi wataendelea kutawala Tanzania wao na vitukuu vyao hamna la zaidi. Mie na wewe tutabakia kwenye keyboard kulalama kila siku humu JF
 
Kwani mna uhakika gani kwamba hata Dr Slaa sio TISS? Waseminari wengi walioshindwa upadre walichukuliwa huko. La kujiuliza hapa ni kwamba Marando atakuwa "asset" au "liability" kwa CHADEMA?

Umesahau anaweza kuwa pia both kwani anaweza kuwa asset ili ashinde minds na heart za wanachadema then akishaingia ndani ya system akajua nini kinaendelea akapeleka taarifa anakokujua yeye hivyo kumfanya kuwa liability
 
CHADEMA ni makini hata kama Mabere atakuwa na nia mbaya hawatampa nafasi kwani wana utaratibu wao wa kuchagua viongozi. Nakumbuka walimgomea Mrema kupewa cheo juu kwa juu alipotoka CCM.
 
Mimi siungi mkono hata kidogo kwa mweshimiwa huyu kujiunga na CHADEMA,Huyu jamaa si mpizani wa kweli ni mvurugaji mkubwa,kumbuka kipindi cha kina lamwai,mi si mwamini hata kidogo sijui wenzangu mnaonaje?:pray:
 
mimi siungi mkono ujio wa Mheshiwa huyu kujiunga chadema,huyu jamaa si mtu wa mageuzi ni mvurugaji mkubwa,kumbuka kipindi cha kina lamwai,naona kama chadema hiyoo ina zama,hili mnalionaje wenzangu?
 
yaan kama alivyo kwenye avatar yake! uongo oungo tu

Edson, Basi nikwambie ndgu yangu hakna avatar ninayoipenda JF km ya huyu jamaa, ikifuatiwa na ile ya zamani ya mzizimkavu, ila maneno yako na avatar ya Rutunga vimeendana sana hapa nilipo sina mbavu, sina uhakika km utakosa murder kesi this time, mbavu zimechoka nakaribia kufa tu!
 
Aisee
Karibu Marando. Ila ujue kila kinachofanyika CHADEMA ni kwa maslahi ya nchi na si ya CCM (kama wafanyavyo wao..... Chama kwanza)
 
Nimesikitika asubuhi niliposikia kuwa Marando hatagombea ubunge. Ashawishiwe agombee jimbo lolote atakaloona anaweza kushinda kama sio huko kwao Rorya.
 
Kwani mna uhakika gani kwamba hata Dr Slaa sio TISS? Waseminari wengi walioshindwa upadre walichukuliwa huko. La kujiuliza hapa ni kwamba Marando atakuwa "asset" au "liability" kwa CHADEMA?

Jibu rahisi ni kwamba Marando ni liability kwa CHADEMA ....... big time liabillity; mark my words.
 
Acheni utani jamani Mabere siyo ajenti wa TISS na wala hajawahi kuwa ajenti wa TISS.. kama makumi ya watu ambao wamekuwa wakijipitisha kuwa ni maajenti wa TISS.. ni wale wanaoitwa huku "starving artists"

Naungana nawe Mwanakijiji kuwa Marando si TISS na wala hajawahi kuwa agent. Maagent wa TISS tunawafahamu na CHADEMA pia inawajua na wnegine tayari wapo ndani ya Chama.

Mimi nimemfahamu Marando kwa muda na nilijua kuwa atasuport CHADEMA kwenye uchaguzi toka mwezi wa tatu. Ila sikujua kuwa atajiunga rasmi kama Mwanachama.

Sasa tuongelee potentiality ya Marando:
1. kwanza kuwepo kwake kutahakikisha jimbo la Rorya linaenda CHADEMA (atakayebisha kwenye hili asubiri Octoba 31).
2. Ataisaidia sana CHADEMA kurejesha jimbo la Tarime ambalo kwa bahati mbaya sana CHADEMA ina kila dalili ya kulikosa kutokana na migongano isiyo ya lazima (infighting kati ya Mwikabe, heche na Mwera).
3. Mabere atakuwa msaada mkubwa sana kwa SLAA kwa kanda ya Ziwa maana anaheshimika sana.
4. Marando is a reputed public orator na anaweza kuteka masikio na kura za wasomi.
5. Marando hagombei uongozi wowote katika CHADEMA wala nchi so CHADEMA haina cha kupoteza.

Mimi si mshabiki wa personalities za watu ila imenibidi niseme kuweka records straight.
 
Asema atachanja mbunga kumnadi Slaa

Na Muhibu Said


Muasisi wa vyama vingi nchini na Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Mabere Marando, amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku akisema amefikia uamuzi huo ili kuendeleza mageuzi na kuongeza nguvu za kuking’oa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.
Sababu nyingine ya uamuzi wake huo, amesema inatokana na kuhamasishwa na uamuzi wa Mbunge wa Karatu anayemaliza muda wake, Dk. Wilibrod Slaa, wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia chama hicho mwaka huu.
Marando ambaye kitaaluma ni mwanasheria na Wakili wa Mahakama Kuu, alitangaza uamuzi wake huo katika mkutano na wahariri wa vyombo vya habari, jijini Dar es Salaam jana.
Hata hivyo, alisema uamuzi wake huo usichukuliwe kuwa una nia ya kutaka uongozi, kwani hana mpango wa kugombea nafasi yoyote ndani au nje ya chama hicho.
“Maswali mengi yameulizwa. Nimeulizwa mimi kama nagombea nafasi yoyote au sigombei. Napenda kuwaarifu Watanzania kupitia kwenu kwamba, sigombei cheo chochote. Sigombei urais, sigombei ubunge wala sigombei uongozi katika chama,” alisema.
“Kwa msingi huo ndugu zangu, nimewaita hapa kuwaeleza kwamba, leo nimeamua kwamba nahama chama cha NCCR-Mageuzi na nitajiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema,” alisema Marando.
Aliongeza: “Sijapotea njia, kwa sababu Chadema ni wapiganaji, ni wapambanaji na upambanaji ndiko nyumbani kwangu.”
Alisema amekuwa na msimamo wa dhati wa kutobadili mwelekeo wa kimageuzi katika nafsi yake, pia amekuwa na uvumilivu wa miaka 10 akitegemea kwamba, viongozi wake katika NCCR-Mageuzi, wangeweza kuinuka na kufanya kazi waliyodhamiria tangu awali ya kuongoza mageuzi nchini, bila mafanikio.
“Nimeamua kubadili chama. Nimehamasishwa zaidi na uamuzi wa Dk. Wilibrod Slaa kugombea kiti cha urais kupitia chama cha Chadema,” alisema Marando.
Aliongeza: “Niliwahi kumuambia Dk. Slaa kwamba yeye binafsi kama akiamua kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa umakini wake ninaoufahamu, uwezo wake wa kujenga hoja bungeni na uongozi wake ambao umekifanya chama chake katika miaka yote hii kisiharibike kama chama chetu kilivyowahi kuharibika, nimeamini kwamba anaweza kuongoza na nimemuahidi kwamba akiniingiza katika timu yake ya kampeni kutafuta urais wa nchi hii, nitakata mbuga nchi nzima kumsaidia.”
Alisema anaamini Dk. Slaa ataibuka mshindi na kwamba, asipofaulu, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, ana uhakika atakuwa Rais nchini.
Marando alisema ana imani kwamba, wenzake waliopo na waliokuwa NCCR-Mageuzi, kuna wengi, ambao wanaheshimiana nao, hivyo akiwaomba wampe kura kwa niaba ya Chadema, ana uhakika watafanya hivyo.
Alisema pia anaamini akiwaomba wakipigie kura chama hicho nchi nzima, kwa heshima wanayopeana toka walivyoanzisha mageuzi mwaka 1990, watamuunga mkono.
“Ni hawa watu ambao sasa nawanyooshea mkono nikiomba kwamba tufuatane, tujiunge na chama hiki, ambacho kweli kinaonyesha dhati ya kuendeleza mageuzi katika nchi yetu kwa nia ya kukiondoa Chama Cha Mapinduzi madarakani,” alisema Marando na kuongeza:
“Najua wengine watauliza hujarudisha kadi yangu ya NCCR-Mageuzi. Mimi nina kadi namba moja katika Chama cha NCCR-Mageuzi. Mimi ni mwanasheria. Jambo moja ambalo najua, ni kwamba ukiwa ni mwanachama wa CCM na uhame uende chama kingine, automatically (moja kwa moja) wewe ni mwanachama wa chama hicho kipya kisheria.
“Hivyo, ninapohama na kujiunga na Chadema na kuchukua kadi mpya na kuilipia, nirudishe kadi yangu ya zamani au nisirudishe, mimi ni mwanachama wa chama kipya cha Chadema. Kadi moja namba moja ya chama chetu cha mageuzi, ni historia ya Mabere Marando, hatimaye siku moja hata wanangu watatoa kama baba yetu alikuwa ni mshiriki katika kuanzisha chama hiki, hii ndiyo kazi yake.”
Marando alisema yeye na watu alioshirikiana nao katika kuanzisha mageuzi nchini, walikuwa na malengo makuu mawili; ikiwamo kuelimisha wananchi umuhimu wa demokrasia pana ya vyama vingi vya siasa na kuwahamasisha Watanzania kuanzisha vyama vingine vya siasa, badala ya CCM ili sera za vyama hivyo zieleweke kwa nia ya kukiondoa chama hicho madarakani.
“Nasisitiza kwamba nafasi ya chama cha upinzani siyo kukosoa chama tawala wala kusahihisha chama tawala tu, kazi zao hazistahili kuishia hapo. Kazi za kukosoa na kusahihisha iwe ni kuelimisha umma na umma kutambua chama tawala hakifai na chama tawala kiondoke madarakani,” alisema Marando.
Alisema mabadiliko nchini; kiuchumi na kisiasa yanayotamaniwa na Watanzania, hayataweza kupatikana bila kuiondoa CCM madarakani.
Marando alisema ili kuiondoa CCM madarakani, lazima vyama vingine vikue, vipate nguvu na wananchi wavielewe ili wavipigie kura katika Uchaguzi Mkuu.
Alisema binafsi mwaka 2000, baada ya chama chake cha zamani cha NCCR-Mageuzi kumuondoa Augustine Mrema katika uongozi, aliwania uenyekiti wa chama hicho, lakini akashindwa kupitia kura za kidemokrasia na kuamua kunyamaza.
Marando alisema wakati akiwa Mwenyekiti na baadaye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, alifanya kazi ya kutembea nchi nzima kueneza sera na kukisimika chama hicho, ikiwa ni pamoja na kufungua matawi ili kiweze kuenea na kuwa na uwezo wa kushinda uchaguzi na kuiondoa CCM madarakani.
Hata hivyo, alisema tangu alipoondoka kwenye uongozi wa NCCR-Mageuzi, alivumilia karibu miaka 10 akitegemea kwamba, wataweza kuendeleza kazi hizo alizozifanya katika uongozi, lakini hakuona dhamira njema ya kufanikisha mambo hayo.
Kutokana na hali hiyo, alisema akiwa mwanamageuzi asiyeyumba, alivumilia kuondoka NCCR-Mageuzi, lakini ameangalia muda mrefu jinsi ya kuchangia jitihada za kuhamasisha mageuzi nchini na kuwaelewesha Watanzania ili waweze kuungana kiasiasa kuiondoa CCM madarakani.
Alisema kwa miaka zaidi ya sita, Chadema imefanya kazi kubwa ya kutembea nchini, kuhamasisha umma na kuufanya umma uelewe umuhimu wa kuondoa CCM madarakani ili nchi iweze kupata mabadiliko ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Alizitaja kazi zilizofanywa na Chadema katika kipindi hicho kuwa ni pamoja na Operesheni Sangara, ambayo viongozi wake wakuu walijitahidi na kufanikiwa kuzunguka kila kona ya nchi na kufanya kazi nzuri.
Pia, alisema wabunge wa Chadema walivyokuwa bungeni waliibua hoja nzito na nzuri, ambazo alisema zilidandiwa na baadhi ya wabunge wa CCM wakapata umaarufu.
Alisema hoja za wabunge hao wa Chadema walizozitoa bungeni, zimesaidia kuwaelewesha Watanzania jinsi wanavyoongozwa vibaya, wanavyoibiwa.
“Kwa hiyo, kwa maoni yangu wameonyesha jitihada kubwa katika kuelekea azma, ambayo pia mimi ninayo, ambayo ni hatimaye kuondoa Chama Cha Mapinduzi katika madaraka,” alisema Marando.
Alisema kutokana na hamasa ya kisiasa waliyokuwa wameiweka katika Jimbo la Rorya, alilowahi kuliwakilisha kupitia NCCR-Mageuzi, muda mrefu chama hicho kilikuwa na viongozi katika ngazi za vijiji, kata hadi matawini jimboni humo.
Hata hivyo, alisema katika miaka michache iliyopita baada ya Chadema kuanza kazi hiyo na kutokana na viongozi wa NCCR-Mageuzi waliokuwa hawafanyi kazi ya kuendeleza jitihada hizo, wanachama wengi wa NCCR-Mageuzi waligeuza matawi yao kuwa ya Chadema.

CHANZO: NIPASHE
 
je waliyoyafanya kwa Mrema mpaka akawa kama alivyo leo hayatajirudia huko Chadema?
 
Back
Top Bottom