Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 26,362
- 39,842
Another proof kwa nini CCM haifai kushika hatamu za nchi hii tenaMabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia kwenye baraza la Mawaziri.Ni kiini macho.
Uhalisia ni kwamba Rais Samia alikusudia kujisimika na kujiimarisha kwa mbinu zozote ili kumuweka mkwewe kwenye Tamisemi kwa mpango rasmi kujipanga na uchaguzi mkuu.
Sababu huyo ni mtiifu na mwanafamilia hivyo anaaminika pia hata Msoga.
Rais amemuweka pale nwanafamilia ili kuhakikisha hamuangushi mama mkwe.soon tutaanza kuona mikeka mipya ya ma - RC's na ma- DC's kwa kutegemea nani yuko kundi lipi na mlengo upi ndani ya CCM.
Makamba kapelekwa Mambo ya nje kwa mpango maalumu.Despite kwamba Kikwete na kundi lao wanataka kumuandaa na kuweka mtu wa kulinda na kuyaendeleza maslahi yao ifikapo 2030.
Endapo watakuwa wameponyoka na kupora tena 2025.
Pili Makamba kawekwa pale sababu ndiyo wizara pekee ambayo waziri anasafiri mara nyingi kwenda nje kimajukumu tofauti na wizara zingine.
Ieweke kwamba Makamba kule Tanesco na kwingineko wizarani "Nishati" ameingiza serikali mikataba mingi mikubwa yenye utata, na tena yenye kugharimu maabilioni kama sio trilioni.
Hata kwenye Bwawa la Nyerere kuna harufu kubwa ya ufisadi.
Sasa basi...Kwa kigezo hicho itakuwa rahisi Makamba kufanya monitoring muda wote endapo itahitajika kurekebisha hitilafu vaina ya kundi lao na wapewa tender zenye rushwa huko nje hususan India.
Ni rahisi kwake Makamba kukimbia nje huko na kuyatatua juu kwa juu na kisha kurudi kwa kigezo cha uwaziri mambo ya nje.
Nashauri kama kweli bunge lina wazalendo ni wakati sasa Serikali kupitia Bunge iunde tume huru na ikachunguze madudu ya Tanesco na yatolewe hadharani.
Badala ya kumuuzia Biteko mbuzi kwenye gunia.
Tunachezewa mno.
Sakata la mafuta liwe kianzio!
Nawakilisha!