kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
JUMUIYA ya Afrika Mashariki, inakusudia kufanya mabadiliko makubwa ya mitaala ya elimu kuanzia ya msingi hadi ya chuo, ili kuziwezesha nchi wanachama, kutumia mtaala mmoja tu.Akizungumza na Mwananchi jijini Mwanza, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta alisema mkakati huo, wanafunzi wa nchi hizo kusoma popote ndani ya jumuiya, tofauti na ilivyo sasa.
Kwa mujibu wa Sitta, wanafunzi wanaopata fursa ya kusoma katika nchi za jirani ni wale tu ambao wazazi wao, wana vipato. "Tunaamini mpango wa kuwa na mtaalam wa aina moja, utarudisha haki sawa kwa watoto wa jumuiya hii katika sekta ya elimu, Watoto wa nchi moja watakwenda kusoma katika nchi nyingine kwa usawa kama wanavyosoma sasa katika nchi zao," alisema waziri Sitta.
Alisema pamoja na mpango huo, jumuiya pia imeridhia uhuru kwa wahadhiri wa vyuo vikuu, kuingia na kufundisha katika vyuo vikuu vya nchi yoyote ya Afrika Mashariki.Alisema hatua hiyo imengatia mahitaji makubwa ya wahadhiri katika vyuo vikuu vya nchi wanachama.
Alisema kwa mfano, nchi ya Burundi, inahitaji zaidi ya wahadhiri 1,000 kwa ajili ya kufundisha lugha ya Kiswahili na kwamba milango iko wazi kwa wanaotaka kwenda kufundisha.
"Tunakwenda kwa awamu, baada ya wahadhiri wa vyuo vikuu, tutaenda mbele zaidi kwa walimu wa shule za sekondari na wale wa shule za msingi,"alisema Siita.
Tayari nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimeanza kutekeleza itifaki ya soko la pamoja kwa manufaa ya raia wa nchi hizo.
source EAC mbioni kubadilisha mfumo wa elimu
Kwa mujibu wa Sitta, wanafunzi wanaopata fursa ya kusoma katika nchi za jirani ni wale tu ambao wazazi wao, wana vipato. "Tunaamini mpango wa kuwa na mtaalam wa aina moja, utarudisha haki sawa kwa watoto wa jumuiya hii katika sekta ya elimu, Watoto wa nchi moja watakwenda kusoma katika nchi nyingine kwa usawa kama wanavyosoma sasa katika nchi zao," alisema waziri Sitta.
Alisema pamoja na mpango huo, jumuiya pia imeridhia uhuru kwa wahadhiri wa vyuo vikuu, kuingia na kufundisha katika vyuo vikuu vya nchi yoyote ya Afrika Mashariki.Alisema hatua hiyo imengatia mahitaji makubwa ya wahadhiri katika vyuo vikuu vya nchi wanachama.
Alisema kwa mfano, nchi ya Burundi, inahitaji zaidi ya wahadhiri 1,000 kwa ajili ya kufundisha lugha ya Kiswahili na kwamba milango iko wazi kwa wanaotaka kwenda kufundisha.
"Tunakwenda kwa awamu, baada ya wahadhiri wa vyuo vikuu, tutaenda mbele zaidi kwa walimu wa shule za sekondari na wale wa shule za msingi,"alisema Siita.
Tayari nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimeanza kutekeleza itifaki ya soko la pamoja kwa manufaa ya raia wa nchi hizo.
source EAC mbioni kubadilisha mfumo wa elimu