Mababu zetu waliishi maisha mazuri kushinda kizazi cha sasa

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,313
Enzi hizo mtu anapotaka chakula, anaenda kwenye shamba la migomba, anatazama makumi ya mikungu ya ndizi na kuamua avune upi kwa chakula cha jioni cha siku hiyo. Karibu na shamba hilo kuna bustani ya viazi vitamu, bustani ya mihogo, viazi ulaya na mtama.

Upande wa kusini wa shamba la migomba kuna bustani za maharagwe,njugu mawe au karanga. Chini ya bonde ni ardhi ya malisho na makumi ya ng'ombe wa Kifrisia na wa kuzaliana. Wanampa maziwa kila siku, siku 365 kwa mwaka.

Pia ana mbuzi 20 hivi, maziwa ya mbuzi kwa ujumla hayakuchukuliwa kuwa mazuri, pengine kutokana na wingi wa maziwa ya ng'ombe, kwa hivyo hawakuwahi kukamua mbuzi. Wangeuza wachache ili kuongeza mapato kutoka kwa mazao mengine ili kuwapeleka watoto wao shule. Pia walifuga kuku kadhaa, zaidi kama hobi.

Mahamba yalizalisha zaidi kuliko walivyoweza kutumia. Waliuza ziada ili kumudu huduma muhimu kama vile mafuta ya taa (siku hizi wanatumia Solar), sabuni, sukari (katika umri wao hawakutumia sukari tena, walitumia asali - maagizo ya daktari).

Mashambani kulikuwa na miwa ya kutosha (ya kula, si ya kutengeneza sukari) na miti ya matunda (mapera, maembe, papai, parachichi, machungwa, pasheni, nanasi). Walikunywa juisi safi kutoka kwa maembe na matunda ya passion.

Kama inavyoonekana, kila kitu hapa ni kwa msingi wa kujikimu, siyo biashara, na vyote hapa ni vyakula na maisha ya asili. Na hapa utakuta mzee ana miaka 75 akiwa na maisha hayahaya na bado anadunda.

IMG_20221021_204105.jpg
 
Maisha hayajawahi kuwa rahisi tangu binadamu wa kwanza kinacho badiila ni mitindo ya maisha.
 
Zamani palikua rahaaa sana hasa kwa watu tulio toka mikononi mwa wakulima na wafugaji ...maaana msosi upo wa mwaka mzima maziwa unakunywa mpaka basi sema sasa hivi mabadiliko ya dunia hasa upande wa mazingira ndo umeharibu sana maisha...
 
Y
Hongera mkuu, haya maisha ukiyaishi dunia ya sasa wewe ni bonge la tajiri..
ni hivi kwetu babu yangu anaheka nyingi za mashamba, alafu yapo kwenye udongo wenye rutuba nyingi kwaiyo kila mjukuu wake kampa mashamba,mimi nimefuga mifugo kama kuku,mbuzi,ngombe,bata mzinga na nimelima migomba,miwa,nyanya,matunda nimelima pia kwa sababu shamba langu lipo.pemben ya mto
 
Mfumo huo haujabadilika nenda madafu huko ya mlandizi au pale vikindu na kisemvule nunua eneo lako la ekari mbili au tatu, hapo kama unaweza zungushia fence hata ya nyaya tu, chimba kisima cha maji, weka na matenki kama 4 au 5 ya akiba ya maji, tafuta solar zako za kutosha, jenga nyuma yako room tatu au nne, jenga mabanda yako mazuri tu makubwa kwa kuyatenganisha, yawe manne moja weka kuku wa kienyeji wengi kachukue tabora au singida, la pili weka mbuzi wengi wazaliane kanunue Kondoa huko, ng’ombe nunua manyoni january au february wanakua chini sana mbegu ya kisukuma ukiendelea katafute nyankole kadhaa za rwanda au uganda utazipata ngara, karagwe au benaco leta mwaga hapo, kwenye eneo lako panda majani ya kulishia mifugo yapo yale mazuri uahkikishe unakua unavuna kwa awamu awamu ili ulishie mifugo yako, banda lingine fuga hata kondoo, baada ya hapo tafuta oda sehemu uwe unachukua pumba, na chimvu kwa ajili ya mifugo yako, eneo lingine upande nyanya chungu, karoti, hoho kisasa hizi utakua unauza kwa wachuuzi tena watakuja shambani kabisa, nenda SUA morogoro beba miche ya miembe, parachichi, nanasi, chungwa, chenza panda na uhudumie iwe miche mingi hapa napo utauza matunda vizuri, usisahau kupanda limao, hua zinasoko wakati fulani na kwakua uko labda ukanda wa pwani weka minazi pia yaani unamalizia na pickup yako single au townaice moja kubwa kubwa ya kubebea vitu vya hapa na pale, hapo utakua mwenyeji unatafuta mashamba upande na mihogo mitamu ya kula na mikorosho kadhaa, kwa hiyo mwaka mzima unavitu vya kuuza, miaka mitano mbele ushakua mkulima mkubwa na mwenye maisha mazuri na unakula vitu organic maana mbolea hautumii haya ya kisasa maana mifugo yako ndio itakupa mbolea unajiongeza hata kupanda mahindi ya kuchoma maana wanachoma mwaka mzima kwahiyo nayo utauza maana utakua ushaongeza mashamba na mradi umekua mkubwa
 
Mfumo huo haujabadilika nenda madafu huko ya mlandizi au pale vikindu na kisemvule nunua eneo lako la ekari mbili au tatu, hapo kama unaweza zungushia fence hata ya nyaya tu, chimba kisima cha maji, weka na matenki kama 4 au 5 ya akiba ya maji, tafuta solar zako za kutosha, jenga nyuma yako room tatu au nne, jenga mabanda yako mazuri tu makubwa kwa kuyatenganisha, yawe manne moja weka kuku wa kienyeji wengi kachukue tabora au singida, la pili weka mbuzi wengi wazaliane kanunue Kondoa huko, ng’ombe nunua manyoni january au february wanakua chini sana mbegu ya kisukuma ukiendelea katafute nyankole kadhaa za rwanda au uganda utazipata ngara, karagwe au benaco leta mwaga hapo, kwenye eneo lako panda majani ya kulishia mifugo yapo yale mazuri uahkikishe unakua unavuna kwa awamu awamu ili ulishie mifugo yako, banda lingine fuga hata kondoo, baada ya hapo tafuta oda sehemu uwe unachukua pumba, na chimvu kwa ajili ya mifugo yako, eneo lingine upande nyanya chungu, karoti, hoho kisasa hizi utakua unauza kwa wachuuzi tena watakuja shambani kabisa, nenda SUA morogoro beba miche ya miembe, parachichi, nanasi, chungwa, chenza panda na uhudumie iwe miche mingi hapa napo utauza matunda vizuri, usisahau kupanda limao, hua zinasoko wakati fulani na kwakua uko labda ukanda wa pwani weka minazi pia yaani unamalizia na pickup yako single au townaice moja kubwa kubwa ya kubebea vitu vya hapa na pale, hapo utakua mwenyeji unatafuta mashamba upande na mihogo mitamu ya kula na mikorosho kadhaa, kwa hiyo mwaka mzima unavitu vya kuuza, miaka mitano mbele ushakua mkulima mkubwa na mwenye maisha mazuri na unakula vitu organic maana mbolea hautumii haya ya kisasa maana mifugo yako ndio itakupa mbolea unajiongeza hata kupanda mahindi ya kuchoma maana wanachoma mwaka mzima kwahiyo nayo utauza maana utakua ushaongeza mashamba na mradi umekua mkubwa
Bonge la idea,hii inahitaji kichwa kiwe timamu,tena uwe na daftari. Ufuate hatu kwa hatua
 
Back
Top Bottom