Maaskofu wasiingilie mambo ya siasa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,883
Idadi kubwa ya vyuo mbalimbali vikiwemo vya ufundi na ualimu vimejengwa na kanisa. Hospitali mbalimbali na zahanati zinaendeshwa na maaskofu. Miradi mbalimbali ya umeme vijijini imeanzishwa na kuhudumiwa na maaskofu.
Viongozi wengi hapa nchini wamesoma katika shule na vyuo vilivyojengwa na kanisa.

Nashangaa leo CCM ikisema maaskofu wavue majoho maana yake wafunge shule, vyuo, hospitali, dispensary, nk
 
Maaskafu Sio Wananchi? Hao Maaskofu Walipo Kuwa Wanakwenda Ikulu na Sherehe za CCM, Haikua Uchanganyaji wa Siasa? CCM Msibabaishe Wananchi na Ujinga Wenu wa Kutaka Kufunga Midomo Maaskofu na Wapenda Imani Zao. JK Anataka Waislamu Wajione Kama Wakristo Hawampendi JK Kwa Sababu ya Imani Zao. Ujinga Mtupu, Nakumbuka JK Alikuwa Anapenda Sana Sifa za Maaskofu Leo Wamemgeuka kwa Wizi Wake na Sifa Mbaya za Uongozi, Anaanza Chuki Nao. Watanzania Hatuchagui Kiongozi kwa Kuangalia Dini Zao na JK Alipata Kura Nyingi Sana Hawamu ya Kwanza na Sasa Tume Mgundua ni "JK is One of the Corrupt Person in Tanzania and Has Very Very Poor Leadership Skills" It's Over CCM...
 
Only one who devotes himself to a cause with his whole strength and soul can be a true master. For this reason mastery demands all of a person. Hakuna kurudi nyuma

 
Idadi kubwa ya vyuo mbalimbali vikiwemo vya ufundi na ualimu vimejengwa na kanisa. Hospitali mbalimbali na zahanati zinaendeshwa na maaskofu. Miradi mbalimbali ya umeme vijijini imeanzishwa na kuhudumiwa na maaskofu.
Viongozi wengi hapa nchini wamesoma katika shule na vyuo vilivyojengwa na kanisa.

Nashangaa leo CCM ikisema maaskofu wavue majoho maana yake wafunge shule, vyuo, hospitali, dispensary, nk

mkuu uzi wako uko na utata.............

sasa kwa mfano kama mimi nikiuliza: mashehe na maimamu wamejenga nini? utanijibu nini?
 
CCM $ Co iache ubaguzi kwa raia wa nchi hii ya kushiriki siasa ni Lazima pia haki yao ya msingi na kiraia kwa MAASKOFU Kushiriki siasa kama katiba ya nchi inavyo ainisha anaye wazuia anavunja katiba ASHUGHULIKIWE Kwa mujibu wa Katiba!
 
Nafikiri kuna sababu kubwa ya kuuwambia wasiingilie siasa, kwani wao wana ushawishi mkubwa wa kiroho na mtu yuko tayari kufa kwa imani yake ya kiroho kuliko kufa kwa ajili ya CCM au CHADEMA kwani hivi ni vikundi vya mpito tu leo vipo kesho havipo. Ndio maana nchi zote za Demokrasia watu wa dini wanawekwa pembeni washughulikie wafuasi wao kiroho, kama wanataka kuingia kwenye siasa inawabidi waache kimoja.

Taasisi za kidini zinapewa upendeleo wa kodi kwa ajili ya hili. Sasa kweli wakijiingiza na kuanza kutoa matamshi yasiyokuwa neutral nchi inaweza ikawaka moto, kwani wakijibiwa wasijifanye kwamba hawewezi kukosolewa, nchi itagawanyika kwani Waislamu kamwe haitawaona kuwa wako kupigania interest zao. Tusijidanganye kila mtu anajua viongozi wote wa dini wanataka upande wao ndio uwe mbele awe mkristo au muislamu, sasa awa maaskofu wasipokuwa makini tutageuka Lebanon... Ndiyo maana Nyerere licha kuwa mkatoliki mzuri lakini hakuwaachia maaskofu na mashekhe kuzungumzia siasa na aliondoa sensa ya idadi ya wakristo na waislamu tangu 1967 kwa kuona mbali. Sasa watu wasiokuwa na busara wanataka kuliamsha zimwi ambalo litaiangamiza Tanzania wasipotumia akili. Maaskofu na Mashekhe wanatakiwa kuwa waleta amani katika jamii na sio kuchochea uhasama kutokana na kutofautiana kimawazo kidini au kisiasa .
 
Nafikiri kuna sababu kubwa ya kuuwambia wasiingilie siasa, kwani wao wana ushawishi mkubwa wa kiroho na mtu yuko tayari kufa kwa imani yake ya kiroho kuliko kufa kwa ajili ya CCM au CHADEMA kwani hivi ni vikundi vya mpito tu leo vipo kesho havipo. Ndio maana nchi zote za Demokrasia watu wa dini wanawekwa pembeni washughulikie wafuasi wao kiroho, kama wanataka kuingia kwenye siasa inawabidi waache kimoja.

Taasisi za kidini zinapewa upendeleo wa kodi kwa ajili ya hili. Sasa kweli wakijiingiza na kuanza kutoa matamshi yasiyokuwa neutral nchi inaweza ikawaka moto, kwani wakijibiwa wasijifanye kwamba hawewezi kukosolewa, nchi itagawanyika kwani Waislamu kamwe haitawaona kuwa wako kupigania interest zao. Tusijidanganye kila mtu anajua viongozi wote wa dini wanataka upande wao ndio uwe mbele awe mkristo au muislamu, sasa awa maaskofu wasipokuwa makini tutageuka Lebanon... Ndiyo maana Nyerere licha kuwa mkatoliki mzuri lakini hakuwaachia maaskofu na mashekhe kuzungumzia siasa na aliondoa sensa ya idadi ya wakristo na waislamu tangu 1967 kwa kuona mbali. Sasa watu wasiokuwa na busara wanataka kuliamsha zimwi ambalo litaiangamiza Tanzania wasipotumia akili. Maaskofu na Mashekhe wanatakiwa kuwa waleta amani katika jamii na sio kuchochea uhasama kutokana na kutofautiana kimau .
kumbuka mkuu kuwa roho inakaa kwenye mwili
 
huyo anayesema maaskofu wasiingilie mambo ya siasa , kwa nini NEC iliwapa kazi ya kisiasa kutoa elimu ya uraia wakati wa uchaguzi 2010 ???
 
huyo anayesema maaskofu wasiingilie mambo ya siasa , kwa nini NEC iliwapa kazi ya kisiasa kutoa elimu ya uraia wakati wa uchaguzi 2010 ???

Nakupata Muadhamu Askofu Msaidizi, kutoa elimu ya urai si kujingiza moja kwa moja katika dimbwi la ushindani wa kisiasa, kwani kutoa elimu ya urai unasimamia katika ukweli halisi ("based on facts"), malumabano na mashindano ya kisiasa yanasimama katika uwongo (lies), kupindisha ukweli (exaggerations), kashifa (innuendos) na ahadi za uwongo ( false promises) na ubabe wa kweli au tisha toto (literal or metaphoric threats ) na ukweli kidogo.
 
Nadhani kwa kuanza CCM wasingemteua mama Lwakatare kuwa mbunge.
 
Nafikiri kuna sababu kubwa ya kuuwambia wasiingilie siasa, kwani wao wana ushawishi mkubwa wa kiroho na mtu yuko tayari kufa kwa imani yake ya kiroho kuliko kufa kwa ajili ya CCM au CHADEMA kwani hivi ni vikundi vya mpito tu leo vipo kesho havipo. Ndio maana nchi zote za Demokrasia watu wa dini wanawekwa pembeni washughulikie wafuasi wao kiroho, kama wanataka kuingia kwenye siasa inawabidi waache kimoja.

Taasisi za kidini zinapewa upendeleo wa kodi kwa ajili ya hili. Sasa kweli wakijiingiza na kuanza kutoa matamshi yasiyokuwa neutral nchi inaweza ikawaka moto, kwani wakijibiwa wasijifanye kwamba hawewezi kukosolewa, nchi itagawanyika kwani Waislamu kamwe haitawaona kuwa wako kupigania interest zao. Tusijidanganye kila mtu anajua viongozi wote wa dini wanataka upande wao ndio uwe mbele awe mkristo au muislamu, sasa awa maaskofu wasipokuwa makini tutageuka Lebanon... Ndiyo maana Nyerere licha kuwa mkatoliki mzuri lakini hakuwaachia maaskofu na mashekhe kuzungumzia siasa na aliondoa sensa ya idadi ya wakristo na waislamu tangu 1967 kwa kuona mbali. Sasa watu wasiokuwa na busara wanataka kuliamsha zimwi ambalo litaiangamiza Tanzania wasipotumia akili. Maaskofu na Mashekhe wanatakiwa kuwa waleta amani katika jamii na sio kuchochea uhasama kutokana na kutofautiana kimawazo kidini au kisiasa .

Tunapowaongelea maaskofu tujaribu kuelewa sana kazi zao, Maskofu wanaiongoza na kuihudumia jamii Kiroho na Kimwili maana Huwezi kutenganisha mwili na roho.
Hivyo wanayo haki ya kuikemea serikali maana Nchi ya MUNGU na serikali huwekwa na MUNGU. Na ukiingia ndani zaidi Rais au kiongozi yeyote wa serikali yu chini ya uangalizi wa viongozi wa kidini. Ndiyo maana machifu na watemi zamani hawakufanya jambo lolote bila baraka za ma priest vinginevyo mambo yalienda ovyo.
 
Hivi ni nani asijua mchango wa Rev Desmond Tutu katika maendeleo ya nchi yake S.A.????!!! Mnasema viongozi wa dini wana ushawishi mkubwa sawa kama Kiongozi wa kisiasa he is doing right things nani atamkusoa???? Viongozi wa kidini ni viongozi wa kiroho! Lakini roho bila mwili haitawaliki!!!! Ni jukum la viongozi wa dini kuona kuwa wafuasi wao wanakuwa na hali nzuri kimwili (of which is Siasa) ili roho ziwe salama zaidi. After all misikiti au makanisa si vyombo vya dola!!! Ni taasisi zinazo hubiri amani. Kwa hiyo whoever ambae anahatarisha amani lazima akemewe!!!! Hili la ku - exempt viongozi wa dini kwenye siasa mimi linanikera sana!!! Ni kuwanyima haki yao ya kimsimgi viongozi hao, ambao mchango wao wa maendeleo katika jamii ni mkubwa.
 
Sasa Tume Mgundua ni "JK is One of the Corrupt Person in Tanzania and Has Very Very Poor Leadership Skills" It's Over CCM...

nikweli kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, kila kona watu wanalalamika, wanamsutumu but he never say a thing, he is just quite like nothing is hapenning.
 
Jamani kwa nijuavyo mimi jk nyerere hakuwahi kuruhusu kitu kama hii kamwe, nirahisi kumchagua kiongozi wa dini kuwa kiongozi wa kisiasa kwa elimu yake, na si kuacha viongozi wa dini sasa kuropoka kila kitu bila kujali athari zake kwa jamii.
Haiwezekani leo hii viongozi wa dini wamegeuka utadhani ngos za akina ananilea nkya, wamesahau kabisa wajibu wao makanisani na misikitini kuwa wanamzigo mzito ktk jamii kwa kuanza kuwaweka sawa waumini wao ktk nyumba za ibada maana hao mafisadi ndio waumini na kondoo zao wanao wachunga huko, na anguko la maadili linaanzia kwao.
Kadri siku zinavyo kwenda ndio hali inazidi kuwa mbaya imefikia sasa viongozi wa dini wamekuwa watoa matamko kila panapotokea issue kubwa ya kisiasa, pengine kosa lilianza pale jk alipo kaa kimya baada ya kuambiwa yeye ni chaguo la mungu na sasa hao hao wamekuja kumuona mtu alieshindwa kuongoza nchi(si dhani kama Mungu mpuuzi namna hii), nahii ni kuwa ktk siasa hakuna rafiki wa kudumu na ndio maana tunao tazama mbali hatukubaliani na viongozi wa dini kuwa wasemaji wa mambo ya kisiasa. lazima wajue kuwa wao ni tofauti na vyama vya siasa au ngos.
Mambo ya kidini ni zaidi ya upeo wa kawaida wa mtazamo, ni imani inayogusa hisia kali inayoweza kupelekea hata mtu kufanya mambo ya ajabu.
Warudi ktk nyumba za ibada na wa play part yao kama viongozi wa dini kwa kuwasimamia vizuri waumini wao wawe bora na watii maana katika hao ndio tutapata viongozi bora toka kwao.
 
Tunapowaongelea maaskofu tujaribu kuelewa sana kazi zao, Maskofu wanaiongoza na kuihudumia jamii Kiroho na Kimwili maana Huwezi kutenganisha mwili na roho.
Hivyo wanayo haki ya kuikemea serikali maana Nchi ya MUNGU na serikali huwekwa na MUNGU. Na ukiingia ndani zaidi Rais au kiongozi yeyote wa serikali yu chini ya uangalizi wa viongozi wa kidini. Ndiyo maana machifu na watemi zamani hawakufanya jambo lolote bila baraka za ma priest vinginevyo mambo yalienda ovyo.

Nakupata Mkuu, lakini kumbuka kiongozi wa kiroho anapokuwa hayuko neutral katika ugomvi wa kisiasa na kuunga chama kimoja cha kisiasa hathari zake ni kuwa wafuasi wa dhehebu lakini humfuata kama kondo bila ya kupima hoja na kutumia akili zao wao wenye kupambua mambo kwani wengi wanamchukulia mchungaji kama ndio neno lenyewe, kwahiyo upande unaoungwa mkono na askofu uwambatanishwa na ukweli wa neno wakati hali halisi ni kuwa maaskofu ni kama mimi na wewe wanafanya upenzi kutokana na hisia maslahi yao na wafuasi wao. Sasa kila dhehebu likifanya hivyo kutakuwa hukutawaliki Tanzania. Waislamu watafuata matamshi ya viongozi wao, wakristo na ndio hivyo wamekwisha anza basi nchi itaparaganyika.
 
Tatizo CCM likifanyika jambo baya utasikia wanasema watu wasilihusishe na CCM ila Serikali likitokea jambo zuri utasikia CCM wanakwambia hiyo ni moja ya ilani yao iliyoko kwenye chama chao CCM.
 
Back
Top Bottom