Maaskofu wamshambulia Kikwete

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
• Wamuonya asiilipe Dowans kwa vile alishaikana

na Danson Kaijage, Dodoma
Tanzania Daima


MAASKOFU wa Kanisa la Christian Mission Fellowship (CMF), wamesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete, kuendelea kuwakumbatia watuhumiwa wa ufisadi ndani ya serikali yake kinazidi kuwaangamiza Watanzania kwa umaskini.

Mbali na lawama hizo, pia wamesema kuwa kanisa hilo litaungana na wanaharakati wa kweli na wapenda maendeleo nchini ili kuhakikisha wanaipinga serikali kulipa deni la Dowans la sh bilioni 94.

Maaskofu hao, walitoa kauli hizo jana mjini hapa wakati wa ibada maalumu ya kumsimika Makamu Askofu Mkuu wa Kanisa hilo nchini, Askofu Dorlinad Mhango, iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa CMF, Dk. Mungulu Kilimba.

Kauli hiyo inakuja siku chache tangu Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, isajili tuzo ya Dowans iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), ikilitaka Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO), kulipa fidia hiyo kutokana na kosa la kuvunja mkataba baina yake ya kampuni ya Dowans Tanzania.

Askofu Kilimba alisema kuwa inashangaza kuona serikali inaridhia kulipa deni hilo haraka wakati haina fedha za kuendeshea shughuli mhimu za kimaendeleo za kumkomboa Mtanzania anayeishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku.

Alibainisha kuwa kanisa hilo, kamwe halitanyamazia kitendo hicho na hivyo lazima waungane na wanaharakati nchini kuhakikisha wanapinga ulipwaji wa fedha hizo licha ya ICC kutoa hukumu ya kuitaka TANESCO kulipa fidia hiyo.

"Kamwe viongozi wa dini hatuwezi kunyamaza juu ya hili, kwani tunajiuliza kuna nini hadi serikali iridhie haraka kulipwa kwa fedha hizo wakati kuna matatizo mengi ambayo yanatakiwa kutatuliwa," alihoji askofu huyo na kuongeza:

"Watanzania wangapi wanaishi chini ya dola moja kwa siku na hawajui hatma ya maisha yao, hawana umeme, huduma za afya ni mbovu halafu inakuwaje serikali iwe tayari kulipa deni la Dowans upesi na kuacha kushughulikia matatizo mengine muhimu? Sisi kama kanisa hapa hatuwezi kunyamaza."

Aliitaka serikali kuueleza umma wazi wazi ni wapi fedha hizo za kuilipa Dowans zinatoka na zinalipwa kwa nani ikiwa viongozi wote wa juu akiwemo Rais Jakaya Kikwete, walikiri kuwa hawawajui wamiliki wa kampuni hiyo.

"Jamani ndugu zangu lazima tujiulize kuna nini kati ya serikali na Dowans? Wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hadi leo wanaandamana hadi kulala barabarani hawajalipwa madeni yao, lakini leo hii serikali inaharakisha kulipa deni la Dowans, hii haiwezi kukubalika kirahisi na ni haki yetu kuhoji na kuungana na wanaharakati wa kweli wapenda maendeleo kupinga malipo hayo," alisisitiza askofu huyo.

Katika hatua nyingine, Askofu Kilimba aliwataka watumishi wa kanisa hilo kuhakikisha wanasema ukweli juu ya mambo yanayokwenda kinyume na matarajio ya nchi hasa suala la rushwa, ufisadi na viongozi wa serikali kujilimbikizia mali wakati Watanzania wengi wanakufa kwa umaskini.

"Viongozi wa dini ni lazima kuikosoa serikali bila woga kwani sisi ndiyo kazi kubwa tunayotakiwa kuifanya, sasa angalia viongozi wa serikali wanavyojichukulia mali pamoja na kuingia mikataba mibovu na kulisababishia taifa janga kubwa la umaskini na madeni. Lazima tupige kelele kwa ajili ya kufanya mabadiliko," alisisitiza Askofu Kilimba.

Kwa upande wake, Makamu mpya wa Askofu Mkuu, Mhango, alisema kuwa kinachosababisha umaskini nchini ni Rais Kikwete kutokuwa na maamuzi kwa viongozi aliowachagua.

Askofu Mhango alisema Rais Kikwete ameshindwa kuwa na maamuzi magumu ya kuwawajibisha watendaji wazembe na wale ambao si waaminifu na badala yake amekuwa kinara wa kuwakumbatia.

"Wapo watumishi wengi ambao amewateua kushika nyadhifa mbalimbali ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi lakini Rais amewakumbatia anashindwa kutoa maamuzi magumu kwa lengo la kunusuru nchi katika janga la umaskini uliopindukia.

"Kuna jamaa zake wengi ambao wanatuhumiwa kwa rushwa lakini amewakumbatia. Pamoja na kutoa misemo ya kujivua gamba lakini hizo ni porojo tu wakati Watanzania wakizidi kuangamia," alisema Mhango.

Askofu Mhango alisema kwa nafasi yake, atahakikisha anazungumza na serikali kwa kuitaka ijenge viwanda vikubwa na vidogo ambavyo ni vya ndani ili kuepukana na taifa kugeuzwa dampo la kutupa takataka kutoka nje ya nchi.
 
Ndio hivyo kaka, Kama unaikumbuka hii ya Mh David Kafulila "Serikali legelege ufanya mambo legelege" wakamkomalia wee! lakini ukweli unabaki palepale!
 
mie nangojea tamko la bakwata nione litakuwa na mlengo wa kidini au kutetea maslahi ya taifa, tusubiri

Wale hata siku moja hawatatoa kauli yoyote ya kumpinga Kikwete ukiondoa ile issue ya mahakama ya Kadhi. Yaani utadhani kama nchi kwenda mrama hakuwagusi kabisa wao. Nimejaribu kutafuta kama Bakwata wameshatoa tamko lolote lile la kupinga malipo ya Dowans lakini sikuambua kitu, labda siku za usoni nao watafanya hivyo.
 
mie nangojea tamko la bakwata nione litakuwa na mlengo wa kidini au kutetea maslahi ya taifa, tusubiri

kila siku matamko tu! Mda umefika tunahitaji matendo. Maaskofu na mapadri na mashehe muandae maandamano nchi nzima tumfukuze jakayaa. Nafikili hapo inakuwa ni nchi nzima imeandamana maana naamini kila mtu ana dini. Matamko hayasaidii bali yanawapa mafisadi njia mbadala ya kuiba.
 
kila siku matamko tu! Mda umefika tunahitaji matendo. Maaskofu na mapadri na mashehe muandae maandamano nchi nzima tumfukuze jakayaa. Nafikili hapo inakuwa ni nchi nzima imeandamana maana naamini kila mtu ana dini. Matamko hayasaidii bali yanawapa mafisadi njia mbadala ya kuiba.
Muda wa matamko ushapita,umebaki muda wa vitendo,BAKWATA wao ni kujipendekeza na kujikomba kwa serikali kituambacho ni makosa kwa mujibu wa Qur an na hadth
 
mapinduzi ya kweli 2015 tunaitaji mshikamano maana kwa mwendo huu wa magamba tutakuwa maskini milele.
 
kila siku matamko tu! Mda umefika tunahitaji matendo. Maaskofu na mapadri na mashehe muandae maandamano nchi nzima tumfukuze jakayaa. Nafikili hapo inakuwa ni nchi nzima imeandamana maana naamini kila mtu ana dini. Matamko hayasaidii bali yanawapa mafisadi njia mbadala ya kuiba.

utashambuliwa kwa tuhuma za udini best
 
Maisha yetu,ya watoto wetu, na wajukuu zetu yanategemea uamuzi wetu na matendo yetu ya sasa. Hata humu jf watu ni waongeaji zaidi kuliko vitendo na hata kwenye vitendo tunawaachia watu wachache saana, hatutafika kwa njia hiyo.
Cha kufanya tupange siku moja tunakutana wapi na tuwe wote tuanze harakati za maandamano ya kweli kuna baadhi yetu tutakufa ili wengine wawe huru.
 
naomba tarehe itajwe tukutane pale jangwani ili tujadili hatima ya nch yetu na vizazi vyetu.niko tayari kulipia vyombo vya muziki kwa ajili ya kutumika siku hiyo pale Jangwani,.
 
Alikuja Mwinyi akalaumiwa, akaja Mkapa watu wakasema afadhali Mwinyi, Akaja Kikwete mkasema walau Mkapa kesho mtasema angalau Kikwete. Hapa hata wewe ukipewa shavu utakula tuu. Ufisadi upo palepale lililopo tufanye kazi na viongozi waoneshe njia
 
sijasema afadhali fulani ninachosema tukutane pale jangwani tujadili hatima ya Taifa letu na vizazi vyetu.kogoamano ambalo ahlina sura ya chama chochote yatakayojadiliwa hapo tutajulishana Lakini mloja kubwa ni Wizi,ubadhirifu,ufisadi,rushwa,uwajibikaji,utawala wa sheria,Wapi tunataka kuelekea kesho Tanzania
 
Wale hata siku moja hawatatoa kauli yoyote ya kumpinga Kikwete ukiondoa ile issue ya mahakama ya Kadhi. Yaani utadhani kama nchi kwenda mrama hakuwagusi kabisa wao. Nimejaribu kutafuta kama Bakwata wameshatoa tamko lolote lile la kupinga malipo ya Dowans lakini sikuambua kitu, labda siku za usoni nao watafanya hivyo.

Kosa lingine kubwa serikali ya CCM chini ya kikwete linafanyika ni kujiweka kando na marumbano ya kidini ambayo sasa yanashika kasi, serikali inakaa kimya kana kwamba haijui athari za machafuko ya kidini. KIKWETE NI MWOGA NA SI JASIRI.
 
Unafikiri Rostam alikubali kupiga kampeni Igunga hivi hivi? ilikuwa ni baada ya kuhakikishiwa malipo yatapita immediately! ndo TZ yetu hiyo na JK hajaesema tena kama sasa amewajua wamiliki wa Dowans ama bado
 
• Wamuonya asiilipe Dowans kwa vile alishaikana

na Danson Kaijage, Dodoma
Tanzania Daima


MAASKOFU wa Kanisa la Christian Mission Fellowship (CMF), wamesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete, kuendelea kuwakumbatia watuhumiwa wa ufisadi ndani ya serikali yake kinazidi kuwaangamiza Watanzania kwa umaskini.

Mbali na lawama hizo, pia wamesema kuwa kanisa hilo litaungana na wanaharakati wa kweli na wapenda maendeleo nchini ili kuhakikisha wanaipinga serikali kulipa deni la Dowans la sh bilioni 94.

Maaskofu hao, walitoa kauli hizo jana mjini hapa wakati wa ibada maalumu ya kumsimika Makamu Askofu Mkuu wa Kanisa hilo nchini, Askofu Dorlinad Mhango, iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa CMF, Dk. Mungulu Kilimba.

Kauli hiyo inakuja siku chache tangu Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, isajili tuzo ya Dowans iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), ikilitaka Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO), kulipa fidia hiyo kutokana na kosa la kuvunja mkataba baina yake ya kampuni ya Dowans Tanzania.

Askofu Kilimba alisema kuwa inashangaza kuona serikali inaridhia kulipa deni hilo haraka wakati haina fedha za kuendeshea shughuli mhimu za kimaendeleo za kumkomboa Mtanzania anayeishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku.

Alibainisha kuwa kanisa hilo, kamwe halitanyamazia kitendo hicho na hivyo lazima waungane na wanaharakati nchini kuhakikisha wanapinga ulipwaji wa fedha hizo licha ya ICC kutoa hukumu ya kuitaka TANESCO kulipa fidia hiyo.

"Kamwe viongozi wa dini hatuwezi kunyamaza juu ya hili, kwani tunajiuliza kuna nini hadi serikali iridhie haraka kulipwa kwa fedha hizo wakati kuna matatizo mengi ambayo yanatakiwa kutatuliwa," alihoji askofu huyo na kuongeza:

"Watanzania wangapi wanaishi chini ya dola moja kwa siku na hawajui hatma ya maisha yao, hawana umeme, huduma za afya ni mbovu halafu inakuwaje serikali iwe tayari kulipa deni la Dowans upesi na kuacha kushughulikia matatizo mengine muhimu? Sisi kama kanisa hapa hatuwezi kunyamaza."

Aliitaka serikali kuueleza umma wazi wazi ni wapi fedha hizo za kuilipa Dowans zinatoka na zinalipwa kwa nani ikiwa viongozi wote wa juu akiwemo Rais Jakaya Kikwete, walikiri kuwa hawawajui wamiliki wa kampuni hiyo.

"Jamani ndugu zangu lazima tujiulize kuna nini kati ya serikali na Dowans? Wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hadi leo wanaandamana hadi kulala barabarani hawajalipwa madeni yao, lakini leo hii serikali inaharakisha kulipa deni la Dowans, hii haiwezi kukubalika kirahisi na ni haki yetu kuhoji na kuungana na wanaharakati wa kweli wapenda maendeleo kupinga malipo hayo," alisisitiza askofu huyo.

Katika hatua nyingine, Askofu Kilimba aliwataka watumishi wa kanisa hilo kuhakikisha wanasema ukweli juu ya mambo yanayokwenda kinyume na matarajio ya nchi hasa suala la rushwa, ufisadi na viongozi wa serikali kujilimbikizia mali wakati Watanzania wengi wanakufa kwa umaskini.

"Viongozi wa dini ni lazima kuikosoa serikali bila woga kwani sisi ndiyo kazi kubwa tunayotakiwa kuifanya, sasa angalia viongozi wa serikali wanavyojichukulia mali pamoja na kuingia mikataba mibovu na kulisababishia taifa janga kubwa la umaskini na madeni. Lazima tupige kelele kwa ajili ya kufanya mabadiliko," alisisitiza Askofu Kilimba.

Kwa upande wake, Makamu mpya wa Askofu Mkuu, Mhango, alisema kuwa kinachosababisha umaskini nchini ni Rais Kikwete kutokuwa na maamuzi kwa viongozi aliowachagua.

Askofu Mhango alisema Rais Kikwete ameshindwa kuwa na maamuzi magumu ya kuwawajibisha watendaji wazembe na wale ambao si waaminifu na badala yake amekuwa kinara wa kuwakumbatia.

"Wapo watumishi wengi ambao amewateua kushika nyadhifa mbalimbali ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi lakini Rais amewakumbatia anashindwa kutoa maamuzi magumu kwa lengo la kunusuru nchi katika janga la umaskini uliopindukia.

"Kuna jamaa zake wengi ambao wanatuhumiwa kwa rushwa lakini amewakumbatia. Pamoja na kutoa misemo ya kujivua gamba lakini hizo ni porojo tu wakati Watanzania wakizidi kuangamia," alisema Mhango.

Askofu Mhango alisema kwa nafasi yake, atahakikisha anazungumza na serikali kwa kuitaka ijenge viwanda vikubwa na vidogo ambavyo ni vya ndani ili kuepukana na taifa kugeuzwa dampo la kutupa takataka kutoka nje ya nchi.


Jamani JK, hawa watu wote wanalalamika kutochukua hatua kwa wasaidizi wako. Sikia kilio cha watu. Wanakupenda sana hawa ndio maana wanasema wazi bila unafiki.
 
Back
Top Bottom