Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Miezi mitatu iliyopita Tanzania ilishuhudia siasa za aina yake kutoka kwa Maaskofu hasa wa Kanisa Katoliki na Mapdre wake kutoa matamko kila siku. Ilikua ni vigumu siku ipite bila Kusikia Padre huyu wa TEC kasema hiki, mara wengine wakisema hawaogopi kufa wataendelea kusema tu.
Ilikua ni bandika bandua kwa matamko. Kuna watu wenye busara walihoji juu ya Viongozi wa dini kujiingiza moja kwa moja kwenye siasa na wengine waka ambiwa wavue majoho waingie kwenye siasa.
Kama haitoshi nao mashehe waliendelea kutoa matamko kupinga kinachosemwa na Maaskofu basi ikawa patashika kila kona ya Nchi. Wataalamu wa Masuala ya siasa wanasema naona hasira nyingi zilitokea kwenye uchaguzi wa Mwaka 2010 kwani nao walikua na Wagombea wao maeneo mbalimbali sasa hasira zimeshuka wameendelea na kazi yao ya kulea waumini wao.
Binafsi nawapa Hongera viongozi wote wa dini Maaskofu, mapdre na Mashekhe kwa kuamua sasa kufuata mambo ya kazi yenu na kuwaachia wanasiasa mambo yao. Hongera sana TEC na Pengo kwa kusikia maoni ya wadau mbalimbali.
Hongereni Maaskofu wa Arusha kwa kuamua kutulia. Tuna hitaji Tanzania ya Watanzania isiyokuwa na Mashinikizo ya Viongozi wa dini mbalimbali. Basi kila mtu atimize wajibu wake iwe kwa mwanasiasa, mkulima, mfanyakazi na Viongozi wa Serikali.
Tunahitaji Tanzania yenye amani na Tanzania yenye kutofautiana kwa hoja na sio misingi ya Ubaguzi wa Kidini na Makabila.
Viva Tanzania.
Ilikua ni bandika bandua kwa matamko. Kuna watu wenye busara walihoji juu ya Viongozi wa dini kujiingiza moja kwa moja kwenye siasa na wengine waka ambiwa wavue majoho waingie kwenye siasa.
Kama haitoshi nao mashehe waliendelea kutoa matamko kupinga kinachosemwa na Maaskofu basi ikawa patashika kila kona ya Nchi. Wataalamu wa Masuala ya siasa wanasema naona hasira nyingi zilitokea kwenye uchaguzi wa Mwaka 2010 kwani nao walikua na Wagombea wao maeneo mbalimbali sasa hasira zimeshuka wameendelea na kazi yao ya kulea waumini wao.
Binafsi nawapa Hongera viongozi wote wa dini Maaskofu, mapdre na Mashekhe kwa kuamua sasa kufuata mambo ya kazi yenu na kuwaachia wanasiasa mambo yao. Hongera sana TEC na Pengo kwa kusikia maoni ya wadau mbalimbali.
Hongereni Maaskofu wa Arusha kwa kuamua kutulia. Tuna hitaji Tanzania ya Watanzania isiyokuwa na Mashinikizo ya Viongozi wa dini mbalimbali. Basi kila mtu atimize wajibu wake iwe kwa mwanasiasa, mkulima, mfanyakazi na Viongozi wa Serikali.
Tunahitaji Tanzania yenye amani na Tanzania yenye kutofautiana kwa hoja na sio misingi ya Ubaguzi wa Kidini na Makabila.
Viva Tanzania.