Maaskofu waipinga CHADEMA...

Msikurupuke jaman kuchangia na kuwalaumu maaskofu bila kufwatilia kile kilichosemwa.Hajawakemea chadema bali vyama vyote.Huyu jamaa namkubal sio mnafk hata kidogo

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Mwambieni huyo Askofu aende Lumumba akachukue Buku 7

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Kwan hivi vikosi vya ulinzi binafsi kuwepo nchini inamaana polisi au jeshi hawapo au!!? Sasa kuna tatizo gani chama Kama cdm kuwa na kikosi cha kujilinda? Mim binafsi sitaki kabisaaa habari za maaskofu wachumia Tumbo ndio maana kanisa langu ni sebureni kwangu..... Ilaaaaa!!
 
Asanteni maaskofu, msg sent ila sidhani kama itafanyiwa kazi na hawa watu maana vichwa vyao vigumu sana.
Hana lo lote. Hawa ndiyo maaskofu wa Baali. Kiboko yao Eliya.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Hicho kikundi kipo.kwenye katiba ya Chadema.Viongozi wa dini wafanye tafiti badala ya kupotosha waumini wao

Hawana lolote ni unafiki tu na tabia ya kufikiri nusunusu! Kuhusu kushambuliliwa makanisa mbona waliwaambia waumini wao kuwa wayalinde makanisa? Huko sio kuanzisha vikundi vya ulizi?
 
hajatamka hata neno moja kuhusu chadema hapo. au mtu akisema vyama vya siasa anamaanisha chadema?

mkuu ligangaluma, inaonekana ameisema cdm kwa sababu wao ndio wametangaza rasmi kijilinda kwa kuanzisha kikundi red brigade ila tokea zamani kuna green gurd na blue gurd lkn askofu huyu hakuongea chochote ilona sawa tu. jamani mbona cdm mnaionea sana kuna nini?
 
Nono,

Nimekuelewa sana sana.Tulipiga kelele long time ago hata kabla ya katiba ya mwaka 2006 wakati CUF na CCM wakitunishiana misuli lakini hatukusikilizwa ikabidi nasi kuwa na ulinzi binafsi maana ilionekana order of the day
 
Last edited by a moderator:
Huyu ni mmoja wa maaskofu dhaifu waliopata kutokea nchini hatutaki kuwasema watumishi hawa lkn maadamu kaja acha imnyeshee ajifunze, uchaguzi uliomwingiza madarakani katika Dayosisi ya Dodoma ulileta manunguniko kutokana na uwezo wake kuwa mdogo kulinganisha na washindani wake haswa Mchungaji Mshana ambaye ndiye msaidizi wa Askofu,kinyunyu alipitiswa kwa sababu ya utu uzima wakidhani atakuwa na busara nadhani sasa inabidi walitizame vizuri apishe mtu mwingine kwenye nafasi ile tunataka askofu asiyejifungamanisha na wanasiasa watawalao kwa nguvu ya damu na kuwananga wafuasi wa vyama vingine.
 


Wakati wa mlipuko wa bomu Arusha katika kanisa la Olasiti raisi aliwashauri viongozi wa kidini kuweka ulinzi binafsi katika nyumba za ibada.Kwani makampuni bonafsi ya ulinzi ambayo tunayaona yakilinda mabenki na silaha za kivita Askofu hayaoni?Au hayo makampuni sio vikundi vinavyomilikiwa na watu binafsi?Askofu rudi ukajipange na uhakikishe umeisoma katiba ya Jamhuri ya muungano Tanzania,kama unataka kuingia katika siasa karibu lakini kwa dizaini vile unachungulia haipendezi njoo mzima mzima habari ya kuwa vugu vugu Mungu hapendi kama unakuwa moto basi amua kuwa moto
 
Maaskofu wengine ni uchwara! Hata kakobe ni Askofu! Pamoja na ukristu wangu kuna maaskofu wengine ni uchwara sana..hasa wale wanaojiita ASKOFU!
 
Nadhani imefika wakati tuwe straight tuachane na generalization. Hawa ni watu wawili kati ya Maaskofu wengi sana kwa madhehebu ya Tanzania. Tunashindwa nini kutaja majina yao? Kama wangesema huo ni msimamo wa dhehebu lao (ref. Malasusa kama askofu mkuu wa ELCT) basi tungesema maaskofu wa dhehebu so and so. Hii kauli ya kuunganisha watu wote katika chungu kimoja ni ukihiyo wa hali ya juu wa waandishi wetu wa habari.

CC: JokaKuu
 

siyo maaskofu wa nchi hii mkuu .
 

uaskofu ni wake na mke wake na watoto wake na mawazo yake ni yake na ana haki ya kufanya hivyo lakini cc hatumjui na wala mawazo yake hayana mashiko kabisa yeye anatafuta bahati ya kuteuliwa kama lwakatare
 
hajatamka hata neno moja kuhusu chadema hapo. au mtu akisema vyama vya siasa anamaanisha chadema?
Kwanini aseme wakati huu ambapo CDM imeweka wazi kujilinda baada ya polisi kutowatendea haki.Labda kama ameyasema hayo wakati anasimikwa kuwa askofu tutamsamehe kwa kuwa ndo kwanza anaanza kazi, lakini kama alikuwepo hakuna namna ya kumtenganisha na wanafiki wengine.
 
Mbona hakuna walipotaja chama chochote. Ilivyokaa ni kuwa wanataka ujumbe ufike kwa vyama vyote na sio chama fulani
 
Tatizo la viongozi kama hawa ni UNAFIKI,Hawa ni mafarisayo wanaopenda kuvaa mavazi meupe wakati mioyo yao imekunjana na imeota fungus.Kwa nini mnashindwa kusema ukweli ya kwamba vyama vyote haviruhusiwi kuwa na vikundi vya ulinzi na kwa kuanzia Green Guard ifutwe ili na wengine wanaotaka kuanzisha wasifanye hivo? Mnahofia nini watumishi wa Mungu wakati Yesu aliteswa kwa ajili yetu sote?Mnamwogopa Mungu au Serikali? Siwaelewi hata kidogo! Ni kanisa gani mnaongoza la Mungu au la shetani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…