Maandamano ya raia Ufaransa yanafanana na yale katika tawala za kiimla kama Iran?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,625
46,270
Wale wanapropoganda local anti-west mnaopiga yowe kulazimisha kufananisha maandamano yanayoendelea Ufaransa na Israel na yale ya Iran au Arab spring ni vyema mkaelewa tofauti hizi.

1. Mpaka sasa hakuna waandamanaji waliouwawa na serikali zao katika haya maandamano zaidi sana waandamanaji hawawatafunguliwa kesi. Makadirio ya chini wa waliouwawa katika maandamano Iran ni raia 500, bunge la nchi hiyo lilipendekeza raia wengine 15,000 wapewe adhabu ya kifo.

2. Iran na nchi nyingine za kidikteta huwa wanapinga utawala mzima mbaya. Mfano Iran waandamanaji walikuwa wanapinga wanawake kulazimishwa kuvaa hijabu. Waandishi huko wanapinga mfumo mzima wa utawala ku control maisha yao binafsi juu ya dhuluma nyingine za uchumi na kijamii. Ufaransa waandamanaji hawataki tu kuongezewa muda wa kustaafu kufanya kazi kutoka miaka 62 hadi 64.

3. Raia wa nchi za kidikteta kama Iran hawana fursa ya kubadilisha sera au jinsi nchi zao zinaongozwa kidemokrasia. Ayatollah anayeamua kila kitu Iran ni kiongozi mkuu wa kudumu katika taifa hilo, njia pekee ya kubadilisha mambo ni kwa njia kama hizo za maandamano makubwa na uasi. Ufaransa raia wake wana fursa ya kubadilisha utawala kama hawapendi sera zinazopitishwa. Macron ni Rais wa kwanza wa Ufaransa kuchaguliwa kwa muhula wa pili baada ya miaka 20, hata hivyo mwaka 2027 utawala wake utafika tamati na raia wengi watakuwa na uwezo wa kumuweka mwingine wanayemtaka.
 
Maandamano yamekuwepo Ulaya tangu karne na karne. Huko Ufaransa waliwahi kuandamana hadi wakauondoa ufalme na wakamkata kichwa mfalme wao wa mwisho Louis XVI l.
La msingi ni kwamba hata kwao wameandamana maana wakiandamana kwingine full kunyoosha vidole sasa na huko mambo si mazuri nyoosheni vidole pia
 
Maandamano yamekuwepo Ulaya tangu karne na karne. Huko Ufaransa waliwahi kuandamana hadi wakauondoa ufalme na wakamkata kichwa mfalme wao wa mwisho Louis XVI l.
Na maelezo yako yanalenga nini? Yes, tunajua French revolution. Sasa kama maandamano yapo ulaya tangu na tangu kwanini wakiandamana Iran iwe kama jabu wafanye big deal out of it.
 
Watu kuandamana kupinga kulazimishwa kuvaa hijabu unaona sio Big deal ??
Na maelezo yako yanalenga nini? Yes, tunajua French revolution...
Sasa kama maandamano yapo ulaya tangu na tangu kwanini wakiandamana Iran iwe kama jabu wafanye big deal out of it.
 
Watu kuandamana kupinga kulazimishwa kuvaa hijabu unaona sio Big deal ??
Kila nchi ipambane na matatizo yake. Sio big deal kama ni mila zao mbona sisi tunapinga kulazimishwa kukubali ushoga?
 
Wale wanapropoganda local anti-west mnaopiga yowe kulazimisha kufananisha maandamano yanayoendelea Ufaransa na Israel na yale ya Iran au Arab spring ni vyema mkaelewa tofauti hizi.

1. Mpaka sasa hakuna waandamanaji waliouwawa na serikali zao katika haya maandamano zaidi sana waandamanaji hawawatafunguliwa kesi. Makadirio ya chini wa waliouwawa katika maandamano Iran ni raia 500, bunge la nchi hiyo lilipendekeza raia wengine 15,000 wapewe adhabu ya kifo.

2.Iran na nchi nyingine za kidikteta huwa wanapinga utawala mzima mbaya. Mfano Iran waandamanaji walikuwa wanapinga wanawake kulazimishwa kuvaa hijabu. Waandishi huko wanapinga mfumo mzima wa utawala ku control maisha yao binafsi juu ya dhuluma nyingine za uchumi na kijamii.
Ufaransa waandamanaji hawataki tu kuongezewa muda wa kustaafu kufanya kazi kutoka miaka 62 hadi 64.

3.Raia wa nchi za kidikteta kama Iran hawana fursa ya kubadilisha sera au jinsi nchi zao zinaongozwa kidemokrasia. Ayatollah anayeamua kila kitu Iran ni kiongozi mkuu wa kudumu katika taifa hilo, njia pekee ya kubadilisha mambo ni kwa njia kama hizo za maandamano makubwa na uasi. Ufaransa raia wake wana fursa ya kubadilisha utawala kama hawapendi sera zinazopitishwa. Macron ni Rais wa kwanza wa Ufaransa kuchaguliwa kwa muhula wa pili baada ya miaka 20, hata hivyo mwaka 2027 utawala wake utafika tamati na raia wengi watakuwa na uwezo wa kumuweka mwingine wanayemtaka.

Unaweza Kuwa Shabiki ukawa Na Mpumbavu usie Jitambua
Kinacho zungumzwa ni Nguvu inayo tumia Ufaransa dhidi ya Raia
Hatusikii Uk,Us wakitoa Matamko dhidi ya Serikali ya Ufaransa
Hatusikii Haki za Binadamu kukemea hilo

IMG_20230324_165159.jpg
IMG_20230324_165153.jpg



Hebu Niambie Umri wa Mzee kamaa huyu Kweli wakuburuzwa hivi?
Hili lingetokea Urusi,China au Africa nini Kingejiri
Wewe na Wapuuzi wenzie mngelikuwa Wakwanza Kuropoka kila Aina ya Utumbo humu

 
Hii picha moja ndio umeamua kuzunguka nayo wiki nzima sasa!
Poor you.
Unaweza Kuwa Shabiki ukawa Na Mpumbavu usie Jitambua
Kinacho zungumzwa ni Nguvu inayo tumia Ufaransa dhidi ya Raia
Hatusikii Uk,Us wakitoa Matamko dhidi ya Serikali ya Ufaransa
Hatusikii Haki za Binadamu kukemea hilo

View attachment 2567445View attachment 2567446



Hebu Niambie Umri wa Mzee kamaa huyu Kweli wakuburuzwa hivi?
Hili lingetokea Urusi,China au Africa nini Kingejiri
Wewe na Wapuuzi wenzie mngelikuwa Wakwanza Kuropoka kila Aina ya Utumbo humu

View attachment 2567449
 
Mnajitahidi sana kufichaficha na kutetea uovu unaofanywa na serikali ya ufaransa dhidi ya raia waandamanaji lkn ukweli unadhihiri,, sipati picha ingekuwa ndo Russian, China na Iran haya maandamano ndo yanafanyika zingefunguliwa nyuzi jf kutwa kucha, huko bbc cnn sikwambii.
 
Maandamano hayakulwenda vizuri kwa sababu hawakutegemea kuwa na utawala wa kidini wa ki Ayatollah. Ni kama vile Misri walivyomuondoa dikteta Mubarak wakishindwa kuelewana mpaka jeshi likamuweka dikteta mwingine Al Sisi.
Hata Iran waliwahi kuandamana na kumtoa Madarakani mfalme shaah na kibaraka mkubwa wa Marekani kwa hiyo hata Iran maandamano ni jadi yao.
Hiyo punguza ujuaji wa kifala.
 
Ni kwamba BBC au CNN hawaripoti au hujaridhishwa na jinsi wanavyoripoti hayo maandamano ya Ufaransa ??
Mnajitahidi sana kufichaficha na kutetea uovu unaofanywa na serikali ya ufaransa dhidi ya raia waandamanaji lkn ukweli unadhihiri,, sipati picha ingekuwa ndo Russian, China na Iran haya maandamano ndo yanafanyika zingefunguliwa nyuzi jf kutwa kucha, huko bbc cnn sikwambii.
 
Maandamano hayakulwenda vizuri kwa sababu hawakutegemea kuwa na utawala wa kidini wa ki Ayatollah. Ni kama vile Misri walivyomuondoa dikteta Mubarak wakishindwa kuelewana mpaka jeshi likamuweka dikteta mwingine Al Sisi.
Maandamano sio shida shida ni kupigwa waandamanaji. Hiyo haifai iwe imetokea Ufaransa au Irani au kokote kule. Kwa nini jeshi liwapige watu wanaoandamana bila silaha kwa amani!?

Tulitegemea hilo tulione kwa mapioneer wa demokrasia na uhuru wa kujieleza duniani. France & Co. Imekuwa ni kinyume chake na badala yake badala ya kukemea kama mnavyokemeaga kokote kule yanapotokea mnatafuta namna ya kuhalalisha.

Mapinduzi ya Irani hayana yanachofanana na mapinduzi ya Misri. Ukilazimisha kuyafananisha unaonekana hujui kitu. Na baada ya kuondolewa mubaarak hakufuata Al sisi ila Morsi. Na morsi hakuwekwa na jeshi bali uchaguzi mkuu. Alipoondolewa Morsi kwa maandamano ndipo jeshi likachukua nchi chini ya jenerali al sisi na baada ya muda ukafanyika uchaguzi na al sisi akaushinda. Na wala Al sisi sio dikteta as far as westerners are concerned!
 
Maandamano sio shida shida ni kupigwa waandamanaji. Hiyo haifai iwe imetokea Ufaransa au Irani au kokote kule. Kwa nini jeshi liwapige watu wanaoandamana bila silaha kwa amani!?

Tulitegemea hilo tulione kwa mapioneer wa demokrasia na uhuru wa kujieleza duniani. France & Co. Imekuwa ni kinyume chake na badala yake badala ya kukemea kama mnavyokemeaga kokote kule yanapotokea mnatafuta namna ya kuhalalisha.

Mapinduzi ya Irani hayana yanachofanana na mapinduzi ya Misri. Ukilazimisha kuyafananisha unaonekana hujui kitu. Na baada ya kuondolewa mubaarak hakufuata Al sisi ila Morsi. Na morsi hakuwekwa na jeshi bali uchaguzi mkuu. Alipoondolewa Morsi kwa maandamano ndipo jeshi likachukua nchi chini ya jenerali al sisi na baada ya muda ukafanyika uchaguzi na al sisi akaushinda. Na wala Al sisi sio dikteta as far as westerners are concerned!
Mpe shule huyo shabiki wa westerns anayejiita Yoda .
 
Maandamano hayakulwenda vizuri kwa sababu hawakutegemea kuwa na utawala wa kidini wa ki Ayatollah. Ni kama vile Misri walivyomuondoa dikteta Mubarak wakishindwa kuelewana mpaka jeshi likamuweka dikteta mwingine Al Sisi.
Hawakutegea ww unawasemea wairani kama nani?
Ww unaangalia tu upande wa wanao pinga utawala wa kidini ,vipi kuhusu wanao unga mkono utawala huo ,haki yao iko wapi au wao hawana haki?

Katika dunia yote hakuna serikali ambayo ilisha kukubalika kwa raia wote.

Ni kweli kuna mamilion ya Wairan wanaona mfumo wa kidini ni mbaya lakini wakati huo huo kumbuka kuna mamilion ya Wairan wanaona ni mfumo mzuri na unao faa kuongoza taifa lao hivyo na wao unatakiwa uwafikirie, hiyo ndio demokrasia na uhuru ambayo umekuwa ukihubili humu.

Hata ulaya kuna mamilion ya watu hawakubaliani na muundo unao ongoza mataifa yao lakini wakati huo kuna mamilion ya watu Ulaya wanaona mfumo unao ongoza sasa ni sahihi na ndio maana huo mfumo umeendelea kutawala.

Hapa tz kuna mamilion ya watz hawaitaki CCM lakini pia kuna mamilion ya wtz wanaipenda ccm na ndio maana mpaka sasa inatawala.

Hapo kenya asilimia 48 ya wakenya ambao ni mamilion ya wakenya wangetaka rais wao awe Odinga ,lakini kuna aslimia 50 ya wakenya ambao ni mamilion ya wakenya hawakumtaka Odinga awaongoze na ndio maana sasa hivi sio raisi.

Mamilion ya Wamarekani nalitaka Trump awe aendelee kuwa rais lakini pia kuna mamilion ya Wamarekani hawakutaka aendelee kuwa raisi na ndio maana aliondolewa mamlakani na sasa rais ni Baden.

Hata mungu aliye tuumba kuna mabilion ya watu duniani hawamuamini lakini wakati huo kuna mabilion ya watu wanamuami na ndio maana bado dini zipo.

Unapo ona mfumo fulani unaendelea kutawala sehemu jua bado kuna mamilion ya watu wanauunga mkono na kukubaliana nao.
Hata hii ccm siku hao mamilion ya watz wanao iunga mkono siku wakitupa mkono itafurushwa Madarakani kwa aibu na hamtaamini.
 
Back
Top Bottom