Ahsante kwa kuniwekea kumbukumbu sawa kuhusu Sheikh Kassim na BALKUTA, na nilikuwa sifahamu chanzo cha Mwaipopo ambae enzi zile alikuwa maarufu kweli kweli! Tena wala sikufahamu kwamba kumbe alikuwa ni kijana mdogo tu!!Mhenga mwenzangu umeeleza vizuri sana, naomba kuongezea kidogo sana ili nisiharibu uliyasema; Sheikh Kasim alikua member wa Balkuta na hata kile kikundi kilichokua kinasema Yesu sio mwana wa Mungu nadhani na chenyewe kilikua ni zao la hao hao Balkuta, kiliwahi kumsilimisha kijana mmoja wa Kiluteli ambaye wao walikua wanamwita "askofu Mwaipopo", huyo dogo aliishiwaga ada ya shule alikua akisoma siminari moja kule Tukuyu; anywan back to the topic; baada ya hilo tukio, vijana kadhaa waliongoza uvunjaji wa mabucha yale walikamatwa na kuwekwa lock up, kesi ikawa inaunguruma Kisutu, wakili wao alikua Musa Kwikima (nadhani kafariki mwaka hu mwezi April, habari zake zipo humu jukwaani ). Namkumbuka kijana mmoja (ki umri nadhani alikua ananizidi mimi so ni makosa kumwita kijana ) anaitwa Rashid Idd Athuman Njeja, vijana wa sheikh Kassimu aliyehitimu elimu nyingi za dini, huyu "dogo" ndiye aliyeongoza hasa uvunjaji ule wa yale mabucha. Kwasasa wengi wa hao watu ni RIP. Well, kilikua kipindi kigumu sana kwa Tanzania hasa jiji la Dar kama ulivyo sema.
Hilo la mijadala ya Yesu ni Mungu/sio Mungu niligusia kwenye post yangu lakini nika-edit kwa hofu kwamba wengine wasije wakavuruga mjadala manake JF Members bhana, kwa mihemuko ndo wenyewe!!!