Maandamano ya mabucha ya Nguruwe 1993

Mhenga mwenzangu umeeleza vizuri sana, naomba kuongezea kidogo sana ili nisiharibu uliyasema; Sheikh Kasim alikua member wa Balkuta na hata kile kikundi kilichokua kinasema Yesu sio mwana wa Mungu nadhani na chenyewe kilikua ni zao la hao hao Balkuta, kiliwahi kumsilimisha kijana mmoja wa Kiluteli ambaye wao walikua wanamwita "askofu Mwaipopo", huyo dogo aliishiwaga ada ya shule alikua akisoma siminari moja kule Tukuyu; anywan back to the topic; baada ya hilo tukio, vijana kadhaa waliongoza uvunjaji wa mabucha yale walikamatwa na kuwekwa lock up, kesi ikawa inaunguruma Kisutu, wakili wao alikua Musa Kwikima (nadhani kafariki mwaka hu mwezi April, habari zake zipo humu jukwaani ). Namkumbuka kijana mmoja (ki umri nadhani alikua ananizidi mimi so ni makosa kumwita kijana ) anaitwa Rashid Idd Athuman Njeja, vijana wa sheikh Kassimu aliyehitimu elimu nyingi za dini, huyu "dogo" ndiye aliyeongoza hasa uvunjaji ule wa yale mabucha. Kwasasa wengi wa hao watu ni RIP. Well, kilikua kipindi kigumu sana kwa Tanzania hasa jiji la Dar kama ulivyo sema.
Ahsante kwa kuniwekea kumbukumbu sawa kuhusu Sheikh Kassim na BALKUTA, na nilikuwa sifahamu chanzo cha Mwaipopo ambae enzi zile alikuwa maarufu kweli kweli! Tena wala sikufahamu kwamba kumbe alikuwa ni kijana mdogo tu!!

Hilo la mijadala ya Yesu ni Mungu/sio Mungu niligusia kwenye post yangu lakini nika-edit kwa hofu kwamba wengine wasije wakavuruga mjadala manake JF Members bhana, kwa mihemuko ndo wenyewe!!!
 
Asante sana mkuu Chige hapo juu. Mimi JF inanieleimsiha nina list ya watu wa kuita kulingana na uzi. Wakitaja magari, historia, vita, ndege, Zanzibar, mahusiano, habari za mjini, wizi na utapeli kote uko najua nani aje kuongezea na mara nyingi hakosi neno.

Sasa nikajua mambo ya VPN tena umekosa maana nimezoea kwenye nyuzi hizi unatinga bila kuitwa, tena mapema sana.
Hizi block za Internet/social media kutoka kwa JPM mimi huwa hazinisumbui lakini ukweli ni kwamba, mijadala ya aina hii huwa najaribu kuikwepa manake wengine hawakawi kuleta mihemuko ya kidini!!
 
Umeandika kwa ufupi kaka Mohamed.

Wito na hamasa ya kwenda "kuyafunga" mabucha ya nyama ya nguruwe Mbokomu pale Manzese yalitolewa na baadhi ya wahadhir baada ya mtoto wa kiislamu kutumwa nyama na mzazi wake na akajikuta anauziwa nyama ya nguruwe! Mzazi alipofatilia kutaka arudishiwe pesa akakataliwa na wauzaji na yeye akalipeleka public

Katika madai yao Waislamu walisema njia zote za kisheria walizotumia kuhakikisha kunakua na mipaka/kutengwa kati ya maduka ya kuuzia nyama za nguruwe na wanyama wengine kama ng'ombe na mbuzi, sio tu zilishindikana bali pia walikua wanaambulia kauli za kashfa na kebehi kutoka kwa watendaji wa Wilaya/Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Dar. Walikua wanadai sheria za kuzuia mabucha ya nguruwe kwenye maeneo ya mchanganyiko zipo lakini kwa makusudi na kwa kuwadharau Waislamu zilikua hazifuatwi

Baada ya sakata lile la kuvamia mabucha ya Mbokomu Pork Centre pale Manzese ili kuondoa "munkari" kwa mkono basi ndipo crackdown ya Masheikh ikafuata. Walisombwa waliohusika na wasio husika. Kama alivyosema mletaa uzi, miongoni mwao alikua Sheikh Kassim Bin Jumaa Bin Khamis, Imamu wa Msikiti wa Mtoro aliyekua safarini Arusha!

Kabda ya hapo kulikua na fukuto la hali ya kutoridhika kwa Waislamu kutokana na kuhisi walikua wanatendewa na serikali kama raia wa daraja la pili. Kuna vijana wanaharakati wa dini ya Kiislamu miongoni mwao ni marehemu Mtengwa Buruhani, marehemu Mdidi Musa, Mjeja na wengineo walikua "wamewaamsha" sana Waislamu na lile kundi lao la WARSHA ya waandishi wa Kiislamu katikati ya miaka ya 1980s kuelekea miaka ya mwanzo ya 1990s

Hii ilichukuliwa kama ni uamsho (renaissance) ya harakati za Waislamu na ni kwenye kipindi hiki (1992) Waislamu walipoamua kuichukua BAKWATA iwe mikononi mwao kwa mapinduzi ili iwe kwa faida yao kabda ya move hiyo kuzuiwa na Rais Mwinyi na baadae Augustine Mrema kuja kuendesha harambee ya pesa kutoka kwa viongozi wa kikristo ili kuiwezesha BAKWATA ifanye mkutano wake mkuu ambao walishindwa kuuitisha kwa muda mrefu kutoka na ukata pamoja na kua na rasilimali lukuki hapa nchini

Kuna watu humu wameandika kuhusu BALUKTA kwamba ilikua inamilikiwa na Sheik Kasim Bin Jumaa. Ukweli ni kwamba BALUKTA (Baraza la Kuendeleza Usomaji Kur an Tanzania) ilikua ni taasisi iliyoasisiwa na kuendeshwa na marehemu Sheikh Yahya Hussein. Taasisi hii ni miongoni mwa taasisi zilizokuja kupigwa marufuku na serikali(nadhani ilifutiwa usajili) katika kile kinachodhaniwa ni kuendelea kuipa BAKWATA nguvu ya kupumua baada ya Waislamu kuipuuzilia mbali

Kaka yangu Mohamed Said sina hadhi wala uwezo wa japo kukusogelea kwa tafiti na uandishi wako ila nime tabaruku katika kile kidoogo sana nikijuacho kutokana na kadhia ile ya mabucha ya nguruwe ambayo yalipelekea kufungwa jela kina Habibu Mazinge na wenzake japo kulikua na very strong "alibi" kwamba baadhi yao hawakuwepo kabisaaa Manzese wakati watu "wakiondoa munkari" kwa mkono
 
Ahsante kwa kunikaribisha kwenye mjadala ingawaje sina mengi sana ya kuchangia kwa sababu wakati ule bado nilikuwa kijana mdogo tu... ndo kwanza nilikuwa nimeanza Form I.

Hata hivyo, si kwamba nilikuwa kijana mdogo kama walivyo vijana wadogo wengi wasiopenda kufuatilia kinachoendelea nchini na duniani kwa ujumla, manake, moja ya mambo ambayo nilikuwa nawashangaza sana watu pale nyumbani na mtaani ilikuwa ni tabia yangu ya kupenda kusikiliza BBC, station ambayo ilionekana kama ni ya watu wazima na sio watu wa rika langu!

Lakini kwa upande mwingine, nimekulia kwenye kota za polisi... kwa maana nyingine, ingawaje sikuwa mkubwa sana lakini sikutoka kapa moja kwa moja kuhusu kilichokuwa kinaendelea kwa sababu kwa upande mmoja nilikuwa mtoto wa BBC, na kwa upande mwingine, nilikuwa nashuhudia kwa macho yangu harakati za polisi baada ya lile tukio!!!

It's a mess!!!

Sifahamu ni nini hasa kiliwapelekea baadhi ya Waislamu kuvamia mabucha ya nguruwe ingawaje utetezi ulikuwa kwamba, wao kama wao hawakuwa wakipinga uwepo wa hizo bucha bali walikuwa wakipinga uwepo wa bucha hizo kwenye maeneo yenye mchanganyiko wa watu, huku mengi yake yakiwa kwenye maeneo yanayokaliwa na Waislamu wengi hapo Magomeni na Manzese, huku wakidai hiyo ilikuwa ni kinyume hata na sheria zenyewe (bila shaka za mipango mji), na wakazi wa huko walipojaribu kulalamika, serikali iliwapuuza na ndipo watu wakachukua sheria mkononi!

Nakumbuka siku anayoisema Mohammed Said hapo juu, nilikuwa naenda pale Central alipokuwa Bi Mkubwa hata hivyo kufika Posta ya Zamani nililazimika kugeuza manake Posta yote ilikuwa imetanda magari ya polisi waliobeba silaha za kivita!

Uzoefu wangu wa kuishi Kota za Polisi haukusaidia kunipa ujasiri wa kutowaogopa polisi wale manake ilikuwa ni kama Uwanja wa Vita!!

Huyo Sheikh Kassim Bin Juma sie wengine ndo tulianza kumfahamu kupitia tukio hili! Na kama kumbukumbu zangu zipo sawa, movement mzima ilikuwa inaendeshwa na BALKUTA iliyokuwa chini ya Sheikh Yahya Hussein.

Sina uhakika wa uhusiano wa Sheikh Kassim na BALKUTA lakini nisicho na shaka nacho ni ushawishi wake mkubwa aliokuwa nao pale Msikitini kwa Mtoro!

Hii BALKUTA ilikuwa mwiba mkali kwa serikali... cjui ilifia wapi lakini nadhani ilipigwa ban na serikali, manake kwa jinsi ambavyo ilikuwa na ufuasi mkubwa hususani wa vijana, I doubt kama ingeweza kufa yenyewe!

Bila shaka Mohamed Said atakuwa analifahamu vizuri hili suala na kuweka kumbukumbu isiyo shaka sawa! Na kama kweli ilifutwa na serikali basi sina shaka moja ya taasisi ambazo zilifanya sherehe kutokana na kufutwa huko basi ni BAKWATA ambayo wakati ule ilikuwa chini ya Sheikh Hemed bin Juma bin Hemed!!

BAKWATA ilikuwa inanyimwa sana usingizi na BALKUTA!!

Hizi movements za Sheikh Ponda si lolote si chochote mbele ya BALKUTA manake hata mapinduzi kwenye misikiti ili kuondoa ma-Imam wa BAKWATA, kama sikosei movement za aina hiyo ziliasisiwa na BALKUTA, na kufutwa kwa BALKUTA ndiko kukaja kuibua akina Sheikh Ponda!!

Anyway, kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Tanzania, hususani Dar es salaam!!!
Chige,
Kuna pp niliwasilisha kwenye mkutano Chuo Kikuu Cha Kenyatta Nairobi mwaka wa 2007 bahati mbaya sana ni ya Kiingereza ingia uisome:

 
Kuna mambo yanapotokea tunategemea viongozi wetu wayasolve bila kuwakwaza raia kwa kufuata misingi ya sheria.

Kwa mfano hapo ilikuwa very simple, huyo aliyewauzia familia nyama ya kitimoto na amejulishwa kuwa amekosea then lilikuwa swala la kumalizwa serikali ya mtaa kwa kusuluhisha na kufidia gharama na wazazi kuwa makini wanapowatuma watoto.

Lakini pia, ilikuwa ni swala la kuhoji kama hayo maduka yana exists mitaa hiyo it means biashara ipo. Haiyumkiniki mfanyabiashara afungue duka manzese halafu wateja watoke kigogo, big no, wateja wapo mitaa hiyo.

Kitendo cha hicho kikundi kuvamia maduka haya na kuamua kuyavunja ni uvunjaji wa sheria za nchi na ni ukorofi dhidi ya raia. Elimu ni muhimu sana kutolewa na kuelimisha raia kutambua mipaka na kujua tofauti ya imani, dini na sheria za nchi zinazolinda maisha yetu ya kila siku.

Tukiruhusu kila mtu afanye vile akili, matakwa yake anapenda au kufuata mlengo fulani na kulazimisha wengine wafuate kwasababu tu anahisi yeye ni sahihi then tunafanya kosa kubwa sana kuwaza hivyo.....

Hili ni taifa, linamiiko, sheria, kanuni na taratibu ambazo viongozi, raia, na makundi ya itikadi na milengo tofauti wanapaswa kufuata. Kama unaona hii inchi haielekei kule unataka then why uingie gharama ya kutaka kutumia nguvu kubadili watu wote wafananie na wewe, kwann usihamie pale panapofanania na mitazamo yako ambayo uaniona halali.

Kukosa hekima, busara na uelewa ni tatizo kubwa sana miongoni mwa raia.
 
Kuna mambo yanapotokea tunategemea viongozi wetu wayasolve bila kuwakwaza raia kwa kufuata misingi ya sheria.

Kwa mfano hapo ilikuwa very simple, huyo aliyewauzia familia nyama ya kitimoto na amejulishwa kuwa amekosea then lilikuwa swala la kumalizwa serikali ya mtaa kwa kusuluhisha na kufidia gharama na wazazi kuwa makini wanapowatuma watoto.

Lakini pia, ilikuwa ni swala la kuhoji kama hayo maduka yana exists mitaa hiyo it means biashara ipo. Haiyumkiniki mfanyabiashara afungue duka manzese halafu wateja watoke kigogo, big no, wateja wapo mitaa hiyo.

Kitendo cha hicho kikundi kuvamia maduka haya na kuamua kuyavunja ni uvunjaji wa sheria za nchi na ni ukorofi dhidi ya raia. Elimu ni muhimu sana kutolewa na kuelimisha raia kutambua mipaka na kujua tofauti ya imani, dini na sheria za nchi zinazolinda maisha yetu ya kila siku.

Tukiruhusu kila mtu afanye vile akili, matakwa yake anapenda au kufuata mlengo fulani na kulazimisha wengine wafuate kwasababu tu anahisi yeye ni sahihi then tunafanya kosa kubwa sana kuwaza hivyo.....

Hili ni taifa, linamiiko, sheria, kanuni na taratibu ambazo viongozi, raia, na makundi ya itikadi na milengo tofauti wanapaswa kufuata. Kama unaona hii inchi haielekei kule unataka then why uingie gharama ya kutaka kutumia nguvu kubadili watu wote wafananie na wewe, kwann usihamie pale panapofanania na mitazamo yako ambayo uaniona halali.

Kukosa hekima, busara na uelewa ni tatizo kubwa sana miongoni mwa raia.
Samcezer, nakubaliana nawe kwamba masuala mengine yanaweza kumalizwa bila ya kuleta vurugu wala bughudha kwa watu

Lakini kuna kiburi na dharau cha baadhi ya watendaji wa serikali. Hii husababisha migongano isiyo ya lazima kwa wananchi. Pamoja na kwamba mwenye bucha aliona pale ndio kwenye biashara lakini sheria ndogo(by laws) za Manispaa zinakataza hilo

Hii inanikumbusha kwa mfano wakati wa upangaji wa miji ya Kibada, Kisota(Kigamboni) na Mbweni ambapo palipimwa viwanja 20,000 vya makazi na shughuli mbali mbali kulikua na maeneo yaliyopangwa kama sehemu za ibada bila ku specify eneo lipi ni kwa ajili ya ibada ya watu wa imani ipi.

Matokeo yake maeneo karibia yote yanayoitwa ya ibada yalichukuliwa na watu wenye imani moja maana inasemekana wao ndio walianza kupata taarifa ya kugaiwa viwanja kwa bei ndogo ya Serikali kabda ya taarifa rasmi kutolewa kwa umma! Katika hali ya kawaida watendaji wa mradi walitakiwa waainishe kwamba eneo fulani ni kwa ajili ya nyumba za ibada za imani fulani kama wanavyofanya kwenye upangaji wa makaburi ili kuweka uwiano mzuri na wa haki kwa jamii.

Sura iliyopo sasa ni kwamba katika maeneo hayo yaliyopimwa baada ya wakazi wake kunyang'anywa ardhi zao kwa fidia ndogo sana(yalichukuliwa kabda ya sheria mpya ya ardhi) kume tamalaki nyumba za ibada za imani moja tu na ukiona kuna nyumba ya ibada ya imani tofauti basi ujue ni mtu kaamua kujitolea kiwanja/viwanja vyake kwa ajili hiyo!

Ni vyema watendaji wa serikali katika ngazi zote wafanye kazi kwa uadilifu na kutenda haki kwa watu wote ili kuendeleza utangamano wa kitaifa
 
Ndahani,
Umezungumzia mgawanyiko ndiyo nasema ume- "assume."

Fanya utafiti ili ujue ukweli.

Mzee unalazimisha sana Baadhi ya mambo yawe kama unavyotaka wewe. Ukiongea na wapambe wako kadhaa, Haina maana tafiti wako una mashiko. Siku zote unasukumwa na agenda sadikika.

Dini hizi zinatupa changamoto sana, ila kama mimi na wewe tulivyokuja na tutakwenda, zenyewe zitaendelea kubaki kama zilivyo. Hakuna atakayezifuta.

Ukiwa unaongelea Tanzania, hebu acha dhana kwamba dini yako tu ndio inayoonewa. Nani ameionea? Eti Nyerere! Unajua Nyerere aliondoka madarakani lini.

Aliyemfuata ikawaje? Yeye hakufanya dhuluma za kidini?
Tanzania ni zaidi ya Imani ya dini moja. Nina hakika ipo siku utagundua unayofanya hayatakaa kutokea
 
Umeandika kwa ufupi kaka Mohamed.

Wito na hamasa ya kwenda "kuyafunga" mabucha ya nyama ya nguruwe Mbokomu pale Manzese yalitolewa na baadhi ya wahadhir baada ya mtoto wa kiislamu kutumwa nyama na mzazi wake na akajikuta anauziwa nyama ya nguruwe! Mzazi alipofatilia kutaka arudishiwe pesa akakataliwa na wauzaji na yeye akalipeleka public

Katika madai yao Waislamu walisema njia zote za kisheria walizotumia kuhakikisha kunakua na mipaka/kutengwa kati ya maduka ya kuuzia nyama za nguruwe na wanyama wengine kama ng'ombe na mbuzi, sio tu zilishindikana bali pia walikua wanaambulia kauli za kashfa na kebehi kutoka kwa watendaji wa Wilaya/Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Dar. Walikua wanadai sheria za kuzuia mabucha ya nguruwe kwenye maeneo ya mchanganyiko zipo lakini kwa makusudi na kwa kuwadharau Waislamu zilikua hazifuatwi

Baada ya sakata lile la kuvamia mabucha ya Mbokomu Pork Centre pale Manzese ili kuondoa "munkari" kwa mkono basi ndipo crackdown ya Masheikh ikafuata. Walisombwa waliohusika na wasio husika. Kama alivyosema mletaa uzi, miongoni mwao alikua Sheikh Kassim Bin Jumaa Bin Khamis, Imamu wa Msikiti wa Mtoro aliyekua safarini Arusha!

Kabda ya hapo kulikua na fukuto la hali ya kutoridhika kwa Waislamu kutokana na kuhisi walikua wanatendewa na serikali kama raia wa daraja la pili. Kuna vijana wanaharakati wa dini ya Kiislamu miongoni mwao ni marehemu Mtengwa Buruhani, marehemu Mdidi Musa, Mjeja na wengineo walikua "wamewaamsha" sana Waislamu na lile kundi lao la WARSHA ya waandishi wa Kiislamu katikati ya miaka ya 1980s kuelekea miaka ya mwanzo ya 1990s

Hii ilichukuliwa kama ni uamsho (renaissance) ya harakati za Waislamu na ni kwenye kipindi hiki (1992) Waislamu walipoamua kuichukua BAKWATA iwe mikononi mwao kwa mapinduzi ili iwe kwa faida yao kabda ya move hiyo kuzuiwa na Rais Mwinyi na baadae Augustine Mrema kuja kuendesha harambee ya pesa kutoka kwa viongozi wa kikristo ili kuiwezesha BAKWATA ifanye mkutano wake mkuu ambao walishindwa kuuitisha kwa muda mrefu kutoka na ukata pamoja na kua na rasilimali lukuki hapa nchini

Kuna watu humu wameandika kuhusu BALUKTA kwamba ilikua inamilikiwa na Sheik Kasim Bin Jumaa. Ukweli ni kwamba BALUKTA (Baraza la Kuendeleza Usomaji Kur an Tanzania) ilikua ni taasisi iliyoasisiwa na kuendeshwa na marehemu Sheikh Yahya Hussein. Taasisi hii ni miongoni mwa taasisi zilizokuja kupigwa marufuku na serikali(nadhani ilifutiwa usajili) katika kile kinachodhaniwa ni kuendelea kuipa BAKWATA nguvu ya kupumua baada ya Waislamu kuipuuzilia mbali

Kaka yangu Mohamed Said sina hadhi wala uwezo wa japo kukusogelea kwa tafiti na uandishi wako ila nime tabaruku katika kile kidoogo sana nikijuacho kutokana na kadhia ile ya mabucha ya nguruwe ambayo yalipelekea kufungwa jela kina Habibu Mazinge na wenzake japo kulikua na very strong "alibi" kwamba baadhi yao hawakuwepo kabisaaa Manzese wakati watu "wakiondoa munkari" kwa mkono
Sesten,
Hiyo hapo chini ni pp nilitoa Kenyatta University kuhusu Sheikh Kassim Juma na Mabucha ya Nguruwe:

http://mohamedsaidsalum.blogsp...h?q=sheikh+kassim+juma&m=1
 
Asante sana mkuu Chige hapo juu. Mimi JF inanieleimsiha nina list ya watu wa kuita kulingana na uzi. Wakitaja magari, historia, vita, ndege, Zanzibar, mahusiano, habari za mjini, wizi na utapeli kote uko najua nani aje kuongezea na mara nyingi hakosi neno.

Sasa nikajua mambo ya VPN tena umekosa maana nimezoea kwenye nyuzi hizi unatinga bila kuitwa, tena mapema sana.
Mimi utaniita wapijoking
 
Mwaka wa 1993 ulikuwa mwaka mzuri sana kwangu kwani katika miezi 12 nilikuwa nimesafiri mara tatu tena ukichukulia kuwa mwaka wa 1991/92 nilikuwa Uingereza.

Nilikwenda Harare na ulikuwa mwezi wa Ramadhani.

Nilikaa Harare kwa majuma matatu na nikafika hadi Bulawayo.

Nikaenda Lusaka Zambia.

Niliporudi nikaenda Ufaransa nikawa Le Havre na Paris na safari ya kurudi nikapita London nikasali Eid Kubwa Regent Park Mosque hapo London kisha nikaenda Cardiff nikarudi Dar es Salaam.

Wakati huo Bunge liko Karimjee linaunguruma na sakata la Rais Mwinyi kuruhusu Zanzibar kuingia Organisation of Islamic Conference (OIC) na aliyehusika alikuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Ahmed Hassan Diria.

Barua za Kiuchungaji zinashambulia serikali ya Rais Mwinyi pamoja na magazeti yote hata yale ya Chama na Serikali.

Rais Mwinyi akajikuta hana wa kumtetea ila Sheikh Kassim bin Juma Imam Mkuu wa Msikiti wa Mtoro Mwinyi Mangara na ndani ya serikali akifarajiwa na Prof. Kighoma Ali Malima.

Hotuba za Ijumaa za Sheikh Kassim kwenye membar ya Mtoro zilitikisa nyoyo za Waislam na serikali nzima.

Siku ya Ijumaa msikiti unajaa hadi nje kufikia Mtaa wa Livingstone.

Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamu Waziri Mkuu alikuwa Augustine Mrema.

Kulikuwa na makaratasi ya "uchochezi," yakimwagwa misikiti yote ya Dar es Salaam yaliyokuwa yakiandikwa na "waandishi wasiojulikana," yakijibu Barua za Kiuchungaji.

Wachina wana msemo, "May you live in interesting times."

Hizi nyakati zilikuwa za kipekee kabisa hazikupata kutokea hata wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii safari yangu ya Ufaransa ilikuwa imenifanya nipitwe na mengi ya mjini.

Niliporudi nikaenda Zanzibar kushughulikia mambo fulani kuhusu OIC mimi na mwenzangu mmoja.

Tulipokuwa ndani ya chombo tunarejea ndiyo tukapata taarifa kuwa Waislam wamevunja mabucha ya nguruwe baada ya sala ya Ijumaa.

Rais Mwinyi kwa hofu akasema wale waliovunja mabucha ya nguruwe "nguvu za dola ziwaangukie."

Hiki ndicho kilichokuwa kinasubiriwa.

Usiku mmoja hadi kufika asubuhi masheikh na wahadhiri wa Kiislam wakakamatwa.

Waislam wakahamaki taarifa ikatoka kuwa wakutane Msikiti wa Mtoro kujadili kuwatoa masheikh walipokuwa wamewekwa rumande Central Police.

Katika kikao kile cha Mtoro siku ya Jumapili asubuhi msikiti ulijaa vijana hakuna sheikh hata mmoja aliyehudhuria.

Allah amenijaalia kuona kwa macho yangu matukio makubwa katika historia ya Waislam wa Tanganyika.

Mjadala ulikuwa mkali vijana ndani ya msikiti wakidai kuwa uamuzi wowote utakaofikiwa siku ile utoke kwenye Qur'an na Sunna hapatakiwi rai ya mtu binafsi.

Kikao hiki bila kuuma maneno kilikuwa kikao cha vita.

Sijapata kuona hamaki kwa Waislam kama niliyoshuhudia siku ile.

Ndipo Sheikh Waziri Ramadhani akasimama na kusema, "Ndugu zangu Allah leo ametuletea mtihani kutuangalia kama tunaweza kusimama kuipigania dini yake.

Kama dhulma tumeshafanyiwa sana ifike mahali tuseme basi kwa kukamatwa viongozi wa Waislam ni dharau ya juu kabisa dhidi yetu.

Kila unachokiona duniani kinamtumikia Allah basi ndugu zangu tutokeni twendeni Central Police tukawatoe masheikh zetu."

Hapo ndipo yalipotokea maandamano ya kwanza ya Waislam na yalipofika Mnazi Mmoja katika hali ya jua kali ghafla wingu likatanda na mvua ikaanza kunyesha.

Maandamano yalipofika Clock Tower askari wa FFU walikuwa wanawasubiri waandamanaji hapo mapambano yakaanza.

Mabomu mengi yaliyopigwa pale moshi wake ulipeperushwa na ule upepo wa mvua.

Milango ya Central Police ambayo daima haifungwi ikafungwa kwa kuhofu ule umma ungeweza kuingia hadi ndani ya selo za polisi.

Waislam wengi walikamatwa na kufunguliwa mashtaka.

Nahitimisha kwa kusema kuwa wakati haya yanatendeka Sheikh Kassim alikuwa Arusha akielekea Nairobi kwenye matibabu.

Hii ilikuwa "turning point," katika maisha yake kwani yeye alikuwa karibu sana na serikali na iliwashangaza wengi kumuona ameigeukia.

Kama si yeye kufanya vile na kusimamia haki Sheikh Kassim Jums angepita dunia hii kama walivyopita masheikh wengi wengine kabla yake.

Ndugu zanguni msimuone ndugu yenu kakataa kuitambua haki na akawa upande wa dhulma mkamkatia tamaa.

Muombeeni dua.

Kile kibri chake cha yeye kuwa upande wa wenye mamlaka na nguvu kisituvunje moyo.

Picha ambayo hainitoki kichwani mwangu ni picha ya Sheikh Kassim Juma mwaka wa 1979 anamkaribisha Nyerere ndani ya Msikiti wa Mtoro kwenye khitma ya aliyekuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.
Sijaokota chochote hapa zaidi ya udini na uharo.
 
Kuna mambo yanapotokea tunategemea viongozi wetu wayasolve bila kuwakwaza raia kwa kufuata misingi ya sheria.

Kwa mfano hapo ilikuwa very simple, huyo aliyewauzia familia nyama ya kitimoto na amejulishwa kuwa amekosea then lilikuwa swala la kumalizwa serikali ya mtaa kwa kusuluhisha na kufidia gharama na wazazi kuwa makini wanapowatuma watoto.

Lakini pia, ilikuwa ni swala la kuhoji kama hayo maduka yana exists mitaa hiyo it means biashara ipo. Haiyumkiniki mfanyabiashara afungue duka manzese halafu wateja watoke kigogo, big no, wateja wapo mitaa hiyo.

Kitendo cha hicho kikundi kuvamia maduka haya na kuamua kuyavunja ni uvunjaji wa sheria za nchi na ni ukorofi dhidi ya raia. Elimu ni muhimu sana kutolewa na kuelimisha raia kutambua mipaka na kujua tofauti ya imani, dini na sheria za nchi zinazolinda maisha yetu ya kila siku.

Tukiruhusu kila mtu afanye vile akili, matakwa yake anapenda au kufuata mlengo fulani na kulazimisha wengine wafuate kwasababu tu anahisi yeye ni sahihi then tunafanya kosa kubwa sana kuwaza hivyo.....

Hili ni taifa, linamiiko, sheria, kanuni na taratibu ambazo viongozi, raia, na makundi ya itikadi na milengo tofauti wanapaswa kufuata. Kama unaona hii inchi haielekei kule unataka then why uingie gharama ya kutaka kutumia nguvu kubadili watu wote wafananie na wewe, kwann usihamie pale panapofanania na mitazamo yako ambayo uaniona halali.

Kukosa hekima, busara na uelewa ni tatizo kubwa sana miongoni mwa raia.
Suala la kuchanganya nyama kwa mteja leo ndio nalisoma humu baada ya mdau mmoja ku share nasi; napata shida sana kukubaliana nae au kumkatalia cause wakati ile issue inatokea, hili halikua moja ya malalamiko yaliokwepo. Shida moja ya Historia you can cook the way you like. Baadhi ya hao vijana aliowataja ambao walishiriki uvunjaji wa hayo mabucha walikua wanaishi TEMEKE huko, sasa issue imetokea Manzese, huyu wa Temeke inamuhusu nini? Ambacho nakubaliana na huyu jamaa aliyezungumza kuhusu "mchanganyiko wa hiyo nyama" na hiki; je was it busara kua na maduka ya nyama ya kiti moto pamoja na nyama za wanyama wengine sehemu moja? Hili jambo ni uzembe kabisa wa serikali, uzembe kama uliosababisha kifo cha Akwirine kwa uchaguzi wa ubunge Kinondoni, the same. Sema tu serikali huwezi kuishtaki but mauaji mengine yanatengenezwa na serikali yenyewe.
 
... kati ya maamuzi muhimu ya kitaifa yaliyowahi kuamuliwa kwa hekima ya hali ya juu ni hili la Rais Mwinyi kuamua suala la uvunjaji wa bucha za nguruwe Dar-es-Salaam; ulikuwa uamuzi wa level ya "Hekima ya Sulemani"! Kwamba "anayetaka kula (chochote) ruksa, na asiyetaka ruksa"; haya yalikuwa maamuzi neutral sana na ya hekima yasiyoegemea upande wowote labda kwa wale ambao always walijiona kuonewa pengine wangependa kuona kauli ya Rais ikiwa-support directly lakini ilikuwa kinyume na matarajio yao!

Pili, majaabu yaliyotokana na uhuni ule ni kwamba kwa tukio lile nguruwe alipata daraja ya juu sana sio tu Dar bali nchini kote; ndio ikawa mwanzo wa hafla za "kiti moto" mtaa kwa mtaa nchini kote na hata maelfu kwa maelfu ya wale wengine wanashiriki hafla hizo nchini kote! Vijana wengi wakajiajiri, wakulima wakapata kipato, na watanzania kwa ujumla wakapata lishe.

Sina hakika kama wale jamaa walifanya tathmini kuona kama uamuzi wao ule ulikuwa na +ve au -ev effects! Labda Mzee Mohamed Said atakuwa na matokeo ya utafiti atujuze.
 
Back
Top Bottom