mende 2014
JF-Expert Member
- Apr 13, 2014
- 763
- 131
Wanachama wa chama cha CHADEMA wapigwa mabomu baada ya kufanya maandamano katika mtaa wa @Nyasura center hapa mjini Bunda mkoani Mara. Watu kadhaa wamekamatwa na kupelekwa polisi.
Leo kuanzia saa mbili asubuhi Makamanda na wanachama wa CHADEMA na wananchi wasio na vyama vya siasa walikusanyika katika mtaa wa Nyasura kwa ajili ya kuanza maandamo ya kupinga Bunge la Katiba kuendelea na vikao vyake. Wananchi walikuwa wengi kama 1200 na ilipofika saa tano kamili maandano yalianza kuelekea stendi ya zamani ambapo ilitalajiwa ufanyike mkutano mkubwa, polisi walikuja na kuanza kulusha mabomu ya machozi na kwa kuwa wananchi walikuwa wamejizatiti, mabomu ya machozi ni kama hayakufua dafu ndipo risasi za moto zilianza kutumika. Mpaka sasa wameisha kamatwa viongozi sita wa CHADEMA
Wananchi bado wanaendelea kujikusanya na kutiana hamasa! naona makundi makubwa makubwa ya watu sasa yanatoka kwenye nyumba zao na wameanza kujikusanya wakiwa na lengo la kuendelea na maandamo!
ntaendelea kukupa habari, maana macho yanawasha!!