Maandamano ya CCM Singida Thibitisho la Kifo Chake

Maandamano ya CCM Singida Thibitisho la Kifo Chake

Vipi safari hii hawakuwapata wanafunzi wa shule za msingi kujazia idadi? ...au walikua likizo??

fuso ngapi zilileta watu...? je pilau ilikuwepo....?
 
pole sana kwa taarifa yako ccm itatawala miaka mingine mia moja ijayo sababu kubwa ni kwamba upinzani umekosa viongozi makini.mfano mbowe anahutubia wananchi huku anajisifia ya kuwa ni lazima watasusia baadhi ya maamuzi ya bunge kwa kutoka nje kama si utoto ni nino

hiyo ndiyo sababu ya kuongoza miaka 100? Kama huo ndiyo umakini basi umakin siutaki.
 
pole sana kwa taarifa yako ccm itatawala miaka mingine mia moja ijayo sababu kubwa ni kwamba upinzani umekosa viongozi makini.mfano mbowe anahutubia wananchi huku anajisifia ya kuwa ni lazima watasusia baadhi ya maamuzi ya bunge kwa kutoka nje kama si utoto ni nino
CCM ipo siku itaondoka, hivi sasa imebaki na njia moja kuchakachua ikizibwa hiyo na katiba mpya safari itakuwa imefika maana saizi haina mvuto kwa wananchi licha ya kujivua gamba.
 
189 wa kuchakachua? Ngulume alifanya kazi nzuri sana akiwa na mgumia kwa kuonesha tv za mauaji ya rwanda eti wanyaturu wakichagua upinzani watachinjana kama ilivyotokea kati ya wanyaturu na wabarbaig. Shukrani ziende kwa hayati askofu Bernado mabulla aliyemwita mgumuia na kuhubiri kanisani kuwa ilikuwa serikali ipitishe sheria ya kuruhusu vyama vingi huku ikijua watu watauana, na akaelekeza video hizo zzisionyeshwe. Sishangai wale mabibi na mababu wa singida kufanya hivyo ni kazi uliyofanyika kipindi cha uasisi wa vyama vya upinzani.
 
Mkuu wangu Sijatunga hizi Habari nimeziona Mwenyewe kwenye Taarifa ya Habari, nimeona CCM wakiandama lakini wengi wa Waaandamanaji ni Vikongwe

Hata mimi nmeona.baadhi yao walikuwa miguu peku huku wamevaa tisheti za kijani na njano.nguo za kupauka walizo vaa zimeandikwa maisha bora kwa kila mtz.
 
Dua la kuku! Sisiemu wanaongoza kwa kupata wabunge wengi wa majimbo chadema mna wabunge wa majimbo 23 wao 188 sasa dalili za kuingusha ni maandamano mnayofanya? CCM sio ya kuanguka mapema hivyo!

Bado wabunge wa CHADEMA ni wengi kwasababu mbunge 1 wa CHADEMA ni sawa na wabunge 20 CCM.Ili wawe sawa ilibidi wabunge wa CHADEMA wawe 10!! CCM mnapeleka akina Jah People yule mbunge wa Njombe kaskazini au akina Vicky Kamatta mnategemea nini?
 
Yani wanaCDM mna moyo kweli, kama jamaa alivyosema kuwa wabunge wenu ni 23 na wa ccm ni 188 sasa kweli mnategemea kuwa nyie ndio mnasauti hapa Tanzania? Hizi ni kelele za humu JF tukitoka nje unakuta mambo tofauti. Basi kwa habari yenu 2015 hata hao 23 hamtawapata.
 
HUKU NI KuSHUSHA kabisa heshima ya forum hii, CCM wanawapokea Sekretarite yao kesho sasa hayo maandamano ya wapi? Khaaaaaaa inatia kichefuchefu unatufurahisha hapa kwa uongo na uzushi. Kwaheri CCM, RIP CCM
Hilo si hoja tatizo lenu hamuangalii taarifa za habari, jana ungeangalia ITV CCM waliandamana kumuunga mkono mwenyekiti wao kwa suala la kuvua gamba, huko Kahama; sasa wewe unabisha nini; kwataarifa yako ni kwamba asilimia 99 walikuwa vikongwe na wazee; waongeaji walikuwa wanashindwa hata kuongea kilichowafanya waandamane; hii inaonenyeha wananchi hasa wazee wasivyoelewa dhana ya kujivua gamba; LAKINI CCM TANGULIA KABURINI; BURIANI; KANSA ANAYOISEMA MAHANGA NDO INAUA CHAMA CHENU.
 
waacheni wanaoamini ccm bado ngangari waamini hivyo. na ni bora wakiendelea kuamini hivyo, kuliko wakiuona huo ukweli.
 
Narudia tena CCM wameongoza Maandamano ya Wamama na Vikongwe na Mmoja wa waliohutubia ni James Lembeli Taarifa ya Habari ITV Saa Mbili Usiku

hata mimi niliona hyo mzaz, nikastaajabu kwa mahudhurio hafifu tena ya wamama wachache, wabibi na wababu ndo walikuwa wengi! wamevaa fulana chakavuuu, afu wanacheza kama wana upungufu wa sukari mwilini. nikajua sasa chama cha magamba kushnei
 
Narudia tena CCM wameongoza Maandamano ya Wamama na Vikongwe na Mmoja wa waliohutubia ni James Lembeli Taarifa ya Habari ITV Saa Mbili Usiku

hata hii asubuhi taarifa hiyo nimeiona.
 
Aisee CCM wamechoka,wanatia huruma sana,hakika hiki ni chama cha mkoloni mweusi,mauti imewakuta,wangeona maandano ya CHADEMA huko Rukwa jana wasingeongea,maandano yalikuwa yana watu wengi sijawahi kuona mpaka mwenyekiti mstaafu na wawilaya wa CCM walirudisha kadi za chama cha CCM na kujiunga na CHADEMA.
 
pole sana kwa taarifa yako ccm itatawala miaka mingine mia moja ijayo sababu kubwa ni kwamba upinzani umekosa viongozi makini.mfano mbowe anahutubia wananchi huku anajisifia ya kuwa ni lazima watasusia baadhi ya maamuzi ya bunge kwa kutoka nje kama si utoto ni nino

Tunajua watu kama ninyi bado mpo ambao wala hamuelewi la mbele wala la nyuma na hata kinachoendelea katika Tanzania hii hukijui. Hilo dua lako la ccm kutawala tena miaka mia moja inaonyesha kichwani kwako kunahitajika ukarabati wa kuelimishwa. Ni sawa umelala na mtu kitandani kumbe ameshakufa muda mrefu lakini wewe ndiyo unamfunika baridi lisimpige. Bado kuna watu wa sampuli yako wengi katika Tanzania hii ambao mnaona ccm ndiyo baba yenu na mama yenu na bila hiyo ni sawa na kufa. Amka kutoka usingizi huo mzito.
 
ni kweli yaliyoko kwenye fikra zao hao wana sgd na sehemu zingine za tanzania ndio yapo kwenye maamuzi yao pia? kama watakuwa na fikra pevu juu ya uozo wa ccm lakini mwisho wa siku wakawa na maamuzi ya kuichagua tena ccm haina maana kwao kususia maandamano, kama hawayaishi wanayoyafikiri wataendelea kutawaliwa na ccm hata milele,
 
Tunajua watu kama ninyi bado mpo ambao wala hamuelewi la mbele wala la nyuma na hata kinachoendelea katika Tanzania hii hukijui. Hilo dua lako la ccm kutawala tena miaka mia moja inaonyesha kichwani kwako kunahitajika ukarabati wa kuelimishwa. Ni sawa umelala na mtu kitandani kumbe ameshakufa muda mrefu lakini wewe ndiyo unamfunika baridi lisimpige. Bado kuna watu wa sampuli yako wengi katika Tanzania hii ambao mnaona ccm ndiyo baba yenu na mama yenu na bila hiyo ni sawa na kufa. Amka kutoka usingizi huo mzito.
mkuu hao ni jamaa wako nje ya nchi hayajui kinachoendelea nchini! NDO TATIZO HILO!
 
Back
Top Bottom