Bado Niponipo
JF-Expert Member
- Aug 15, 2008
- 680
- 168
Kwa kuwa CDM wanatumia haki yao ya kikatiba kuzunguka nchi nzima kutangaza sera zao na msingi wao juu ya hali mbaya ya umeme, ugumu wa maisha na kadhalika haina budi kwa CCCM na wao kuzunguka nchi nzima kutumia majukwaa na maandamano kujibu hoja na tuhuma za CDM na kuwaeleza wananchi wanampango gani katika kutatua kero zao, na kwa kuanzia waende kanda ya ziwa kufuta nyayo za CDM na wafanye hivyo hivyo kwa mikoa mingine ambayo CDM watafanya maandamano na mikutano ya hadhara.
Lakini angalizo langu ni jee, nani katika CCCM mwenye mvuto na anayekubalika na watanzania ambaye atazunguka Tanzania nzima kujibu tuhuma na hoja za CDM, je CCCM watapata mahudhurio makubwa kama wanayopata CDM na je mwitikio wa maandamano na mikutano ya hadhara ukiwa mbaya hii itatufundisha nini?
Je mwenyekiti na katibu wa CCCM wako tayari kuchukua jukumu hili na kuzunguka Tanzania nzima kujibu hoja za CDM kwa wananchi.
Nawakilisha.
Lakini angalizo langu ni jee, nani katika CCCM mwenye mvuto na anayekubalika na watanzania ambaye atazunguka Tanzania nzima kujibu tuhuma na hoja za CDM, je CCCM watapata mahudhurio makubwa kama wanayopata CDM na je mwitikio wa maandamano na mikutano ya hadhara ukiwa mbaya hii itatufundisha nini?
Je mwenyekiti na katibu wa CCCM wako tayari kuchukua jukumu hili na kuzunguka Tanzania nzima kujibu hoja za CDM kwa wananchi.
Nawakilisha.