Maandamano ya amani+viongozi wa dini+diaspora

Maandamano ya amani+viongozi wa dini+diaspora

KAYGREKO

Member
Joined
Jan 18, 2013
Posts
38
Reaction score
33
MAANDAMANO YA AMANI + VIONGOZI WA DINI + DIASPORA

Nianze na ukweli ambao wengi tutakubaliana. Afrika hatuna mazowea ya kuwa na maandamano ya amani. Na hata zile nchi zenye uzoefu wa maandamano ya amani, huanza kwa amani na mwishowe huzuka fujo. Kwa nchi yetu ya TZ, na hasa baada ya yaliyotokea 29/10, kuitisha maandamano ya amani NI KUDANGANYANA.

Viongozi wa dini sehemu yoyote duniani huwa wana nguvu na uwezo wa kiajabu wa kusikilizwa na kufuatwa na wafuasi wao. Lakini wanapojisahau na wakawa wanaweka mbele maslahi yao ya kibinadamu kwa kuitumia dini, hapo hata Mungu huwapa uelewa wafuasi wao wa kutowafuata, japo wataendelea kuhudhuria misikitini na makanisani.

Nyumbani TZ kuna wanaoelewa vibaya kuwa sisi tunaoishi huku ughaibuni (diaspora), wote tunashabikia yatokee machafuko. Wanasahau kuwa SIYO WOTE TULIOPO UGHAIBUNI TUNA MSIMAMO HUO. Huku tupo wengi hatuzingatii vyama wala dini. Tuna ndugu na jamaa zetu TZ, na hatufurahishwi kuona ndugu zetu wanadhurika.

 
  • Thanks
Reactions: Tui
Point yako hasa ni nini? What did you wanna accomplish with this poor written and illogical verbatim?

Tumeshajua kuwa we ni dayaspora? So what?
 
Back
Top Bottom