GrEaTthinkers,
Think kiasi gani tumepoteza kama taifa,
Kwa nini jasho letu linatumika vibaya hivi!
Nasema hawa si wa kuchekea wanaiumiza Nchi,
- TICTS
- RADAR
- NDEGE YA RAIS
- SAFARI ZA NJE YA NCHI-UTADHANI YEYE NI WAZIRI WA MAMBO YA NJE
- TWIN TOWERS BOT
- MIKATABA ISIYO NA TIJA KWA NCHI(Madini)
- KAGODA(EPA)
- MEREMETA
- RICHMOND/DOWANS
- WAKUU WA MIKOA na WILAYA(Hao ni Watumishi wa CCM)
- IPTL
- KIWIRA COAL MINES
- NETGROUP SOLUTIONS
- MISAMAHA YA KODI(Nchi inakosa mapato)
- ALEX STEWART
- BEI YA BIDHAA ie. UMEME (watanzania ndiyo wanaofidia misamaha ya kodi)
- RITES
- ALLIANCE AIR
- KUJENGA BARABARA KUPITIA MBUGA YA SERENGETI(Matumizi mabaya ya kodi zetu)
- LOLIONDO
- BARABARA YA KILWA NA MANDELA KAZI KURUDIWA(Matumizi mabaya ya kodi zetu
Kwa Asili ni sisi ni matajiri, tunafilisiwa na wapuuuzi
Haiwezekani madudu yote hayo, hakuna hata mwenye hatia ukitoa Liyumba.
Ukinunua soda ya 500Tsh umetoa 90Tsh. kama kodi.
Amkeni, Toeni sauti, Nchi inakwisha.:target:
Nonda,
Anza na wadau huko huko Gongo La Mboto Mwisho wa Lami,SunguraTex(KIU), Mombasa, Mzambarauni, Mzizini na Majohe
Nategemea Viongozi pia wamesikia muda umekaribia, Rais Wangu amesema Januari analianzisha la katiba.
Ishu ya katiba ifunguliwe Rasmi na Maandamano haya ili watu wafahamu, kIsha Operation Katiba Ianze.
Hawa ni wezi na Mafisadi wanaokumbatiana, hakuna kuwaogopa Tena.
Namuogopa MUNGU pekee, hivyo namtiii- Mafisadi siwaogopi nikifa mimi najua Elfu watasimama badala yangu
:whoo:
Peoples......Power
mkakati ni huu tuma ujumbe wa simu kwa watu unao wafahamu kama walivyofanya msumbiji kwa njia ya simu hili tunaliweza kuingia mitaani hatuna sababu yakuchelea andika hivi wote maandamano ya amani ya kudai vyote vilivyoorodheshwa hapo siku ya jumanne nchi nzima
Mimi nasema tuamue tusiende kazini siku moja kwa kila mmoja awe mkulima hadi mfugaji lakini hii hamasa tukiiweka kwenye ballot box si tosha kabisa
Mkuu,
Nimekufahamu vizuri tu.
Usisahau wazo ni maandamano nchi nzima, sio Dar tu.
Kwa hiyo, kutokana na wananchi wengi kutokuwa na muamko ndio maana nikashauri kutumia network ya vyama vya upinzani,katika kila mji,wilaya ,mkoa Tanzania kuna at least network ya chama kimoja cha upinzani ,hii itafanya kazi ya kuelimisha wananchi juu ya haya uliyoyaorodhesha kuweza kufafanuliwa kwa wananchi.
Wananchi wakishaelimika juu ya hili basi ugumu utakuwa umepungua, atakapotokea kuandamana atajuwa mtu anaandamana kwa sababu gani. Sio kuja kusema nimeeambiwa na kiongozi wangu au mtu fulani niandamane.
Ili maandamano yawe na impact tunayoitegemea basi ni lazima yapangwe, yapangike yasiwe ad hoc ! yakiwa adhoc ni rahisi kuwa branded « wahuni wachache ! ». na polisi hii tuijuavyo, watapata kazi wanayoipenda, kuwadhalilisha wananchi. Tusiwape nafasi hiyo au kisingizio.
Unless hapa hatuzungumzii tena « maandamano ya amani » bali ni unrest ! au fujo!
Wazo lako ni zuri mkuu,ila tusikurupuke tu kwa jazba.
Naunga mkono tuandamane kupinga kwanini watanzania tunakuwa mabwege nasema nikotayari kuandamana hata kufa
1. Shomari, nani kakudanganya huo msemo kwenye nyekundu ni wa Kikwete??
2. Swali lako....."nani aanzishe" = very simple, tuanze kujiorodhesha hapa hapa:
- M-mbabe
- Spencer
- Iwanga
- Ezan
- Stein
- Byendangwero
- King of Kings
- Bruce Lee
- Wewe mwenyewe (Shomari)
- El Nino (huyu tutambeba juu juu kibabe maana anataka kuleta logic nyingi)
Tukiyaita "maandamano" tutalazimika kuomba kibali kwa S. Mwema. Tuyaite " Matembezi ya Amani Nchi Nzima". Mwishoni mwa matembezi hayo tunapeana mikakati ya kuiboresha nchi kiutawala. Faida ya kuyaita "Matembezi" ni kuwa wale ambao walikuwepo tangu enzi za TANU itakuwa rahisi kuelewa somo kwani watakumbuka "Matembezi ya Mshikamano"
Mkuu,
Wazo lako ni zuri, zuri sana!
Nani ata-coordinate maandamano hayo?
Nategemea jawabu ya, wote wanaochukia ubadhirifu wa mali za umma na ufisadi
Ugumu wa kulitekeleza wazo lako.(Kama nilivyosema ni wazo zuri,mimi naliunga mkono)
Katika Tanzania ya leo, nakusudia nchi ambayo wananchi wake wengi hawana elimu ya uraia(civic education) na hakuna juhudi za makusudi zinazofanywa ili kurekebisha udhaifu huu.kuwafanya watu watambue haki zao na wajibu wao kwa taifa.
Kwenye nchi ambayo muamko wa wananchi juu ya haki zao katika taifa ni mdogo sana.
Kwenye nchi ambayo kila mmoja wetu anasubiri mwenzake afanye, aanzishe jambo la kuwanufaisha wananchi wote.
Kwenye nchi ambayo serikali iliyopo madarakani kwa miongo zaidi ya minne inachukulia udhaifu huo nilioutaja hapo juu kama mtaji wa kukinufaisha kikundi kidogo cha jamii kumiliki, kuharibu, kujitwalia kila kitu,kurubuni mlalahoi wakati wa kura, vyombo pekee ambavyo tungetegemea vingefanikisha wazo lako ni Asasi za kiraia, vyama vya wafanyakazi, jumuia za wananchi, na vyama vya siasa.
Hapa sitaji,vyama vya wasomi na wanasheria kwani hivi kazi yao nikuitisha makongamano, warsha waalikwa ni wavaa tai na suti, si mlalahoi, kuandika magazetini, au kusubiri kuhojiwa watoe mawazo yao halafu wanakwenda zao bar kupata bia na kiti moto au soda na chipskuku, siku inakuwa imepita!
Asasi nyingi zinaanzishwa sio kwa lengo la kumnufaisha mwananchi. Mwananchi mlalahoi hutumiwa tu kama kisingizio cha kuombea fedha kutoka kwa mfadhili,wafadhili ili watu wamege donge nono,watunishe mifuko yao na fedha kidogo humfikia mlengwa na huwa geresha tu.
Sina nia ya kusema kuwa ni asasi zote ila majority ziko hivyo. Kwa hiyo asasi hizi hazitajibebesha jukumu hili la kuandaa maandamano ya amani kwa nchi nzima. Hali kadhalika jumuiya za wananchi na vyama vya wafanyakazi havina ubavu huo, ziko weak sana.
Kimbilio pekee ni vyama vya siasa vya upinzani. Vyama hivi vikiamua,vikiweka manunguniko ya wananchi na maslahi ya taifa mbele vinaweza kuthubutu kuitisha maandamano kwa nchi nzima. Ni bahati mbaya kuwa havijitambui kuwa maslahi ya taifa ni superior kuliko kujitangaza kichama. Kukosekana kwa ujasiri na utashi kwa vyama hivi kuwa na sauti ya pamoja katika kuiwajibisha serikali inayokumbatia uoza,ufisadi,ubadhirifu wa mali ya umma ni ufinyu wa mawazo wa viongozi wa vyama hivyo.
Tusitegemee CCM kuitisha maandamano ya nchi nzima kuitaka serikali iwajibike kwa wananchi.
Lakini hili la vyama vya upinzani kushindwa kufanya hili ni uwendawazimu. Kama lugha hii ni kali basi niseme viongozi wa vyama vya upinzani wana muono finyu kama vyama vya siasa.
Wao wanapokuja kuomba kura hutuambia tuwachague ili wakatutumikie, wakatuwekee mambo sawa, ok, siku ya kushika hatamu haijafika lakini wanataka tuamini kuwa hata ku-coordinate na ku-organise maandamano ya wananchi kwa nchi nzima kunawashinda ?
Ubinafsi wa kila chama kuwa kinataka kionekane kuwa ndio chama dume,chama kikuu cha upinzani kisiwe kikwazo cha kushirikiana katika mambo, au jambo linalowaunganisha wananchi wote.
Mkuu, mchango wangu katika kuunga mkono wazo lako, ni kuwaomba wanaJF ambao wanaweza kupata sikio la hawa viongozi wa vyama vya upinzani wawapitishie ujumbe huu. Halafu baada ya miezi mitatu tuone kama watapata utashi na ujasiri wa kuja pamoja kama nguvu moja itakayowakilishia vilio vya wanyonge.
Kama wao watashindwa, kwa mazingira ya Tanzani yalivyo hii leo, basi kuitisha maandamano ya nchi nzima itabaki kuwa ni ndoto. Hatuko tayari, bado jamii inapiga mbonji ! na kukoroma.
1. Shomari, nani kakudanganya huo msemo kwenye nyekundu ni wa Kikwete??
2. Swali lako....."nani aanzishe" = very simple, tuanze kujiorodhesha hapa hapa:
- M-mbabe
- Spencer
- Iwanga
- Ezan
- Stein
- Byendangwero
- King of Kings
- Bruce Lee
- Wewe mwenyewe (Shomari)
- El Nino (huyu tutambeba juu juu kibabe maana anataka kuleta logic nyingi)