PostGE2025 Maandamano ya 9D yamekaa kimtego sana

PostGE2025 Maandamano ya 9D yamekaa kimtego sana

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Kizibo

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
4,554
Reaction score
10,327
Nimekaa nikatafakari, nikagundua haya maandamano ya 9D ni myego mkubwa sana kwa pande zote mbili, serikali na Gen Z wote.

1 Gen Z tusipoandamana kama tunavuohamasishana mitandaoni, au serikali ikifanikiwa kuzima au kuzuia hayo maandamano, maanake Gen Z tutakuwa tumepoteza pambano. Kitakachofuata..tutaishi kwa tabu sana. Watawala watatufanya chochote watakavyojisikia. Watatuteka, watatuua, watachota mali za umma vile watakavyo na hatutakuwa na mtetezi.

Serikali ikitudhibiti Gen Z, maanake kwa miaka yote, yoyote atakaethubutu kuinua mdomo ni kuuawa tu.

2 Ikiwa Gen Z tutaandamana kwa wingi, kisha serikali ikaua tena kama ilivyoua siku ile ya MO29, kipi kitafata kwa serikalli?? Jumuia za kimataifa watachukua hatua gani?? Au wataacha tuuane tu kwa kuwa ni swala la mambo ya ndani (Home affairs)

Na je, Gen Z watakaosalimika na wanachi watakao kuwa wamepoteza watoto, wazazi, ndugu jamaa na marafiki wataridhika na kukubaliana na swala la kuuliwa kwa wapendwa wao kwa mara ya pili?? Au ndo utakuwa mwanzo wa watu kutafuta na kuingiza siraha nchini kimagendo na kuanzisha ugaidi na uasi msituni ili kulipiza??

3 Ikiwa serikalli itaacha maandamano yawepo na watu waandamane kwa amani, kitakachofata ni MAFURIKO YA RAIA KARIBIA WOTE KUINGIA BARABARANI. sasa hapa ndo serikali na ccm wataona ni kwa namna gani watu hawapo upande wao.

Hata wazee na watoto watajaa barabaarani. Matokeo yake serikali itaanguka mapema asubuhi.

Kwa ujumla, swala la 9D limekaa kimtego na kimkakati sana.

Nawasilisha
 
Mkuu hii kitu ni nature ya mwanadamu. Unapomtesa mtu sana tegemea kuna siku atareact, atahitaji ukombozi.

Na kibaya au kizuri akishareact huwa hakuna kurudi nyuma hadi lengo litimie.

CCM inajaribu kupingana na Nature.
 
Watawala tu wapo na upper hand ya kuzuia maandamo lakini kwa mwelekeo wao wa maneno na matendo kuna maandamano ambayo yatazaa uasi hata kama siyo trh 09
Kinachosikitisha tukifika hatua hiyo ya uasi au machafuko watawala huwa wanakimbia nchi. Huu ujinga wa kuaribu nchi harafu kukimbia bila kuchukukiwa hatua huwa unanikera sana. Mtu kasababisha vifo halafu unasikia anaishi uamishoni, na ndio basi hapo aliyoyafanya hawajibiki nayo tena. Kuwepo na sheria za kimataifa kupiga marufuku nchi kupokea kiongozi yoyote sliesababisha machafuko nchini kwake. Umesababisha machafuko nchini kwako bako hapo hapo nchini kwako kusubiri hatma yako.
 
Imekaa kimtego haswaaa, ila mm my take naona;

Serikali sasa hv haitoweza kuchukua hatua zozote kali kwasababu wapo pabaya sana ..kila camera inaangazia nn kinaendelea Tanzania....vyombo vya nnje vipo on high alert hasa baada ya kusikia nn kimetokea wiki kadhaa zilizopita. So sidhani kama watafanya waliyoyafanya, zaidi ya kutumia measures za kawaida tu za kutawanya watu, maybe mabomu ya machozi and such. So ishu sasa hv ipo mikononi mwa wananchi na ndio maana njia pekee imebaki, ni kuwagawanya wananchi wasiwe na umoja, iwe kidini, kikabila au whatever.
 
Waruhusu tu watu waandamane kwa amani. Penyewe wameshinda uchaguzi kwa 97.66 ya kura zote! Hofu ya nini? Mbona watakaojitokeza kwenye hayo maandamano ni 2% tu ya wapiga kura na vijana wao wachache!!

Polisi, fanyeni basi mruhusu hayo maandamano yafanyike kwa amani na utulivu. Nyinyi kaeni tu pembeni muangalie. Hakuna sababu ya kuua raia wasio na silaha.
 
Waruhusu tu watu waandamane kwa amani. Penyewe wameshinda uchaguzi kwa 97.66 ya kura zote! Hofu ya nini? Mbona watakaojitokeza kwenye hayo maandamano ni 2% tu ya wapiga kura na vijana wao wachache!!

Polisi, fanyeni basi mruhusu hayo maandamano yafanyike kwa amani na utulivu. Nyinyi kaeni tu pembeni muangalie. Hakuna sababu ya kuua raia wasio na silaha.

Maandamano ya amani yenye lengo la kuangusha serikali. Uliwahi yaona wapi Mkuu?
 
Ukikaa ndani unapigwa risasi ,ukitoka unapigwa risasi ila angalau upo field ila pia uwezo wa kupona ni mkubwa , so bora kutoka tu.

Ushauri hata kama maandamano vyoyote vile yatakua ,ila barabara kuu zinazo ingia kila mkoa zifungwe.

Police ndo huanzisha vurugu so iyo siku maandamano yalindwe na jwtz tu ,

Inatakiwa siku iyo ni jwtz na waandamanaji kwenye barabara basi ,

Sio mbaya wenginge mkiendele kujitolea kupika masufulia ya wali ,maji , Ugali, mikate n.k kwa ajili ya waandamanaji.

Maduka fungeni wekeni katoni za maji, vitu vidogo kama biskuti ,au pipi wape waandamanaji , na msiwe mbali na mali zetu ili kusaidiana na nao kudhibiti waporaji,
 
Na bet maandamano ya 9dec yatakuwa sio ya amani..

Matokeo au majibu mpaka leo hayajapatikana
Sasa utayapataje kwa njia ya amani?
 
Back
Top Bottom