Maandamano: Hali iliyotoweka sasa yarudi tena!

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
WanaJF:

Baada ya JKI kuingia madarakani miaka mitano iliyopita, mivutano baina ya vyama vya siasa vya upinzani na serikali (yaani polisi) kuhusu maandamano ilionekana kutoweka kabisa.

Wengi waliipongeza serikali ya JK kwa kuiondoa mivutano hiyo ambayo ilikuwapo kwa takribankipindi chote cha Mkapa. Itakumbukwa yule IGP Mahita daima alikuwa anavutana na wapinzani, wakati huo CUF (iliyokuwa na nguvu kubwa) kuhusu maombi yao ya kufanya maandamano.

Mahita aliibua ile kauli yake maarufu dhidi ya CUF: “Kama nyie ngangari, basi mie ni ngunguri.”

Askari wake walikuwa wanatembeza virungu dhidi ya wafuasi wa CUF na kuwaumiza vibaya, akiwemo hata mwenyekiti wao Lipumba ambaye aliwahi kuvunjwa mkono.

Miaka mitano ya JK tumeona maandamano yakiruhusiwa bila pingamizi na polisi wakiyalinda, na yalifanyika kwa amani, hadi watu wakafikia kusema; “kumbe ni polisi ndiyo huwa wanaanzisha vurugu kwenye maandamano.”

Baada ya uchaguzi huu tunaona tena hali ya wakati wa Mkapa na Mahita inaanza kujirudia polepole – maandamano ya wapinzani – hasa ya Chadema (chama cha upinzani ambacho sasa ndiyo chenye nguvu) yanakataliwa kwa sababu zisizo na msingi.

Tumeshuhudia kule Arusha wiki hii, maandamano ya Chadema yakikataliwa eti kwa kisingizio kwamba idara ya polisi haina askari wa kuyalinda – huku ikipeleka kwenye uwanja wa mkutano askari kibao kwa lengo la kuyazuia maandamano.

Kulikoni serikali ya JK sasa? Inaogopa nini? Kwa nini isiendeleze tu sera yake ya awali ya kuyaruhusu maandamano na kuyalinda kama ilivyokuwa katika miaka yake mitano iliyopita?
 
WanaJF:

Baada ya JKI kuingia madarakani miaka mitano iliyopita, mivutano baina ya vyama vya siasa vya upinzani na serikali (yaani polisi) kuhusu maandamano ilionekana kutoweka kabisa.

Wengi waliipongeza serikali ya JK kwa kuiondoa mivutano hiyo ambayo ilikuwapo kwa takribankipindi chote cha Mkapa. Itakumbukwa yule IGP Mahita daima alikuwa anavutana na wapinzani, wakati huo CUF (iliyokuwa na nguvu kubwa) kuhusu maombi yao ya kufanya maandamano.

Mahita aliibua ile kauli yake maarufu dhidi ya CUF: “Kama nyie ngangari, basi mie ni ngunguri.”

Askari wake walikuwa wanatembeza virungu dhidi ya wafuasi wa CUF na kuwaumiza vibaya, akiwemo hata mwenyekiti wao Lipumba ambaye aliwahi kuvunjwa mkono.

Miaka mitano ya JK tumeona maandamano yakiruhusiwa bila pingamizi na polisi wakiyalinda, na yalifanyika kwa amani, hadi watu wakafikia kusema; “kumbe ni polisi ndiyo huwa wanaanzisha vurugu kwenye maandamano.”

Baada ya uchaguzi huu tunaona tena hali ya wakati wa Mkapa na Mahita inaanza kujirudia polepole – maandamano ya wapinzani – hasa ya Chadema (chama cha upinzani ambacho sasa ndiyo chenye nguvu) yanakataliwa kwa sababu zisizo na msingi.

Tumeshuhudia kule Arusha wiki hii, maandamano ya Chadema yakikataliwa eti kwa kisingizio kwamba idara ya polisi haina askari wa kuyalinda – huku ikipeleka kwenye uwanja wa mkutano askari kibao kwa lengo la kuyazuia maandamano.

Kulikoni serikali ya JK sasa? Inaogopa nini? Kwa nini isiendeleze tu sera yake ya awali ya kuyaruhusu maandamano na kuyalinda kama ilivyokuwa katika miaka yake mitano iliyopita?

Mi nadhani ni woga mkubwa umemwingia JK kutokana na kwamba huenda hakushinda uchaguzi.
 
WanaJF:

Baada ya JKI kuingia madarakani miaka mitano iliyopita, mivutano baina ya vyama vya siasa vya upinzani na serikali (yaani polisi) kuhusu maandamano ilionekana kutoweka kabisa.

Wengi waliipongeza serikali ya JK kwa kuiondoa mivutano hiyo ambayo ilikuwapo kwa takribankipindi chote cha Mkapa. Itakumbukwa yule IGP Mahita daima alikuwa anavutana na wapinzani, wakati huo CUF (iliyokuwa na nguvu kubwa) kuhusu maombi yao ya kufanya maandamano.

Mahita aliibua ile kauli yake maarufu dhidi ya CUF: “Kama nyie ngangari, basi mie ni ngunguri.”

Askari wake walikuwa wanatembeza virungu dhidi ya wafuasi wa CUF na kuwaumiza vibaya, akiwemo hata mwenyekiti wao Lipumba ambaye aliwahi kuvunjwa mkono.

Miaka mitano ya JK tumeona maandamano yakiruhusiwa bila pingamizi na polisi wakiyalinda, na yalifanyika kwa amani, hadi watu wakafikia kusema; “kumbe ni polisi ndiyo huwa wanaanzisha vurugu kwenye maandamano.”

Baada ya uchaguzi huu tunaona tena hali ya wakati wa Mkapa na Mahita inaanza kujirudia polepole – maandamano ya wapinzani – hasa ya Chadema (chama cha upinzani ambacho sasa ndiyo chenye nguvu) yanakataliwa kwa sababu zisizo na msingi.

Tumeshuhudia kule Arusha wiki hii, maandamano ya Chadema yakikataliwa eti kwa kisingizio kwamba idara ya polisi haina askari wa kuyalinda – huku ikipeleka kwenye uwanja wa mkutano askari kibao kwa lengo la kuyazuia maandamano.

Kulikoni serikali ya JK sasa? Inaogopa nini? Kwa nini isiendeleze tu sera yake ya awali ya kuyaruhusu maandamano na kuyalinda kama ilivyokuwa katika miaka yake mitano iliyopita?


JK aliruhusu maandamano kwa lengo la kuwafurahisha wazungu anakoendaga kuhemea ili waTZ tusife na njaa. si unajua wazungu wanaheshimu demokrasia? jk alikuwa anajifanya naye ni mmoja wao.

sasa wazungu wanamuona kama mvurugaji wa demokrasia na serikali yake ina kashfa za rushwa kubwa-kubwa. wazungu wameamua kumtosa. hawezi kuruhusu tena maanadamano kwa sababu hayana faida tena kwake yeye binafsi na utwala wake.
 
kwa sasa hahitaji tena kura zenu, hata akitoa kipondo hana shida na nyinyi, si mlimchagua?
 
Mi nadhani ni woga mkubwa umemwingia JK kutokana na kwamba huenda hakushinda uchaguzi.

Hakushinda.................... Huoni hata kulihutubia taifa anashindwa hata siku ya uhuru. Hivi zile hotuba za mwezi bado zipo?? Matatizo amejitafutia mwenyewe kwa kulazimisha matokeo. Sasa roho inamsuta.
 
mwacheni jamani mtoto wa watu kwa sasa bado yuko kwa Obama anakula raha kidogo,atakapopumzika basi atapata nguvu za kuhutubia, sio kazi rahisi jamani kuhutubia kila mwezi maana mbaya zaidi haoni chochote alichokifanya tangu aingie madarakani zaidi ya bei za vitu kupanda maradufu, msishangae jamaa anakuja na wazo la kuibinafisisha IKULU walau kwa miaka mitatu ya term yake.
Hakushinda.................... Huoni hata kulihutubia taifa anashindwa hata siku ya uhuru. Hivi zile hotuba za mwezi bado zipo?? Matatizo amejitafutia mwenyewe kwa kulazimisha matokeo. Sasa roho inamsuta.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom