Maana ya msemo 'waja leo waondoka leo'?

Maana ya msemo 'waja leo waondoka leo'?

Makini

Senior Member
Joined
Dec 23, 2014
Posts
154
Reaction score
59
Wakuu,

Kuna anayefahamu maana ya msemo 'waja leo waondoka leo'? Kama sijakosea watu kuutumia kuzungumzia mji wa Tanga.

Maana yake ni nini? Ningependa kujuzwa tafadhali.
 
Ukisafiri toka Dar kwenda Tanga sio mbali kihivyo kwamba wafika wafanya shughuli yako na bado utapata usafiri (public) wa kurudi siku hiyohiyo. Ahsante
 
kutakuwa hakuvutii sana hivyo ukifika hakuna cha kukushawishi ubaki lazima utarudi tu.
 
Wakuu,

Kuna anayefahamu maana ya msemo 'waja leo waondoka leo'? Kama sijakosea watu kuutumia kuzungumzia mji wa Tanga.

Maana yake ni nini? Ningependa kujuzwa tafadhali.

Huu ni msemo wa kukushawishi usiondoke. "Waja leo waondoka leo?"
Wakazi wa Tanga hawafurahii mgeni aliyekuja aondoke. Tabia na ukarimu wao mara nyingi unamshawishi mgeni asitake kuondoka. Na hata akiondoka atamani kwenda Tanga tena. Hivyo msemo huo uko katika mfumo wa swali la kukushangaa wewe mgeni unayekuja na kutaka kuondoka haraka haraka. Ukiingia Tanga utaona kibao cha kukukaribisha,lakini ukiondoka hutaona kibao cha kukuaga.
 
Jimena njoo toa msaada huku
 
Last edited by a moderator:
dapangi, asante sana mkuu. Umenielewesha vizuri sana, mi sikujua hata kama ni swali.
 
Last edited by a moderator:
nafikiri kabla ya kutoa maana ya neno mzungu kimtazamo au kimazingira ni vyema kwanza kujua maana ya neno mzungu kimaana na asili yake.
kimaana kwa mujibu wa kamusi ya mtandaoni ya oxford neno mzungu kwa kiingereza ni dexterity lenye maana ya clever skill : the ability to think and act quickly and cleverly.
asili nimetafuta nimeshindwa:shock:. kwangu neno mzungu watanzania wa zamani walilitumia kuwaita watu weupe hasa wakoloni kwani walionekana kuwa na uwezo mkubwa kuwazidi. ile kasumba iliendelea kizazimpaka kizazi
 
naomba nichangie kama ifuatavyo
Kihistoria(etymologically) msemo huu ni wa zamani sana na hautumiki tu kila pahala. hutumika pale mgeni anapokuwa anawaaga wenyeji wake
. anapokuwa anawaaga kuwa anaondoka ,wenyeji ndio huhamaki kuwa kwa nini unaondoka na kuwa bado wanatamani waendelee kukaa na mgeni na wanaona muda aliokaa ni mdogo mno ni km vile alikuja sku hiyo hiyo na anataka kuondoka siku hiyo hiyo.ndipo hapo wenyeji humwambia 'waja leo waondoka leo'.yote ni kuonesha ukarimu na kumjali mgeni.
Tanga wana misemo mingi sana kuhusu mgeni....
pia kuna msemo '.....ukirudi mgeni wa nani'? msemo huu hutumika pale mgeni au mwenyeji anaposafiri bila kuwaaga au kutoa taarifa kwa wanaomzunguka.
 
Wakuu,

Kuna anayefahamu maana ya msemo 'waja leo waondoka leo'? Kama sijakosea watu kuutumia kuzungumzia mji wa Tanga.

Maana yake ni nini? Ningependa kujuzwa tafadhali.
Chanzo cha msemo huu ni wimbo wa Remmy Ongala, nafikiri unaitwa mdundiko. Ukiusikiliza ndio anamuongelea mpenzi wake anayeelekea kuishi Tanga na anakuja Dar na kurudi Tanga siku hiyo hiyo.
 
Huu ni msemo wa kukushawishi usiondoke. "Waja leo waondoka leo?"
Wakazi wa Tanga hawafurahii mgeni aliyekuja aondoke. Tabia na ukarimu wao mara nyingi unamshawishi mgeni asitake kuondoka. Na hata akiondoka atamani kwenda Tanga tena. Hivyo msemo huo uko katika mfumo wa swali la kukushangaa wewe mgeni unayekuja na kutaka kuondoka haraka haraka. Ukiingia Tanga utaona kibao cha kukukaribisha,lakini ukiondoka hutaona kibao cha kukuaga.

uko sahihi, hiyo ndiyo maana ya 'waja leo waondoka leo?'
 
Back
Top Bottom