maana ya maneno haya ni ipi?

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,108
115,837
kuna mdada mmoja sikuwahi kumtongoza
nilifahamiana nae kikawaida.kiofisi zaidi....

sasa juzi nimekutana nae...nikamwambia karibu weekend
moja maeneo ya kwetu...

akanijibu subiri nilee kwanza....
kwa sababu ametoka kujifungua karibuni,

well alimaanisha nini?au alielewa vinginevyo?

halafu kuna msemo mwingine nimewahi sikia wanawake
wakiusema in way huwa najiuliza exactly wanamaanisha nini?

utasikia wakisema kuna wanaume hata ukiwabeba mgongoni hawaridhiki..
now hapa kubebwa mgongoni humaanisha nini hasa???????
 
Ngoja alee kwanza maana yake yuko bize na malezi hana nafasi ya kukaribia kwako!

Hilo lingine ni kwamba huyo mwanaume anaesemwa haridhiki hata apewe au afanyiwe nini. Yani haya ndo yakukufelisha mtihani?
 
Ngoja alee kwanza maana yake yuko bize na malezi hana nafasi ya kukaribia kwako!

Hilo lingine ni kwamba huyo mwanaume anaesemwa haridhiki hata apewe au afanyiwe nini. Yani haya ndo yakukufelisha mtihani?

mhhh
mtu kusema ngoja nilee siokwamba
anahisi utaomba kitu na hataki kubemenda mtoto?

na kubebwa mgongoni sio mambo ya pwani?

au mimi mawazo yangu potofu????????
 
mhhh
mtu kusema ngoja nilee siokwamba
anahisi utaomba kitu na hataki kubemenda mtoto?

na kubebwa mgongoni sio mambo ya pwani?

au mimi mawazo yangu potofu????????
Yote mawazo potofu...unaona kisichokuwepo!
 
Labda pia na wewe umemuelewa vibaya, alimaanisha yeye kwenda out mahala wakati ana mtoto mdogo hawezi
 
Anaposema subiri alee maana yake ni kwamba anajua utamwomba kitumbua ambacho siyo vizuri kula wakati ananyonyesha. Na anaposema hata ukimbeba maana yake hata akikupatia
mtandao ule maarufu unaopendwa na wengi bado huridhiki.
 
Back
Top Bottom