simplemind
JF-Expert Member
- Apr 10, 2009
- 16,409
- 9,183
Kuongezeka kwa bei ya bidhaa au huduma bila shaka ni jambo linatugusa sote. Kupanda kwa gharama za maisha ni kilio cha watanzania wote. Swali hapa ni nini maana halisi ya mfumuko wa bei mfano asilimia 19 Tanzania na asili mia 7 Rwanda ? Hii 19 na 7 zinapatikana vipi kihesabu (calculation)?. Pili nini chanzo cha mfumuko wa bei na kwa nini bei ya huduma au bidhaa nadra kuteremka siku zote inapanda tu?