Maana halisi ya inflation rate a.k.a mfumuko wa bei.

simplemind

JF-Expert Member
Apr 10, 2009
16,409
9,183
Kuongezeka kwa bei ya bidhaa au huduma bila shaka ni jambo linatugusa sote. Kupanda kwa gharama za maisha ni kilio cha watanzania wote. Swali hapa ni nini maana halisi ya mfumuko wa bei mfano asilimia 19 Tanzania na asili mia 7 Rwanda ? Hii 19 na 7 zinapatikana vipi kihesabu (calculation)?. Pili nini chanzo cha mfumuko wa bei na kwa nini bei ya huduma au bidhaa nadra kuteremka siku zote inapanda tu?
 
Kwa mujibu wa muandishi m1 hv anasema kwamba hiyo 19% inflation rate ni uongo hipo zaidi ya 50-200%:

Kuongezeka kwa bei ya kitu;
Mf: mwaka juzi ulinunua mchele kilo 800 mwaka huu unanua kilo 2400 that means kuna ongezeko la bei kwa 200%
Sasa sijui wanafanyaje wanapata 19%
 
Tungoje wataalamu wa hii kitu waje hapa watudadavulie.
 
man unapoongelea inflation ni suala pana sana na limejikita sana sana katika mzunguko wa maisha ya kibinadamu. example in tanzania republic, according to BOT in 2005 inflation rate was 5% but now is 19% sijui hayo mahesabu wameyafanyaje au ndo uchumi unapaa kama ndege. angalia hali halisi especially in the basic needs (food,clothes and shelter) from 2005 t0 2012 mchele per kg was 800 tsh but now is 2400tsh per kg so inflation there is almost 200%. sugar was 700 per kg now is 2500 to 2750 per kg so inflation there is also like 200%.
unapoongelea bidhaa adimu usitegemee ata siku moja kikashuka bei sababu ishakuwa ni bidhaa adimu vilevile usisahau na hizi consumer goods amabazo ndo basics za maisha ya kila mwanadamu katika dunia hii, hizo ndo zipo ghali sana hata kama zinapatikana kwa wingi, kumbuka kila sehemu kuna bidhaa adimu zinatofautiana kulingana na mahitaji.

causes of inflation
1 monetary policy
eg - exchange rate,per capta income,foreign currency reserve,import and export etc.

2 fiscal policy
In Tanzania, inflation may be linked to the value of the national currency, as well as increased cost of living expenses (food, shelter, heat, light, etc.). In most countries, inflation occurs when food prices soar; this is certainly true in the African nation of Tanzania, where food prices have risen to all-time highs.

Inflation in Tanzania presents particular problems for the citizens of that country, since Tanzania is a third-world nation with very high poverty levels. Higher food prices present terrible challenges to ordinary citizens, who often earn a fraction of what people in the Western world would receive for similar work.

Also, there are few social programs in Tanzania to help those who can`t afford to buy goods and services due to inflation; if they lived in America or Canada, they would likely be eligible for welfare, food stamps, social housing or other services designed to assist society`s poorest citizens. However, in Africa, this sort of support safety net (or infrastructure) is not yet in place.

Hope For Tanzania

• International relief agencies offer hope to Tanzania, despite the country`s unprecedented inflation levels. These agencies operate in many African nations, offering food, shelter, education, medical care and advice to poor Africans. Philanthropic societies and organization may be secular, or they may have religious affiliations. Whether relief workers are religious or not isn't really very important - the services they deliver to the needy are always appreciates; regardless of religious denomination.

There are no signs of deflation in Tanzania`s current economy; how high the cost of living will rise is still subject to debate. For citizens of Tanzania, inflation represents undue pressure to come up with money for the basic necessities of life. Hopefully, in time, government officials can work with economists to search for long-term solutions that make life easier for Tanzanians.


tunaendelea tena//changanua kidogo apo.
:A S 465:
 
Kikwet.e anaifilisi nchi sasa hiv tunaemea pua moja tupo icu hali mbaya maji ya uhai ya lita 5 tulikua tunanua kwa 800 now tunanua kwa 1800 duu,maziwa ya kopo medium size ilikua 4500 sasa 8000-9500,nauli ilikua 150 sasa 300,mafuta ya taa ilikua 650 sasa 2056,kibiriti ilikua sh20 sasa 100,soda ilikua 200 sasa 600,feni ilikua 8000 sasa 35000,jeikei fukuza hao kina ndulu na mkulo ni makanjanja hawajui wanachofanya
 
Kila index unayoitumia lazima utafute base year. Kwa hiyo kwa mfumuko wa bei huwa ni mwaka uliopita. Yaani tutakapoongelea inlation ya mwaka 2011tutatumia CPI (consumer price index) ambayo base year yake ni 2010. Kwa hiyo unapongelea bei ya mchele ya 2011 kuwa kilo ni sh 2050 dhidi ya sh 800 za mwaka 2005 utakachopata ni ongezeko la miaka 5 au 6. Inflation inapimwa kwa misingi ya mwaka hadi mwaka. Chukua bei ya 2011 toa na bei ya 2010 halafu hiyo tofauti yake igawanye kwa bei ya mwaka 2010 kisha zidisha mara 100. hiyo index unayopata ndiyo mfumuko wa bei kwa mwaka.

Kwenye uchumi base year ni kitu cha muhimu sana na kupima kwa vipindi vya mwaka mmoja mmoja ndiyo kigezo sahihi. Wachumi wa kale 'contemporary economists' wali tafsiri mfumuko wa bei kama "Too much money chasing too few goods"
 
mimi bado sijaelewa. Anyway somebody help please, hivi 1kg ya mchele au sukari kule Londön au New York ni bei gani?
 
mimi bado sijaelewa. Anyway somebody help please, hivi 1kg ya mchele au sukari kule Londön au New York ni bei gani?

Bei ya mchele wa London haikusaidii wewe kupanga bei yako kwani kuna tofauti katika factors of production za London dhidi ya Nchi yako. Ninapoongelea factors of production ninamaanisha technnoogy, price of labour na hata tax regime. Unapopima inflation ni kwa nchi husika kwa kipindi fulani tu, jinsi gani bei za vitu zinapanda au kuteremka.

Vilevile kama uzalishaji wa bidhaa za kuuza nje ni mdogo na kodi inayokusanywa haikidhi mahitaji ya nchi, basi viongozi wasio makini wanafanya kama yale aliyoyafanya Mobutu Seseseko au Iddi Amini Dada wa Zaire na Uganda respectively ya kukopa kwenye mabenki. Kukopa benki ni kitendo cha kuchapisha noti na kuziingiza kwenye mzunguko bila kuzingatia ukuaji halisi wa uchumi. Hivyo ile dhana ya too much money chasing too few goods ndiyo hutokea hapa.

Kwa mazingira ya nchi yetu unaweza ukaangalia kama kweli kuna uzalishaji unoongezeka katika sekta za kilimo, madini, utalii, viwanda na biashara ambao unatuwezesha kuwa na bidhaa nyingi za kutumia na kuuza nje ya nchi? BOT wanazo takwimu pamoja na National Bureau of Statiscs. Ukipata jibu jiulize tena je serikali yetu kwa kipindi hicho imewahi kukopa benki mara ngapi, then utapata jibu la uwepo wa inflation au mfumuko wa bei.

Uchumi wetu ukiuangalia umegubikwa na uchumi wa wachuuzi au walanguzi. Wafanya biashara wanunue fedha za kigeni nchini ili wakanunue bidhaa Hongkong, Ghuangzou na miji mingine duniani kisha walete Kariakoo kwa ajili ya kuuza.Tunaletewa kuanzia vijiti vya kuchokonolea meno hadi nguo wakati nchi yetu ina pamba na misitu ya kutosha. Kwa hiyo uwiano kati ya biashara ambayo Tanzania inauza nje dhidi ya biashara ambayo Tanzania inaagiza (balance of payment) ni mbaya kwa nchi yetu. Kwa mazingira haya tutakuwa tunalia kila siku kuhusu mfumuko wa bei kama hatutawekeza katika viwanda. Yaani badala ya kuexport magogo au pamba ghafi basi angalao tutengeneze mbao au nyuzi ndiyo tusafirishebili na sisi tuweze kuongeza fedha za kigeni.
 
Kwa mujibu wa muandishi m1 hv anasema kwamba hiyo 19% inflation rate ni uongo hipo zaidi ya 50-200%:

Kuongezeka kwa bei ya kitu;
Mf: mwaka juzi ulinunua mchele kilo 800 mwaka huu unanua kilo 2400 that means kuna ongezeko la bei kwa 200%
Sasa sijui wanafanyaje wanapata 19%

huyo ni mwandishi na si mchumi
 
Back
Top Bottom