Maalum kwa ajili ya wanyama pori

PANTHERA LEO

JF-Expert Member
Jan 25, 2019
2,301
3,429
Habari gani members wa JF? Kama una swali lolote kuhusu Hifadhi zetu za taifa, pia maswali kuhusu wanyama pori wa hapa EAST AFRICA(mammals,reptiles,birds,etc) na baadhi ya maswala yanayohusu utalii. Unaweza ukauliza hapa!

Kwa wale ambao hawana idea ngoja niwadokeze kidogo!

Kwa Tanzania kuna Hifadhi za taifa takribani 16 mpaka sasa! Hifadhi kubwa kuliko zote ni RUAHA NATIONAL PARK ikifuatiwa na SERENGETI NATIONAL PARK yenye ukubwa wa 14763km square
Kuna baadhi ya mkanganyiko na baadhi ya watu wakihusisha NGORONGORO kama hifadhi ya taifa, kwa ufupi NGORONGORO ni mbuga inayo simamiwa na mamlaka ya ngorongoro yaani NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY. Hii ni mbuga ambayo binadamu na wanyama huishi kwa pamoja chini ya sheria zilizowekwa.

Katika hifadhi izi kuna wanyama mbalimbali wakiwemo THE BIG FIVE ambao wote kwa pamoja wanapatikana SERENGETI,MKOMAZI,NGORONGORO na pori la akiba la SELOUS. Katika hifadhi nyingine mnyama ambaye hayupo sana ni FARU kwaiyo unaweza ukawapata THE BIG FOUR. Wanyama wengine wanaopatikana kwa uraisi ni logo ya Taifa letu (TWIGA), swala pala, punda milia, nyumbu, pofu, tohe, ngedere, tumbili, honey badger, buffalo, ngiri,bush baby, bweha,caracal,fisi mbwa mwitu, nguruwe pori, water buck, heartbeast, chimpanzee, duma,mamba, kiboko na wengine wengi siwez kuwataja wote

Lakini kuna ndege pia kama vile EAGLES, STORKS, STARLINGS, WEAVERS, VULTURES, BEE EATERS , KING FISHERS, HORN BILLS, OWLS, ROLLERS, na wengine wengi zaid ya species 900
pamoja na wadudu

KARIBUNI WADAU!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante.
1. Nimewahi sikia kwamba lion anaishi under kingdom. Yaan anaishi katika falme. Je simba anajuaje mipaka ya kingdom yake?

Nimewahi sikia kwamba honey burgers ni viumbe wenye wivu mkubwa wa kimapenzi. Yaan mfano dume akiwa njian na jike na gafla jani likagusa uchi wa jike basi honey Barger dume huanza kupambana na lile jani akiamini kwamba jani limefaidi sana. Je hizi story zinaukweli wowote?

sent using
 
Ahsante.
1. Nimewahi sikia kwamba lion anaishi under kingdom. Yaan anaishi katika falme. Je simba anajuaje mipaka ya kingdom yake?

Nimewahi sikia kwamba honey burgers ni viumbe wenye wivu mkubwa wa kimapenzi. Yaan mfano dume akiwa njian na jike na gafla jani likagusa uchi wa jike basi honey Barger dume huanza kupambana na lile jani akiamini kwamba jani limefaidi sana. Je hizi story zinaukweli wowote?

sent using
Asante kwa swali zuri!
Simba huwa kwa kawaida wanaishi katika makundi na kundi lao linaitwa "PRIDE" , katika kundi hilo kunakuwa na dominant Male ambae ndio kiongozi wa kundi! Kuhusu kujua mipaka, huwa wana mark territory kwa kutumia mikojo na vinyesi vyao! Kwaiyo akinusa anajua haya nd makao yangu.
simba hujitenga wakati wa kujamiina, dume na jike wakiwa kwenye kipindi cha joto huenda mbali na kundi kwaajili ya kupandana.
kwa kawaida wanaeza kukaa siku 5 hadi 7 wakiwa wanapandana, na katika hali hiyo huwa hawawindi wanakunywa tu maji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante.
1. Nimewahi sikia kwamba lion anaishi under kingdom. Yaan anaishi katika falme. Je simba anajuaje mipaka ya kingdom yake?

Nimewahi sikia kwamba honey burgers ni viumbe wenye wivu mkubwa wa kimapenzi. Yaan mfano dume akiwa njian na jike na gafla jani likagusa uchi wa jike basi honey Barger dume huanza kupambana na lile jani akiamini kwamba jani limefaidi sana. Je hizi story zinaukweli wowote?

sent using
Hiyo ni ukweli kuhusu honey badger! Na huyu ni moja ya wanyama ambao ni hatar lakink hawatajwi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una maana hapo kwenye kidonda amepigwa kofi sio kwamba ameng'atwa?

Kama utakuwa na ujuzi naomba unielekeze jinsi ya kufukuza wadudu kama nyoka wasikaribie makazi yangu.naishi nje ya mji.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
Kama ni nyoka unaweza kutumia njia za asili kama vile kuchoma matairi ya gari kwan harufu na moto havipatani kabisa! Hakikisha moshi una sambaa! Pia unaweza ukanyunyuzia mafuta ya taa sehemu unazohis zina nyoka! Pia punguza vichaka na msongamano wa vitu kama vile mawe na nguo!

Hakikisha unapokuwa sehemu za hatar uwe na jiwe la nyoka! Au unaeza kutumia shilingi mia au shilingi hamsini! Kwaiyo kama umeng'atwa unajifunga kuzuia damu alafu unaieka iyo pesa kwenye kidonda

Nyoka aina ya chatu huyu hana sumu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wanyama wachache wenye uwezo wa kutofautisha rangi {colour vision} wanya wengi hawana uwezo mkubwa wa kutofautisha rangi!

Mfano! Hapa ni jinsi binadam anavoona na kulia ni jinsi simba anavoona
FB_IMG_1547836989313.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ni nyoka unaweza kutumia njia za asili kama vile kuchoma matairi ya gari kwan harufu na moto havipatani kabisa! Hakikisha moshi una sambaa! Pia unaweza ukanyunyuzia mafuta ya taa sehemu unazohis zina nyoka! Pia punguza vichaka na msongamano wa vitu kama vile mawe na nguo!

Hakikisha unapokuwa sehemu za hatar uwe na jiwe la nyoka! Au unaeza kutumia shilingi mia au shilingi hamsini! Kwaiyo kama umeng'atwa unajifunga kuzuia damu alafu unaieka iyo pesa kwenye kidonda

Nyoka aina ya chatu huyu hana sumu

Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa sawa mkuu shukrani sana.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Je Tanzania inajua idadi ya wanyama waliopo nchini, mfano mbuga ya serengeti , sindo tunapakana na maasai mara kenya? Msimu wa kiangazi wanyama huhama kutoka mbuga A kwenda B kupitia mto/chanzo cha maji , huwa mnatumia vigezo gani kutoa takwimu za idadi ya wanyama wapatikanao serengeti ,.

NIPO TAYARI KUTEKEBISHWA KAMA NIMEKOSEA KATIKA UTAJAJI WA MBUGA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je Tanzania inajua idadi ya wanyama waliopo nchini, mfano mbuga ya serengeti , sindo tunapakana na maasai mara kenya? Msimu wa kiangazi wanyama huhama kutoka mbuga A kwenda B kupitia mto/chanzo cha maji , huwa mnatumia vigezo gani kutoa takwimu za idadi ya wanyama wapatikanao serengeti ,.

NIPO TAYARI KUTEKEBISHWA KAMA NIMEKOSEA KATIKA UTAJAJI WA MBUGA

Sent using Jamii Forums mobile app
Hujakosea ndugu! Idadi ya wanyama huwa inahesibiwa ila sio kwa wote! Mfano sensa ya mwisho idadi ya nyumbu wanao hama inakisiwa kuwa 1.5 milion na zebra zaid ya laki nne

Sensa hufanyika kwa kutenga kila eneo la mraba na wanafanya kwa kutumia magari, ndege ndogo na hata kwa miguu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom