Maalim Seif si amrudishie msajili figo yake yaishe

Maalim Seif si amrudishie msajili figo yake yaishe

Tee Bag

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
7,220
Reaction score
5,626
MAALIM SEIF SI AMRUDISHIE MSAJILI FIGO YAKE YAISHE?

KUNA mlevi alikuwa glasi nyingi kichwani. Nikashtukia kaja mezani kwangu. Akaniomba akae, nikamkatalia. Akaniambia: "Na wewe usiwe kama Msajili, unanichukia nina figo yako?" Nikamtolea macho kwa hasira!

Akasema: "Mimi shida yangu nikuulize swali moja tu... Hivi Maalim Seif alimchukulia nini Msajili?" Badala ya kujibu, nikamuuliza, kivipi?

Akaniambia: "Si unaona jinsi haziivi? Au Maalim alimchukulia Msajili figo yake? Si amrudishie amani iwepo? Vipi, walikutana anga zipi. Kama kuna chochote Maalim alimchukulia Msajili, bora amrudishie maana sasa ni too much!" Nikamuuliza sababu ya kusema hivyo.

Akanijibu: "Si unajua Maalim ndo alikuwa Don pale Cuf? Msajili akambeba Lipumba wakati alijiuzulu na kusepa. Mwisho Maalim akawa hana chake Cuf kwa nguvu ya Msajili. Maalim katimkia ACT-Wazalendo. Msajili kamfuata Maalim hukohuko na sasa anataka kuifuta ACT." Nikamjibu kuwa Msajili anafuata sheria.

Ooh, mlevi akawa mbogo: "Sheria inamshughulikia Maalim tu? Anasema ataifuta ACT kwa sababu ya hesabu za mwaka 2013, wakati mwaka huo ACT ilikuwa haijazaliwa. Mbona kabla Maalim hajahamia ACT, hiyo hoja ya mahesabu haikuwepo? Miaka yote hiyo, alipohamia Maalim tu ndo yameibuka haya." Hapa mlevi akanibana hasahasa!

Mlevi akacheka, halafu akasema: "Tangu vyama vingi vianze, hatujawahi kuona chama cha upinzani kinatetewa na Serikali kama Cuf ya Lipumba. ACT wanatishiwa kufutwa kwa hoja ya wanachama wao kuchoma bendera za Cuf ya Lipumba." Nikaona nimfukuze yule mlevi kwa ukali ili aondoke mbele yangu.

Akageuka aondoke, lakini akaniachia ujumbe: "Simpo tu mwanangu, kama Maalim alichukua figo ya Msajili amrudishie, vinginevyo atapata tabu sana. Au kama kuna anga walikutana, basi akamwangukie, maana Msajili anaonesha hataki mchezo. Anamwandama sana." Sikumjibu ili aondoke.

Kweli aliondoka lakini akarudi mbio: "Unaona sasa, Maalim anaiponza ACT. Unajua Yona alikuwa kimeo melini, alitupwa majini. Sisemi ACT wamtupe Maalim, ila nashauri kama kuna chochote alimchukulia Msajili, amrudishie. Hii vita inaonekana haiishi leo. Atamwandama kokote na hivi kuna sheria mpya!" Nikaona nizibe masikio. Mlevi alipoona simsikilizi akaondoka.

Ndimi Luqman MALOTO

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa, na ndio maana tunampora ushindi wake kila kipindi cha uchaguzi, dah ila jecha alicheza kama pele, bila kusahau policeccm nao wanatubeba sana hata wanajeshi wakati furani tunawapeleka kupiga kura ili kuongeza idadi japo hazitoshi mpaka jecha anajazilizia, sawa kada mwenzangu, mimi niko basement hapa lumumba kwenye mambo yetu yale.
Hamna lolote
Amesha pitwa na wakati
Kazeeka sana walahi


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ndio huyo mlevi..

However you may not start conversation with the following recipient;Tairus
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom