Tee Bag
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 7,220
- 5,626
MAALIM SEIF SI AMRUDISHIE MSAJILI FIGO YAKE YAISHE?
KUNA mlevi alikuwa glasi nyingi kichwani. Nikashtukia kaja mezani kwangu. Akaniomba akae, nikamkatalia. Akaniambia: "Na wewe usiwe kama Msajili, unanichukia nina figo yako?" Nikamtolea macho kwa hasira!
Akasema: "Mimi shida yangu nikuulize swali moja tu... Hivi Maalim Seif alimchukulia nini Msajili?" Badala ya kujibu, nikamuuliza, kivipi?
Akaniambia: "Si unaona jinsi haziivi? Au Maalim alimchukulia Msajili figo yake? Si amrudishie amani iwepo? Vipi, walikutana anga zipi. Kama kuna chochote Maalim alimchukulia Msajili, bora amrudishie maana sasa ni too much!" Nikamuuliza sababu ya kusema hivyo.
Akanijibu: "Si unajua Maalim ndo alikuwa Don pale Cuf? Msajili akambeba Lipumba wakati alijiuzulu na kusepa. Mwisho Maalim akawa hana chake Cuf kwa nguvu ya Msajili. Maalim katimkia ACT-Wazalendo. Msajili kamfuata Maalim hukohuko na sasa anataka kuifuta ACT." Nikamjibu kuwa Msajili anafuata sheria.
Ooh, mlevi akawa mbogo: "Sheria inamshughulikia Maalim tu? Anasema ataifuta ACT kwa sababu ya hesabu za mwaka 2013, wakati mwaka huo ACT ilikuwa haijazaliwa. Mbona kabla Maalim hajahamia ACT, hiyo hoja ya mahesabu haikuwepo? Miaka yote hiyo, alipohamia Maalim tu ndo yameibuka haya." Hapa mlevi akanibana hasahasa!
Mlevi akacheka, halafu akasema: "Tangu vyama vingi vianze, hatujawahi kuona chama cha upinzani kinatetewa na Serikali kama Cuf ya Lipumba. ACT wanatishiwa kufutwa kwa hoja ya wanachama wao kuchoma bendera za Cuf ya Lipumba." Nikaona nimfukuze yule mlevi kwa ukali ili aondoke mbele yangu.
Akageuka aondoke, lakini akaniachia ujumbe: "Simpo tu mwanangu, kama Maalim alichukua figo ya Msajili amrudishie, vinginevyo atapata tabu sana. Au kama kuna anga walikutana, basi akamwangukie, maana Msajili anaonesha hataki mchezo. Anamwandama sana." Sikumjibu ili aondoke.
Kweli aliondoka lakini akarudi mbio: "Unaona sasa, Maalim anaiponza ACT. Unajua Yona alikuwa kimeo melini, alitupwa majini. Sisemi ACT wamtupe Maalim, ila nashauri kama kuna chochote alimchukulia Msajili, amrudishie. Hii vita inaonekana haiishi leo. Atamwandama kokote na hivi kuna sheria mpya!" Nikaona nizibe masikio. Mlevi alipoona simsikilizi akaondoka.
Ndimi Luqman MALOTO
Sent using Jamii Forums mobile app
KUNA mlevi alikuwa glasi nyingi kichwani. Nikashtukia kaja mezani kwangu. Akaniomba akae, nikamkatalia. Akaniambia: "Na wewe usiwe kama Msajili, unanichukia nina figo yako?" Nikamtolea macho kwa hasira!
Akasema: "Mimi shida yangu nikuulize swali moja tu... Hivi Maalim Seif alimchukulia nini Msajili?" Badala ya kujibu, nikamuuliza, kivipi?
Akaniambia: "Si unaona jinsi haziivi? Au Maalim alimchukulia Msajili figo yake? Si amrudishie amani iwepo? Vipi, walikutana anga zipi. Kama kuna chochote Maalim alimchukulia Msajili, bora amrudishie maana sasa ni too much!" Nikamuuliza sababu ya kusema hivyo.
Akanijibu: "Si unajua Maalim ndo alikuwa Don pale Cuf? Msajili akambeba Lipumba wakati alijiuzulu na kusepa. Mwisho Maalim akawa hana chake Cuf kwa nguvu ya Msajili. Maalim katimkia ACT-Wazalendo. Msajili kamfuata Maalim hukohuko na sasa anataka kuifuta ACT." Nikamjibu kuwa Msajili anafuata sheria.
Ooh, mlevi akawa mbogo: "Sheria inamshughulikia Maalim tu? Anasema ataifuta ACT kwa sababu ya hesabu za mwaka 2013, wakati mwaka huo ACT ilikuwa haijazaliwa. Mbona kabla Maalim hajahamia ACT, hiyo hoja ya mahesabu haikuwepo? Miaka yote hiyo, alipohamia Maalim tu ndo yameibuka haya." Hapa mlevi akanibana hasahasa!
Mlevi akacheka, halafu akasema: "Tangu vyama vingi vianze, hatujawahi kuona chama cha upinzani kinatetewa na Serikali kama Cuf ya Lipumba. ACT wanatishiwa kufutwa kwa hoja ya wanachama wao kuchoma bendera za Cuf ya Lipumba." Nikaona nimfukuze yule mlevi kwa ukali ili aondoke mbele yangu.
Akageuka aondoke, lakini akaniachia ujumbe: "Simpo tu mwanangu, kama Maalim alichukua figo ya Msajili amrudishie, vinginevyo atapata tabu sana. Au kama kuna anga walikutana, basi akamwangukie, maana Msajili anaonesha hataki mchezo. Anamwandama sana." Sikumjibu ili aondoke.
Kweli aliondoka lakini akarudi mbio: "Unaona sasa, Maalim anaiponza ACT. Unajua Yona alikuwa kimeo melini, alitupwa majini. Sisemi ACT wamtupe Maalim, ila nashauri kama kuna chochote alimchukulia Msajili, amrudishie. Hii vita inaonekana haiishi leo. Atamwandama kokote na hivi kuna sheria mpya!" Nikaona nizibe masikio. Mlevi alipoona simsikilizi akaondoka.
Ndimi Luqman MALOTO
Sent using Jamii Forums mobile app