MSHINO
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,067
- 709
Mwaka 1988 Maalim Seif alifukuzwa CCM kutokana na mgogoro ndani ya chama.
- Kwa kipindi cha miaka 26 Maalim Seif Hamadi amepambana bila kuchoka, amechochea mageuzi makubwa ndani ya Tanzania.
- Maalim amepambana na vigogo wakubwa kwenye chaguzi za kisiasa tangu mwaka 1995 na kuwatoa jasho kweli kweli (Salmin Amour), mwaka 2000 na 2005 (Amani Karume, mtoto wa rais wa kwanza wa Zanzibar Abeid Karume), mwaka 2010 na 2015 (Dk. Ali Mohammed Shein).
- Amesababisha ushawishi wa chama cha ACT-Wazalendo kupanuka na kukua bara na Visiwani.
- Mafanikio makubwa ni matokeo ya jitihada zake katika siasa ni pamoja na kuleta umoja wa kitaifa, mpaka kufanikiwa kubairishwa kwa katiba ya Zanzibar kuwa na nafasi za makamu wawili wa rais wa Zanzibar.