Maajabu ya Tanzania

Sina uakika lakini Nigeria ndiyo nchi yenye watu wengi barani Afrika ikilingana na United States Of America yani watu wake ni million mia na hamsini (150) na siyo 300 maybe but this is what i know abaut Nigeria
 
Sasa mbona mnasema mnamuenzi Nyerere?
Kwa hiyo mnaenzi huo umaskini au?
Lakini upnda mwingine alikua safi elimu wote walisoma bure alafu ilikua bora, watu walikua wanatibiwa bure, Viwanda vingi wakati ule, UDA ilikuwepo tofauti na viongozi waliofatia almost wote wamefirisi viwanda vyote, Elimu imechakachuriwa, Matibabu sio bure tena, ufisadi kibao.
Sasa TZ imeendelea kwa wizi, rushwa, mauaji, ujambazi na kila aina ya uchafu mwingi upo TZ. Usimlaumu sana Nyere.
Viongozi waliofata walitakiwa kurekebisha makosa ya Nyerere sio kuongeza matatizo kama ilivyo sasa.
 

tatizo huyo dada sigara kali anamchukia nyerere huku akikiabudu chama cha nyerere
 

Unasemaje kwa Watanzania kuwa wachache kuliko Wanigeria? Hili ni swala mojawapo mtoa mada ameliongelea
 

Kuna mambo mengi uliyoandika sikubaliani na wewe.

Mwaka 1975 kweli uchumi wa Tanzania ulikuwa mzuri, kwa mwaka ule kutokana na bei ya kahawa kupanda sana baada ya kahawa ya Brazil kuungua kwa baridi 1974. Mwaka 1973 na 1974 uchumi wa Tanzania haukuwa mzuri kabia kutokana na kupanda sana kwa mafuta- Petroleum.

Hata kabla ya vita vya Amini mambo hayakuwa shwari sana. Vitu madukani mara nyingi vilikuwa vinakosekana hasa hasa, unga, mchele, mafuta ya kupikia, sabuni, n.k.

Nyerere aliondoka madarakani akiiacha Tanzania ikiwa hoi kwelikweli kiuchumi. Benki Kuu walikuwa hawana hata dollar millioni moja!

Alipoingia Mwinyi alikuta mambo mazito. Mwanzoni tu nchi nzima ilikuwa haina kabisa mafuta (hiki kilikuwa ni kitu cha kawaida wakati wa JKN). Ilibidi kusaini mkataba na Waarabu kubadilishani kahawa na mafuta. Mwinyi alijaribu kufungua uchumi wa Tanzania lakini walionufaika walikuwa ni wachache sana na kodi hazikulipwa. Tanzania ilibanwa sana na World Bank, IMF, na nchi wafadhili hasa kutokana na deni kubwa lililokuwa linaisonga Tanzania.

Mkapa alipoingia alijitahidi kulipa madeni kusudi angalau nchi ikopesheke. Ukata (Ukapa) uliumiza wengi lakini baada ya hapo madeni yalisamehewa madeni mengi. Migodi mingi ilifunguliwa na mashirika mengi yaliuzwa. Kwenye migodi kwa kweli Watanzania hawakunufaika sana lakini vile vile hili lilitokana na shinikizo la World Bank na IMF waliotaka Tanzania ifuate model ya nchi kama Chile. Uuzaji wa mashirika ulikuwa na matatizo yake lakini binafsi nakubaliana naye 100%. Mashirika na viwanda vilikuwa ni mzigo mkubwa kwa wananchi. NBC ilikuwa ni mzigo mkubwa kwa wananchi. Serikali ilikuwa haipati kodi kutoka NBC. Sana sana NBC ilikuwa mbele kuchangia mikutano ya NEC ya CCM kule KIzota na sherehe nyingin za chama. Afadhali ilikufa! Leo wanalipa kodi na serikali inapata gawio la faida.

Mkapa alifanaya vizuri sana sana katika kuinua uchumi wa Tanzania. Kikwete alipoingia madarakani alikuta mwanga na hewa safi katika uchumi wa Tanzania. Forex Reserves aliyoacha Mkapa ilikuwa kama USD 4 bn na Export zilikuwa juu kuliko alipochukua nchi.

Marais walioingia madrakani wakiwa na wakati mzuri ni Nyerere na Kikwete. Nyerere alichukua nchi ikiwa maskini lakini system zote zilikuwa zinafanya kazi. Kikwete amechukua nchi ikiwa katika hali afadhali kiuchumu kuliko wakata Mwinyi na Mkapa wanaingia madarakani.

Samahani kwa ujumbe mrefu.
 

Mwinyi alikuwa mwoga kidogo lakini aliweza kufanya mambo kinyume cha matakwa ya Nyerere japokuwa Nyerere alikuwa hapendi alikuwa anayamezea.

Mkapa vilevile alifanya mambo kinyume cha matakwa ya Nyerere kwa mfano kuwakumbatia WB na IMF na kubinafsisha mashirika na viwanda.

Kikwete amechukua nchi ikiwa tayari imeanza kujenga misingi mizuri ya Uchumi, tofauti na Mwinyi na Mkapa. Kikwete alichuka nchi ikiwa tayari ina Foreign Reserves kama USD 4bn hivi na Exports zikiwa kubwa. Mwinyi alichukua nchi wakati ina Forex Reserves zisizozidi dola millioni moja. Mkapa naye alichukua nchi kutoka kwa Mwinyi wakati uchumi wake ukiwa umedondoka kabisa.

Mafanikio ya Kikwete katika kujenga uchumi na miundo mbinu yanatokana na Foreign Reserves alizozikuta na misingi mizuri ya uchumi iliyowekwa na Mkapa.
 

Mazao gani ya kilimo? Sana sana Tanzania ilikuwa inasifika kwa zao la mkonge kwa dunia nzima. Zaidi ya hilo hakuna tena zao ambalo Tanzania ilikuwa inaongoza Afrika.
 


Viwanda vya Nyerere ilibidi lazima vifilisike. Kuna vilivyoanzishwa kwa kutaifisha na kupewa mameneja ambao walikuwa hawana elimu yeyote ya Biashara, achia uchungu wowote na hiyo mali. Hata viwanda vilivyoanzishwa na na serikali tatizo lilikuwa hilo hilo. Havikuendeshwa kibiashara. Afadhali yale mashirika na viwanda vimefilia mbali.

Kuhusu UDA kumbuka kuwa ilitokana na kutaifishwa kwa Dare es Salaam Motor Transport (DMT) na ndipo ilipozaliwa UDA na KAMATA. UDA na KAMATA yakageuka baadaye kuwa vichaka vya wavivu, wazembe, na wezi. Ilikuwa ni kitu cha kawaida kungojea basi la UDA kituoni kwa zaidi ya masaa matatu, hasa baadaya ya saa moja jioni.

Elimu bure, matibau bure, n.k. lakini havikuwa bure. Aliyekuwa naumia alikuwa mkulima wa Tanzania kwani ndiye aliyekuwa akinyonywa . Yeye bei za mazao yake zilipangwa na serikali bila kujali gharama za uzalishaji. Wakulima pole pole walianza kukata tamaa na ukosefu wa vyakula ukawa ni kitu cha kawaida. Ule uwanja wa Taifa kila mwaka ulikuwa unafurika na vyakula vya misaada - unga wa Yanga.

Elimu ilianza kudorora enzi za Nyerere. Unajua kitu kinaitwa Universal Primary Education? Kulitokea walimu wa UPE.

Wizi na ufisadi vilikuwepo hata enzi za Nyerere. Tofauti yake ni kuwa Nyerere alikuwa havifumbii macho tofauti na viongozi waliofuata hasa wa kipindi hiki.

Nyerere siyo Mungu. Alikuwa na mazuri mengi lakini na mapungufu vile vile.
 
unategemea mnachagua rais average minded kama jk uwe na maendeleo halafu wasaidizi wake ni malima,nchemba,lukuvi,nkamia,wasira,ghasia..na maprofesa njaa kama tibaijuka,muhongo,kapuya na wabunge akili mavi kama lusinde
 
Tuliosoma bure tumefaidika maana tulitumia vyema oppurtunity ile adimu.
Kama ulitegemea Nyerere aingie jikoni kwako hadi kukupikia basi una haki ya kulalamika maana upeo wako ulikuwa mdogo.
 

Hiyo elimu ya bure alitoa pesa mfukoni mwake? mimi sikusoma bure wazee wangu walikuwa wanalipa kodi.

Hayo matibabu ya bure ni yepi> hakuna cha bure, ni zile kodi walizokuwa wanalipa wazee wetu! na huo wakati wa Nyerere ndio wakati matibabu yalikuwa mabovu kabisa, Mtanzania alikuwa ana "life expectancy" ya miaka 38 tu.

Hayo niliyokuwekea nyekundu kajifunze namna ya kuyaandika sawa, hata kuandika hujajuwa halafu unataka kubishana?
 
Mazao gani ya kilimo? Sana sana Tanzania ilikuwa inasifika kwa zao la mkonge kwa dunia nzima. Zaidi ya hilo hakuna tena zao ambalo Tanzania ilikuwa inaongoza Afrika.

Nisome vizuri, ni nani kaitaja dunia nzima> au kwa upunguani wako "Afrika" ndio dunia nzima?

Amma kweli Watanzania tuna matatizo makubwa sana ya IQ zetu. Aliyesema tupo kwenye uwiano wa 72 namkatalia, mimi nna uhakika tupo kwenye 50.

Ikiwa ufahamu wenyewe ndio kama huo wako.
 

Tanzania foreign reserves 1985 = 16,000,000 - aliyoiacha Nyerere, aibu.
Tanzania foreign reserves 1995 = 270,203,522 - Mwinyi
Tanzania foreign reserves 2005 = 2,048,775,565 - Mkapa
Tanzania foreign reserves 2012 = 4,052,224,356 - Kubwa lao, na bado ana miaka 3 ya ku double hiyo figure.

Source: Total reserves (includes gold, current US$) | Data | Table

Kumbuka, siku nyingine uje na vitu valid, usifikiri wote humu JF ni mapunguani wenzako.


Huo ni uongo. Unajuwa unachokiandika lakini? au unahororoja tu.
 
Hiki ni kitu cha kawaida nadhani katika dini nyingi ikiwemo Uislamu, Hinduism, Budhism, n.k.

Sema hujui tu, hakuna kuabudu sanamu kwenye Uislam.

Hivi ukaliabudu sanamu, ambalo umelitengeneza mwenyewe kwa mikono yako, una akili kweli?
 
Unasemaje kwa Watanzania kuwa wachache kuliko Wanigeria? Hili ni swala mojawapo mtoa mada ameliongelea

Nimeshajibu juu huko, nisome vizuri. Lakini kwa uelewa wako nnavyousoma humu, nnamashaka kama utanielewa.
 
Lazima tusimame ili tuweze kuiondoa tz ya zamani yenye uchumi mbovu tujenge tz yenye uchumi bora kwa kuwaondoa viongozi wazee wenye siasi za karne ya mkoloni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…