Maajabu ya mchungaji Naijeria

Maajabu ya mchungaji Naijeria

moyafricatz

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2015
Posts
2,905
Reaction score
4,928
Pasta wa Kanisa la Covenant huko nchini Nigeria awaamurisha waumini wake wote wakati wa maombi ya usiku wavue nguo zao ili awaombee ndipo roho mtakatifu atawaingie kirahisi.

Baada ya waumini hao kutii agizo la kuvua nguo ndipo Pasta alianza kuomba na ghafula wakaanza kuanguka na kushindwa kujitambua, kisha Pasta akaanza kupita na kuwakanyaga.

Baadaye aliwaamuru waamuke na kuvaa nguo zao na kuendelea na ibada.
IMG-20180908-WA0008.jpg
IMG-20180908-WA0007.jpg
IMG-20180908-WA0006.jpg
IMG-20180908-WA0005.jpg
 
Kila kitu kikizidi kinakuwa na madhara yake walokole imani yao inatatizo sana hasa ukikutana na mchungaji muhuni , nakumbuka kuna mmoja alimrishwa na mchungaji wake ampe mkewe mchungaji maana sio sio chaguo lake na akatii
 
Makanisa ya kilokole ni vichaka vya wahuni...mbona hatusikii haya mambo .
Lutheran ..Moravian..Roma ..angrikana..na kadhalika..
 
Akili ni mali kila mtu ana zake
 
Wanaopitiwa na huu ulokole wengi wao ni wanawake
 
Makanisa ya kilokole ni vichaka vya wahuni...mbona hatusikii haya mambo .
Lutheran ..Moravian..Roma ..angrikana..na kadhalika..
Shida hujui hata neno la Mungu! Endelea kuhukumu Walokole tu! Kila mchungaji unamuiita Mlokole! Usihukumu ndugu yangu! Yesu mwenyewe alisema watakuja kutokea manabii waongo, sasa wewe unashangaa nini na unakuja kukurupuka kuwahukumu walokole wote! Hayo makanisa mengi wote ni wasafi? Soma sana neno la Mungu ndugu! Na umuombe Roho Mtakatifu akupe macho ya rohoni! Sio unaona baadhi ya wachungaji wanafanya mambo ya ovyo, halafu unakuja kiujumla kuwahukumu wengine!
 
Hoax na picha za kuunga unga!!!. Kwenye picha ya tatu hata proportion imewashinda. Ukimkalia mtu aliyelala chini huwezi kukaa posture ya namna hiyo. Nadhani ni makahaba walikamatwa na kukusanywa mahali usiku. Hata mwanga unavyomulika inaonekana unawalenga wao tu kwa dhumuni la kupata picha. Na picha ya pili kuna mmoja kafunika uso. Ila kwa kweli watengeneza hii hoax wamejitahidi kuunga unga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom