GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,646
- 10,859
Naona ni mtindo wa maisha wa kawaida tu. Hakuna maajabu. Unaweza kuliondoa neno maajabu kwenye story hii.1. Si kubwa kama jiji la Dar Es Salaam, lakini ningeambiwa nichague pa kuishi, ningepapendelea Kampala kutokana na hali yake ya hewa nzuri
2. Lugha ya Kiganda ndiyo imetawala kuanzia kwenye maredio na mitaani. Kizungu hutumika kinapojitajika
3. Kuna maeneo kuna Waswahili pia. Kuna mahali nimepita leo kwenye gesti moja nikakuta watu wanaongea Kiswahili. Nikipata muda nitaenda kuwauliza kama ni Watz au la. Kwenye ubao wa matangazo wa hiyo gesti, matangazo yamewekwa kwa lugha ya Kingereza na Kiswahili
4. Kuna mitaa pikipiki ni nyingi sana. Uliiona zikipita barabarani unaweza kufukiri zipo kwenye maadamano ya "chama"
6. Huenda boda boda wa huku nao wapo rafu katika uendeshaji pikipiki kama wa Bongo. Nimeshuhudia zikipuuzia kuzingatia taa za kuongozea magari. Ni tofauti na boda boda wa Kigali ambao inasemekana ni watiifu sana wa Sheria za barabarani
7. Inawezekana ndilo jiji la Afrika Mashariki linaloongoza kwa mabinti kuvaa vimini. Unakuta mwingine kimini chake ni kifupi sana kiasi kwamba akitaka kupanda boda boda inamlazimu awe na koti la kufunikia mapaja ili kujisitiri. Sijui ni utamaduni wao au ni "Uzungu" umewakolea?
8. Watu ni wachapa kazi. Ni kawaida kukuta maduka yaliyo pembezoni mwa mji yameshafunguliwa saa kumi na mbili Asubuhi, na muda huo mama lishe naye ameshaivisha chakula
9. Utamaduni wao kwenye matumizi ya Vyuo unaweza kuendana na Wakenya, ingawa Wakenya wanaweza wakawa "more advanced". Katika gesti kadhaa nilizolala, hakuna kopo la chooni wala toilet paper. Uzoefu wangu kwenye gesti za Kenya ni kwamba vyoo, hata vile vya umma(vya kulipa), lazima viwe na toilet paper. Lakini kwa Waganda sikuziona toilet paper wala kopo. Nazungumzia gesti za gharama nafuu na siyo mahoteli
10. Gesti za kawaida zinagharimu wastani wa Ugx 20,000 mpaka 30,000. Lakini ukienda nje ya mji, unaweza kupata mpaka Ugx 20,000 (self) na Ugx 13,000 (single)
11. Ndizi (matoke) ni chakula "common" huku
12. Wali wa huku ni kama pilau. Nimeshakula pilau zaidi ya mara moja, lakini mara zote nilipoagiza wali, nililetewa "pilau"
13. Kwa baadhi ya niliongea nao, hasa wale waliokwishafika Tanzania, wanaamini Serikali ya Tanzania inawajali raia wake kuliko ya Uganda😄. Mfano mojawapo waliotumia ni gharama za Internet. Wanadai internet ya Tanzania ni nafuu sana ukilinganisha na ya Uganda
14. Nimeshangazwa pia na chipsi mayai za huku. Chipsi kavu zilipashwa kivyake na mayai yakakaangwa kivyake. Sijui ndiyo kawaida ya huku au ni kwangu tu ndiyo waliamua kufanya hivyo!
NB. Ni "maajabu" kwangu tu ambaye bado "mgeni"
Kwenye Watanzania kuheshimika na kuunga mkono kwa asilimia zote, nakuunga mkono kwa asilimia zote. Uhamiaji hawakunihoji ipasavyo, ni kama vile walinitarajia kupita hapo muda niliopita.Kuhusu boda boda - hao ndo walianza hiyo Biashara na neno boda boda limetokea huko .
"SEKIDO"
Sebo - mwanume
Nyabo - mwanamke
Ichintu chomkazi
Kaunga kamuogo
Esente - PESA.
Kiganda ni moja ya lugha nzuri Sana Ina ladha fulani.
Nb kuhusu HIV/AIDS uwe makini wao wanaiita slim .
Na mwisho abarikiwe Nyerere watz wanaheshimika Sana
Kwa sababu kuna mambo sio rahisi kueleweka bongo, kama huo uvaaji wao wa vimini.Naona ni mtindo wa maisha wa kawaida tu. Hakuna maajabu. Unaweza kuliondoa neno maajabu kwenye story hii.
Ni maajabu kwa upande wangu mkuu. Wasukuma wanaita "cultural shock"Naona ni mtindo wa maisha wa kawaida tu. Hakuna maajabu. Unaweza kuliondoa neno maajabu kwenye story hii.
Ametoa ushamba au amechukua ushamba? Kampala nako ni pakutolea ushamba!?Haya,umeshatoa ushamba,,,,Rudi Tanzania [emoji1241] haraka
Nichangie nauli ya ticket ya ndege mkuu. Usafiri wa barabarani unachosha. Ukiniongezea laki mbili itanitosha.Haya,umeshatoa ushamba,,,,Rudi Tanzania 🇹🇿 haraka
Kwenye Watanzania kuheshimika na kuunga mkono kwa asilimia zote, nakuunga mkono kwa asilimia zote. Uhamiaji hawakunihoji ipasavyo, ni kama vile walinitarajia kupita hapo muda niliopita.
Bado hujazungumzia vyakula vyao maarufu mitaani Kama Kikomandoo (chikomandoo) na Rolex (chapati na mayai).1. Si kubwa kama jiji la Dar Es Salaam, lakini ningeambiwa nichague pa kuishi, ningepapendelea Kampala kutokana na hali yake ya hewa nzuri
2. Lugha ya Kiganda ndiyo imetawala kuanzia kwenye maredio na mitaani. Kizungu hutumika kinapohitajika
3. Kuna maeneo kuna Waswahili pia. Kuna mahali nimepita leo kwenye gesti moja nikakuta watu wanaongea Kiswahili. Nikipata muda nitaenda kuwauliza kama ni Watz au la. Kwenye ubao wa matangazo wa hiyo gesti, matangazo yamewekwa kwa lugha ya Kingereza na Kiswahili
4. Kuna mitaa pikipiki ni nyingi sana. Uliiona zikipita barabarani unaweza kufukiri zipo kwenye maadamano ya "chama"
6. Huenda boda boda wa huku nao wapo rafu katika uendeshaji pikipiki kama wa Bongo. Nimeshuhudia zikipuuzia kuzingatia taa za kuongozea magari. Ni tofauti na boda boda wa Kigali ambao inasemekana ni watiifu sana wa Sheria za barabarani
7. Inawezekana ndilo jiji la Afrika Mashariki linaloongoza kwa mabinti kuvaa vimini. Unakuta mwingine kimini chake ni kifupi sana kiasi kwamba akitaka kupanda boda boda inamlazimu awe na koti la kufunikia mapaja ili kujisitiri. Sijui ni utamaduni wao au ni "Uzungu" umewakolea?
8. Watu ni wachapa kazi. Ni kawaida kukuta maduka yaliyo pembezoni mwa mji yameshafunguliwa saa kumi na mbili Asubuhi, na muda huo mama lishe naye ameshaivisha chakula
9. Utamaduni wao kwenye matumizi ya Vyuo unaweza kuendana na Wakenya, ingawa Wakenya wanaweza wakawa "more advanced". Katika gesti kadhaa nilizolala, hakuna kopo la chooni wala toilet paper. Uzoefu wangu kwenye gesti za Kenya ni kwamba vyoo, hata vile vya umma(vya kulipa), lazima viwe na toilet paper. Lakini kwa Waganda sikuziona toilet paper wala kopo. Nazungumzia gesti za gharama nafuu na siyo mahoteli
10. Gesti za kawaida zinagharimu wastani wa Ugx 20,000 mpaka 30,000. Lakini ukienda nje ya mji, unaweza kupata mpaka Ugx 20,000 (self) na Ugx 13,000 (single)
11. Ndizi (matoke) ni chakula "common" huku
12. Wali wa huku ni kama pilau. Nimeshakula pilau zaidi ya mara moja, lakini mara zote nilipoagiza wali, nililetewa "pilau"
13. Kwa baadhi ya niliongea nao, hasa wale waliokwishafika Tanzania, wanaamini Serikali ya Tanzania inawajali raia wake kuliko ya Uganda😄. Mfano mojawapo waliotumia ni gharama za Internet. Wanadai internet ya Tanzania ni nafuu sana ukilinganisha na ya Uganda
14. Nimeshangazwa pia na chipsi mayai za huku. Chipsi kavu zilipashwa kivyake na mayai yakakaangwa kivyake. Sijui ndiyo kawaida ya huku au ni kwangu tu ndiyo waliamua kufanya hivyo!
NB. Ni "maajabu" kwangu tu ambaye bado "mgeni"
Hivi ushamba ndiyo ukoje lakini? Kama ni mtu aliyetoka shamba, basi mimi siwezi kuachana nao kwa sababu nikifika tu Tz, nitaenda kutumia siku kadhaa shambani kwangu kabla ya kuelekea "Mjini". Lakini kama ni "mshangao", sidhani kama utaniisha kwa sababu karibia kila ninakoenda, iwe Tz au kwingineko, sikosi vya kushangaa:Ametoa ushamba au amechukua ushamba? Kampala nako ni pakutolea ushamba!?
Duu kipande cha broadway Kawempe tuliinjoi sana ,kyungu=jiko,Amazi =maji,Kaunga(ugali),binjanjaro(maharage.janguu (njoo).Nimeanza sahau mengine ila kampala Naipenda kuliko darNimesoma huko Uganda shule moja inaitwa Eagle's Nest iko meko hapo Kati Kati ya jiji karibu na ikulu ya kabaka, miaka ya 2006 - 2009. Nilipapenda ug.
Kwangu Kampala ndo jiji namba moja. Manyabo wa kule Wana nyash za hataree.
Africa, Malawi mademu zao wanaongoza kwa ushamba wa kuvaa... Zambia pia wanavaa Sana vimini kama Afuganistan.Kuhusu vimini hata Africa magharabi nchi kama Ghana, Nigeria n.k wanavaa sana vimini mpaka nikawa najiuliza ndio kwanza vimeingia huku kwao au maana kitu kikiwa kigeni huvaliwa sana hata Bongo mwanzo ilikuwa hvyo.
Afghanistan wanavaa vimini? Sharia inaruhusu?Africa, Malawi mademu zao wanaongoza kwa ushamba wa kuvaa... Zambia pia wanavaa Sana vimini kama Afuganistan.
Joke tu mkuu,ila Ukivuka tu pale tunduma kuingia Zambia utaona tofauti,wanavaa vimini mno wazambiaAfghanistan wanavaa vimini? Sharia inaruhusu?
Mimi nafikiri suala la vimini ni utamaduni, pengine! Sijui ni Wanyankole au ni kabisa jingine la Kiganda, ambalo mavazi yao ya kimila yanaacha sehemu kubwa ya mwili wa mwanamke wazi. Mavazi kam hayo huyavaa kwenye shughuli za kiutamaduni kama ngoma n.k. Inawezekana wameathiriwa na huo utamaduni.Joke tu mkuu,ila Ukivuka tu pale tunduma kuingia Zambia utaona tofauti,wanavaa vimini mno wazambia