Maajabu Tanzania: Kutoka kuuza umeme nje ya nchi hadi kununua umeme 'cheap' toka Ethiopia

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,745
4,277
Kama kawaida yetu Tanzania tumebadili gia angani kwa mara nyingine.

Lengo la Serikali yetu tangu 2013 ni kuuza umeme nje ya nchi. Tena tulijipa mwaka tu hadi kutimiza lengo hili. Yaani tuliambiwa na Muhongo kuwa tutakuwa na Megawati 500 za ziada za kuwauzia majirani zetu wenye shida ifikapo 2014.

Rejea>> Tanzania kuuza umeme nje ya nchi kuanzia mwakani

Muhongo aliyasema hayo kitaalam kabisa akigusia mradi wa Kinyerezi na pia gesi ya Mtwara.

2014, Injinia Felchesmi Mramba alipeleka 'deadline' hadi 2016 na kusema tena kuwa tutauza umeme nje katika Mkutano Mkuu Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la TANESCO na kuongeza matumaini kuwa TANESCO imeshasaini mikataba ya kujenga njia za kusambaza umeme kwa nchi tatu za Afrika Mashariki.

Rejea>>Matumaini: Tanzania kuuza umeme nje ya nchi mwaka 2016

Sasa Mkuu wa nchi anaposema tutanunua umeme kutoka nje, anakuwa anatuchanganya.

Sawa bila umeme hatuwezi kuendesha viwanda vizuri lakini sisi sio wa kununua umeme toka nje, tunatakiwa kuwa na umeme extra.

Je, Megawati 500 za ziada zilizoahidiwa tangu 2013 ziko wapi hadi tunataka kununua Megawati 400 kutoka Ethiopia?? Gesi si tunayo au imeisha? Au tunanunua tu kwa sababu ni wa bei rahisi?

Inashangaza sana.
 
Even donor countries do take loans.. So sioni tatizo katika hili kabisa..
 
mambo yanabadilika mkuu, naona hapa ni mpango wa viwanda ndio umebadilisha hadi inatubidi tununue,
Mwanzoni tulikuwa tuna mpango wa kuuza sababu mipango ya viwanda haikuwepo, sasa kwa sababu Magufuli ataleta viwanda, na vitatumia umeme mwingi sana demand yetu ya umeme imebadilika hivyo inabidi tununue kutoka nje

Ni kama ulikuwa na ng'ombe mmoja na ukawa una mpango wa majani sababu yapo mengi, ila baada ya kubadili mipango na kuanza ng'ombe wengi inabidi uanze kununua majani wewe sasa...yo get the point?
 
wako busy na vi-wonder, Kigoma penyewe hakuna grid ya taifa umeme walionao sidhani kama unaweza kufanya uwekezaji wa viwanda.
Bora kawa mkweli kununua umeme Ethiopia na tumekubaliwa kufundishwa namna ya kukimbia kwa kasi ya 4G marathon :D:D
 
Kwani serikali inamaono? kinachowachanganya ni vyama vya upinzani tu. badala ya kuifikiria Tz miaka 50 ijayo wao wanafikiria namna ya kuwadhibiti wapinzani na kushinda uchaguzi wa 2020.
 
mambo yanabadilika mkuu, naona hapa ni mpango wa viwanda ndio umebadilisha hadi inatubidi tununue,
Mwanzoni tulikuwa tuna mpango wa kuuza sababu mipango ya viwanda haikuwepo, sasa kwa sababu Magufuli ataleta viwanda, na vitatumia umeme mwingi sana demand yetu ya umeme imebadilika hivyo inabidi tununue kutoka nje

Ni kama ulikuwa na ng'ombe mmoja na ukawa una mpango wa majani sababu yapo mengi, ila baada ya kubadili mipango na kuanza ng'ombe wengi inabidi uanze kununua majani wewe sasa...yo get the point?
Viwanda viko wapi?
 
Kama mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam hajulikani jina lake ni nani lakini bado wizara ya fedha inaingiza mshahara kwenye akaunti zenye jina tata,inaonyesha hawa jamaa ni vinyonga kiasi gani

Kama wakili wa ccm kule dodoma wakati anasoma alikuwa anaitwa elia William leo anaitwa godfrey wasonga na hata uraia wake ni tata

Sishangai hawa jamaa kuwa ndimi Mbili
 
hujaelewa, viwanda vitaanzishwa, sasa wenyewe wame project viwanda vitakavyoanzishwa na umeme utakaokuwepo nchini, hautatosha ndio maana wanajipanga kununua
Mkuu bado umelala?

Kuna wale wanaoota ndoto wanatembea,akianza kuota saa tatu asubuhi,msiposhtuka mtamkuta norogoro
 
Anayejua rais Magufuli anatupeleka wapi naomba atuambie, naona kama vile tumepotea.
 
1. Tanzania kuuza umeme nje ya nchi...tuna gesi mita za ujazo zaidi ya trilioni 3000 (Prof. Mwongo).
2. Tanzania kununua Umeme wa bei Nafuu kutoka Ethiopia (Prof. Mwongo, Magufuli). 3.Tanzania kumaliza kabisa Tatizo la umeme baada ya ugunduzi na kuanza kutumika kwa gesi (Ngeleja).
4. Tanzania kuanza kusambaza gesi ya kupikia majumbani kupunguza matumizi ya Mkaa (Prof. Mwongo)

'Uprofesa siku hizi ni wa ovyooo kweli'.
 
Ndio matatizo ya kuongozwa na CCM haya. Watanzania kwa sasa hatuelewi tunakwenda wapi. Rais ana mipango yake ,bunge ya kwake na watendaji nao na mipango yao.
 
hujaelewa, viwanda vitaanzishwa, sasa wenyewe wame project viwanda vitakavyoanzishwa na umeme utakaokuwepo nchini, hautatosha ndio maana wanajipanga kununua
Hivyo viwanda vitaanzishwa lini? Ni viwanda vya kutengeneza nini? Kuna wataalamu wameandaliwa kwa ajili ya kufanya kazi kwenye hivyo viwanda? Kuna masoko yameandaliwa kwa ajili ya kufanya biashara hiyo?
 
Back
Top Bottom