Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Wakati NEC imetoa maelekezo ya kuwa wapigakura tuna uhuru wa kuwa mita 100 kutoka vituo vya kupiga kura na mapolisi wasitusumbue utata umejitokeza pale ambapo msimamizi wa uchaguzi wa Tarime alipoagiza kuwa wapigakura waishie majumbani kwao mara baada ya uchaguzi.
Kauli hii ya huyu msimamizi inakinzana na maagizo ya NEC yaliyotolewa hivi majuzi na Naibu Mwenyekiti wa NEC pale alipokuwa anajibu swali la mgombea ubunge jimbo la Bukoba Mjini Bw. Rwakatare.
NEC inaelekea maagizo yake bado hayajawafikia watendaji wake huko kwenye majimbo au wasimamizi wa uchaguzi wanabeza maelekezo ya mabosi wao. Hili linawezekana kabisa kutokana na NEC kuwatumia waajiriwa wa muda kutoka serikali za mitaa ambao hawana sauti juu ya ajira zao.
Inawezekana kabisa wasimamizi hawa wanapokea maagizo kutoka viongozi serikalini wagombeaji na wenye mkakakati wa kuchakachua matokeo ......
Kauli hii ya huyu msimamizi inakinzana na maagizo ya NEC yaliyotolewa hivi majuzi na Naibu Mwenyekiti wa NEC pale alipokuwa anajibu swali la mgombea ubunge jimbo la Bukoba Mjini Bw. Rwakatare.
NEC inaelekea maagizo yake bado hayajawafikia watendaji wake huko kwenye majimbo au wasimamizi wa uchaguzi wanabeza maelekezo ya mabosi wao. Hili linawezekana kabisa kutokana na NEC kuwatumia waajiriwa wa muda kutoka serikali za mitaa ambao hawana sauti juu ya ajira zao.
Inawezekana kabisa wasimamizi hawa wanapokea maagizo kutoka viongozi serikalini wagombeaji na wenye mkakakati wa kuchakachua matokeo ......