Maafisa wa Afya watakiwa kuhuisha leseni zao kabla ya Machi 5, 2022

Kasomi

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
11,036
20,337
Maafisa Afya nchini wametakiwa kurejesha upya (renew) leseni zao kabla ya Machi 5 mwaka huu na hatua kali zitachukuliwa kwa atakayekiuka agizo hilo ikiwemo kufutiwa usajili.

Hayo yamesemwa na Msajili wa Baraza la Afya Mazingira Iddi Hoyange katika kikao cha Baraza la Afya kilichofanyika mkoani Morogoro.

Hoyange amesema endapo mwanataaluma atafutiwa usajili ni wazi kwamba hawezi kutekeleza tena majukumu ya Afisa Afya nchini

Aidha, amewataka wadaiwa wote kukamilisha malipo ya usajili ili kuepuka kufungiwa baada ya kufika muda huo wa mwezi mmoja.

Hoyange amesema Baraza limefanikiwa kupitisha muongozo wa maadili kwa maafisa Afya nchini kwa kufanyiwa marekebisho kwa lugha ya kiingereza na kutaka kila mwanataaluma kufuata miongozo iliyowekwa.

Hoyange amesema hadi kufikia kikao kingine cha baraza hilo kinachotarajia kufanyika baada ya miezi minne utakua umetafsiriwa kwa lugha ya kiswahili ili iwe rahisi kusomeka na kueleweka kwa wadau wote.

Imetolewa na;
Wizara ya Afya Tanzania
 
Serikali inatumia nguvu sana kupuruni wataalamu wa afya kwa mbinu tofaut tofauti,, kila kukicha vigezo vinakuwa vingi ,, Tena kwa lazima taka usitake.

Imagine mtu amepata license ya kazi,, amekaa nayo bila kuitumia ( kwa kuwa ajira ni ngumu), Bado unamlazimisha arenew Tena bila kujali ana ajira au laah!!

Tunajua, serikali inakusanya mapato kupitia mabaraza ya wataalamu wa afya kwa mgongo wa license,, lakini sometimes zingatieni utu,, !!

Ni bora serikali ikapuruni vyuo vya taaluma za afya,, kuliko kudeal na waliohitimu ili kuwaangamiza bila kujali gharama walizozitumia kuwekeza kwenye taaluma hizo.
 
Waanze Kulipia Na Vyeti vya Sekondari na Chuo vilivyopo makabatini sasa.
Tunakoelekea ni huko,, hii sector ya afya hususan Madaktari wameandamwa kweli kweli!!

Sector zote waanzishiwe utaratibu wa license nao walipie,,, na Kama shida ni ongezeko la wahitimu wasio na kazi,, Dawa sio kupandisha vigezo kwa wahitimu,, Dawa ni kufunga license za vyuo vinavyotoa taaluma hiyo na kuvifuta kabisa
 
Back
Top Bottom