Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,988
Wadau mbalimbali wa Kada za Afya wametoa malalamiko yao wakiomba Mabaraza ya taaluma ya kada hizo kurejea upya miongozo mbalimbali ya utozaji wa pesa hasa kwa vijana wa kada hizo wasio na ajira.
Mdau mmoja ambaye ni Afisa Tabibu (Clinical Officer) ameeleza kuwa wao hutozwa Tsh. 300,000/= kila mwaka pasipo kujali una ajira au la kwa utaratibu ufuatao-
Pia, mdau mwingine wa Kada ya Famasi ngazi ya shahada (Pharmacist) ameeleza kuwa Baraza lao hutoza Tsh. 320,000/= kwa kila mwanafunzi aliyefaulu ili aweze kupata usajili wa kudumu. Aidha, Tsh. 150,000/= hulipwa kila mwisho wa mwaka kama ada ya kuhuisha leseni ili waendelea kubaki kwenye rejesta ya msajili.
Uchunguzi ambao JamiiForums imeufanya umebaini kuwa kada nyingi za Afya zimeyapa mabaraza ya kitaaluma nguvu ya kusajili, kufuta na kufuatilia mienendo ya wanataaluma wake, ambapo hata michango hii inayotajwa hulipwa huko.
Wadau waeleza kuwa kwenye kada za afya, kigezo cha kwanza kupata ajira inabidi uwe na leseni hai (Active licence to practice). Je, kwa ambao hawajapata ajira watawezaje kuajiriwa pamoja na kumudu gharama za kulipia huduma hizi kila mwaka ili waendelee kutambuliwa na mabaraza yao kama wanachama hai?
Wanaomba utaratibu huu ufanyiwe marekebisho, waanze kulipia leseni na kuzihuisha baada ya kupata ajira ili waweze kujimudu kiuchumi.
Wamesema kumtoza mtu gharama kwa huduma ambayo hajatumia ni unyonyaji, pia ni kikwazo kikubwa kwa vijana wasio na ajira kwa kuwa kila nafasi inayotangazwa huwadai wawe wanachama hai kabla hata hawajaanza kutumikia taaluma hiyo.
Mdau mmoja ambaye ni Afisa Tabibu (Clinical Officer) ameeleza kuwa wao hutozwa Tsh. 300,000/= kila mwaka pasipo kujali una ajira au la kwa utaratibu ufuatao-
- Enrollment registration Tsh 75,000/=
- Renewal practicing license Tsh 75,000/=
- Pending debt Tsh 150,000/= ambayo amesema hawaelewi humaanisha nini.
Pia, mdau mwingine wa Kada ya Famasi ngazi ya shahada (Pharmacist) ameeleza kuwa Baraza lao hutoza Tsh. 320,000/= kwa kila mwanafunzi aliyefaulu ili aweze kupata usajili wa kudumu. Aidha, Tsh. 150,000/= hulipwa kila mwisho wa mwaka kama ada ya kuhuisha leseni ili waendelea kubaki kwenye rejesta ya msajili.
Uchunguzi ambao JamiiForums imeufanya umebaini kuwa kada nyingi za Afya zimeyapa mabaraza ya kitaaluma nguvu ya kusajili, kufuta na kufuatilia mienendo ya wanataaluma wake, ambapo hata michango hii inayotajwa hulipwa huko.
Wadau waeleza kuwa kwenye kada za afya, kigezo cha kwanza kupata ajira inabidi uwe na leseni hai (Active licence to practice). Je, kwa ambao hawajapata ajira watawezaje kuajiriwa pamoja na kumudu gharama za kulipia huduma hizi kila mwaka ili waendelee kutambuliwa na mabaraza yao kama wanachama hai?
Wanaomba utaratibu huu ufanyiwe marekebisho, waanze kulipia leseni na kuzihuisha baada ya kupata ajira ili waweze kujimudu kiuchumi.
Wamesema kumtoza mtu gharama kwa huduma ambayo hajatumia ni unyonyaji, pia ni kikwazo kikubwa kwa vijana wasio na ajira kwa kuwa kila nafasi inayotangazwa huwadai wawe wanachama hai kabla hata hawajaanza kutumikia taaluma hiyo.