Ma-IT wa NECTA mjitathmini

Ma-IT wa NECTA mjitathmini

Shebbydo

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2015
Posts
1,174
Reaction score
1,937
Habari Wandugu

Ni matumaini yangu mu wazima.
Ni jana tarehe 08/01/2018, baraza la mitihani la taifa lilitangaza matokeo ya upimaji ya kidato cha pili na darasa la nne. Mimi pia nikiwa ni mdau wa elimu, nikaona vyema niingie kwenye website yao niangalie maendeleo ya vijana wetu. Jambo la kushangaza tangu jana majira ya saa kumi jioni mpaka sasa naandika uzi huu sijaweza kuingia kwenye website ya NECTA. Majibu ni "the site you are requesting can't be reached". Maana yake nini; yawezekana website hii ipo katika marekebisho au imedukuliwa na kufungiwa na washenzi.

Hii ni aibu kwa wataalam wa IT wa taasisi hii. Wanajisikia je Watanzania wanapohangaika ku-access website yao. Kama hampo vizuri kwenye IT security ni bora kuleta watu wenye uwezo mkubwa ili kupambana na changamoto za IT. IT si lelema, inabidi kuwa current haswa kwa sababu hizi ndizo zama zake, kila siku kuna mbinu na utaalam mpya. Sasa kama nyinyi mmejifungia tu huko maofisini na kula viyoyozi mtateswa na hackers.

Ni bora nimesema kuliko kubaki na maumivu.
 
Habari Wandugu

Ni matumaini yangu mu wazima.
Ni jana tarehe 08/01/2018, baraza la mitihani la taifa lilitangaza matokeo ya upimaji ya kidato cha pili na darasa la nne. Mimi pia nikiwa ni mdau wa elimu, nikaona vyema niingie kwenye website yao niangalie maendeleo ya vijana wetu. Jambo la kushangaza tangu jana majira ya saa kumi jioni mpaka sasa naandika uzi huu sijaweza kuingia kwenye website ya NECTA. Majibu ni "the site you are requesting can't be reached". Maana yake nini; yawezekana website hii ipo katika marekebisho au imedukuliwa na kufungiwa na washenzi.

Hii ni aibu kwa wataalam wa IT wa taasisi hii. Wanajisikia je Watanzania wanapohangaika ku-access website yao. Kama hampo vizuri kwenye IT security ni bora kuleta watu wenye uwezo mkubwa ili kupambana na changamoto za IT. IT si lelema, inabidi kuwa current haswa kwa sababu hizi ndizo zama zake, kila siku kuna mbinu na utaalam mpya. Sasa kama nyinyi mmejifungia tu huko maofisini na kula viyoyozi mtateswa na hackers.

Ni bora nimesema kuliko kubaki na maumivu.
Sio kwamba imedukuliwa la hasha, ni kwamba watu walipopata taarifa kuwa matokeo yametoka basi watu wote wakaanza kuifungua hiyo website ili waweze kuangalia hayo matokeo, sasa kinachotokea ni kwamba website inazidiwa uwezo wa kutoa huduma kwa watu wengi kwa wakati mmoja ndio maana unaona ukijaribu kuingia kwenye hiyo site unapata huo ujumbe. walichotakiwa kufanya hao jamaa ni kuyaweka hayo matokeo sehemu tofauti tofauti, mfano wangeweza kuweka na kwenye website ya wizara ya elimu, ili kupunguza idadi ya watu.
 
Ukweli waone aibu, wanashindwa kuhandle traffic ya Tanzania ilivyo ndogo.
Mimi nina server zinahandle million requests kwa sekunde moja bila tatizo, kama NECTA kushindwa watu elfu chache kwa sekunde ni aibu, ile ni institution inayotakiwa kuchukuliwa serious sana ila wanafanya mzaa tu.
 
Wana server chache sana....halafu wanaona ni upotevu wa pesa kuongeza server ambazo zinatumika mara moja kwa mwaka wakati wa matokeo tu
 
Sio kwamba imedukuliwa la hasha, ni kwamba watu walipopata taarifa kuwa matokeo yametoka basi watu wote wakaanza kuifungua hiyo website ili waweze kuangalia hayo matokeo, sasa kinachotokea ni kwamba website inazidiwa uwezo wa kutoa huduma kwa watu wengi kwa wakati mmoja ndio maana unaona ukijaribu kuingia kwenye hiyo site unapata huo ujumbe. walichotakiwa kufanya hao jamaa ni kuyaweka hayo matokeo sehemu tofauti tofauti, mfano wangeweza kuweka na kwenye website ya wizara ya elimu, ili kupunguza idadi ya watu.
Sidhani kama unachosema ni kweli. Mwanzo nilidhani hivyo, nikajipa kazi kuvizia usiku muda ambao nilijua hata kama ni jam basi itakuwa imeisha lakini tatizo lipo pale pale. Hata kama hiyo ingekuwa ni sababu bado ni IT ya ubabaishaji. Wewe unafikiri ni watu wangapi wanaingia facebook kwa sekunde moja?
 
Sidhani kama unachosema ni kweli. Mwanzo nilidhani hivyo, nikajipa kazi kuvizia usiku muda ambao nilijua hata kama ni jam basi itakuwa imeisha lakini tatizo lipo pale pale. Hata kama hiyo ingekuwa ni sababu bado ni IT ya ubabaishaji. Wewe unafikiri ni watu wangapi wanaingia facebook kwa sekunde moja?
Kwa hiyo unahisi wewe peke yako ndio unaweza kuvizia usiku, facebook ni kitu kingine kabisaaaa, huwezi linganisha hapoo, hilo ni kosa, hapo unafanya uonevu mkubwa sana kulinganisha hivyo.
 
Sidhani kama unachosema ni kweli. Mwanzo nilidhani hivyo, nikajipa kazi kuvizia usiku muda ambao nilijua hata kama ni jam basi itakuwa imeisha lakini tatizo lipo pale pale. Hata kama hiyo ingekuwa ni sababu bado ni IT ya ubabaishaji. Wewe unafikiri ni watu wangapi wanaingia facebook kwa sekunde moja?
mimi pia jana nimekesha usiku kuccha natafuta kuangalia hiyo website nimeshindwa kuna kipindi saa tisa usiku nili-access mpk jina la shule ila haikufunguka baada ya hapo
 
Ukweli waone aibu, wanashindwa kuhandle traffic ya Tanzania ilivyo ndogo.
Mimi nina server zinahandle million requests kwa sekunde moja bila tatizo, kama NECTA kushindwa watu elfu chache kwa sekunde ni aibu, ile ni institution inayotakiwa kuchukuliwa serious sana ila wanafanya mzaa tu.
hii kitu ni balaa, aina gani hizo
 
Labda wameshutdown temporarily huku wana upload hayo matokeo
 
Sio Necta tu bali tofuti kama Tamisemi, moe Tcu, heslb huwa zinajam wakati wa matukio maalumu. Hawa ma IT wetu pendwa wa serekali dah
 
Wanachosha sana hawa NECTA hata website tu haifunguki . Uzembe wenu unatia aibu
 
Habari Wandugu

Ni matumaini yangu mu wazima.
Ni jana tarehe 08/01/2018, baraza la mitihani la taifa lilitangaza matokeo ya upimaji ya kidato cha pili na darasa la nne. Mimi pia nikiwa ni mdau wa elimu, nikaona vyema niingie kwenye website yao niangalie maendeleo ya vijana wetu. Jambo la kushangaza tangu jana majira ya saa kumi jioni mpaka sasa naandika uzi huu sijaweza kuingia kwenye website ya NECTA. Majibu ni "the site you are requesting can't be reached". Maana yake nini; yawezekana website hii ipo katika marekebisho au imedukuliwa na kufungiwa na washenzi.

Hii ni aibu kwa wataalam wa IT wa taasisi hii. Wanajisikia je Watanzania wanapohangaika ku-access website yao. Kama hampo vizuri kwenye IT security ni bora kuleta watu wenye uwezo mkubwa ili kupambana na changamoto za IT. IT si lelema, inabidi kuwa current haswa kwa sababu hizi ndizo zama zake, kila siku kuna mbinu na utaalam mpya. Sasa kama nyinyi mmejifungia tu huko maofisini na kula viyoyozi mtateswa na hackers.

Ni bora nimesema kuliko kubaki na maumivu.
Wanamchosha Rais. Inawezekana hawajui kile anachokitaka Rais wetu.
 
Kiukweli ni aibu kwa IT wa Necta. Wenye watoto na wadau wa elimu toka jana hatujaweza kuaccess matokeo.
 
Wana server chache sana....halafu wanaona ni upotevu wa pesa kuongeza server ambazo zinatumika mara moja kwa mwaka wakati wa matokeo tu

Usiseme chache, nahisi wanayo moja alafu ndogo mno ya zamani.
Kuhandle watu elfu 10, 20 kwa sekunde moja haihitaji hata server kumi, server moja tu inatosha kabisa, weka 4GB RAM, cache data zote kwenye memory, CPU 2 tu zinatosha kuhandle watu wote hao kwa sekunde bila tatizo lolote sababu data inayoflow pale ni ndogo mno na schema yake ni nyepesi. Hakuna hata relationship yoyote between data, yaani ni kuchagua shule au namba, unapata matokeo moja kwa moja, aibu mno.

Hata wakiwa tuseme watu laki tano kwa sekunde kitu ambacho sidhani coz hakuna site bongo inapata watu wote hao kwa sekunde hata facebook, caching results zote kwenye memory unaweza handle watu wote hao kwa machine moja kabisa bila tatizo. Schema ya matokeo ni rahisi mno kuifanyia caching, yaani hiyo kazi haihitaji hata watu wawili, moja tu anaweza kuifanya vizuri mno. Miaka kadhaa sasa matokeo yakitoka necta inakua very busy, niliona jamaa flani waliotengeneza hii system kama miaka 5 iliyopita walikua wako shallow balaa, sijui kama walibadilisha system wakaweka watu wengine toka enzi hizo.
 
Usiseme chache, nahisi wanayo moja alafu ndogo mno ya zamani.
Kuhandle watu elfu 10, 20 kwa sekunde moja haihitaji hata server kumi, server moja tu inatosha kabisa, weka 4GB RAM, cache data zote kwenye memory, CPU 2 tu zinatosha kuhandle watu wote hao kwa sekunde bila tatizo lolote sababu data inayoflow pale ni ndogo mno na schema yake ni nyepesi. Hakuna hata relationship yoyote between data, yaani ni kuchagua shule au namba, unapata matokeo moja kwa moja, aibu mno.

Hata wakiwa tuseme watu laki tano kwa sekunde kitu ambacho sidhani coz hakuna site bongo inapata watu wote hao kwa sekunde hata facebook, caching results zote kwenye memory unaweza handle watu wote hao kwa machine moja kabisa bila tatizo. Schema ya matokeo ni rahisi mno kuifanyia caching, yaani hiyo kazi haihitaji hata watu wawili, moja tu anaweza kuifanya vizuri mno. Miaka kadhaa sasa matokeo yakitoka necta inakua very busy, niliona jamaa flani waliotengeneza hii system kama miaka 5 iliyopita walikua wako shallow balaa, sijui kama walibadilisha system wakaweka watu wengine toka enzi hizo.
Hili tatizo hata website ya jkt ni hivyo hivyo yani yakitoka majina ya vijana wa kujitolea inaweza maliza siku hata nne haifunguki....sijui website za serikali zina shida gan
 
Back
Top Bottom